AirTanzania
JF-Expert Member
- Mar 17, 2011
- 1,139
- 1,033
Mpaka 2015 Chama Chama Magamba atakuwa amebakia Fisadi wa Magogoni na House boy wake Nape pamoja na Majambazi
Wakuu magamba yanazidi kupata moto. Katibu mwenezi wa vijana wilaya ya Longido Ndugu YOHANA LAIZER ameamua kuhama ccm na bado hajaweka wazi atajiunga na chama gani. Katibu huyo anadai kachoshwa na magamba kuchanganya siasa na mila.
Pia anadai magamba wamekuwa wakidanganya wananchi kuwa alama nyekundu iliyopo kwenye bendera ya CDM inaonyesha kuwa ni chama cha hatari hivi wasijiunge nacho.
Pia imefika mahali wanatumia viongozi wa jamii ya Kimaasai kuwalaani watakaojiunga na Upinzani. Chanzo mahojiano na Sunrise Radio. Na bado!! Nawasilisha!
Huyu dogo amesema kweli, leo nimeona gazeti la jambo leo limeandika Cdm ni chama cha freemason. Wameweka picha za viongozi wa nchi flani flani wanaonyesha alama ya vidole viwili. Pia wamemweka hadi papa benedicto wa 16. Wameandika Dr. Slaa ana jini sebuleni. Ki ukweli leo nimejisikia vibaya kuona zile habari ila kwa sababu najua jambo leo ni gazeti la serikali nikajua ni mkakati wao wa kuidhoofisha Cdm ambapo hata hawawezi. Gazeti la jamba leo ni uchafu kabisa. Huyu dogo wa Longindo ndo atamwondoa Lekule Laizer welcome kijana.
Saaa ya ukombozi ni sasa
KORIANGA ni muda wao kushika hatamu. Wazee wote wakapumzike.