Mwanahabari Huru
JF-Expert Member
- Mar 9, 2015
- 14,243
- 34,899
Katibu wa Kanda ya Kaskazini Mhe.Amani Golugwa akiwa ameambatana na Naibu Mstahiki Meya wa Jiji la Arusha Mhe.Viola Likindikoki, leo Aprili 7, 2018 wamehudhuria maadhimisho ya kumbukumbu za Mauaji ya kimbari yaliyotokea Rwanda 1994 (GENOCIDE AGAINST THE TUTSI IN RWANDA 1994).
Maadhimisho hayo yaliyofanyika katika Makao Makuu ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC Arusha Headquarters), yalihudhuriwa na wawakilishi kutoka jumuiya mbalimbali za kimataifa wakiwemo Mabalozi, Wabunge wa EALA na wawakilishi kutoka taasisi za kimataifa.
Wito mkubwa katika maadhimisho ya mwaka huu ambapo watu zaidi ya 1,000,000 waliuawa kinyama imekuwa ni Kukumbuka, Kuungana, Upya (Remember, Unite, Renew) na kuwa mauaji ya namna hii yasitokee Tena Rwanda, Afrika Mashariki na Dunia kwa ujumla.