JanguKamaJangu
JF-Expert Member
- Feb 7, 2022
- 2,308
- 5,460
Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi, Dkt Allan Kijazi amesema Dodoma kuna migogoro mingi ya ardhi na imekuwa ikisababishwa na uelewa mdogo kuhusu sheria, taratibu na kanuni zinazohusu masuala ya ardhi na kusababishwa wananchi wengi kukosa haki.
Amesema: "Changamoto ni nyingi lakini tunaendelea kuzifanyia kazi kwa kushirikiana na mamlaka zinazohusika nina imani baada ya muda sehemu kubwa ya malalamiko ya wananchi ambayo tumepokea yatapatiwa ufumbuzi.
"Tunachokifanya ni kuboresha mifumo ya kupanga, kupima na kurasimisha, tumepata fedha (Tsh.) bilioni 50 ambazo tunashirikiana na Halmashauri na majiji ili kubaini maeneo ambayo yanafaa kwa ajili ya mwendelezo wa makazi.
Source: EATV
Amesema: "Changamoto ni nyingi lakini tunaendelea kuzifanyia kazi kwa kushirikiana na mamlaka zinazohusika nina imani baada ya muda sehemu kubwa ya malalamiko ya wananchi ambayo tumepokea yatapatiwa ufumbuzi.
"Tunachokifanya ni kuboresha mifumo ya kupanga, kupima na kurasimisha, tumepata fedha (Tsh.) bilioni 50 ambazo tunashirikiana na Halmashauri na majiji ili kubaini maeneo ambayo yanafaa kwa ajili ya mwendelezo wa makazi.
Source: EATV