Katibu Mkuu TFF na Msemaji wa Yanga warushiana maneno mazito na ya kashfa Clouds fm

Huyu
Usitoe habari ili watu wakushangae wew mtoa habari jitahidi watu washangae habari yenyewe.unaongea vitu ambavyo avipimiki unajua kuna maneno ukiyatamka sehemu watu wanapima na kujua namna gani ulivokuwa waki.wewe unahisi shafii au clouds wanajua nini cha kusema leo kila wanalosema uliamini.na pia mtu anatoa clip ya uyo jamaa ili watu wafanyaje sasa unajua usiwajenge fikra watu kwa mambo ya kubuni
Haya yanarudiwa tu hapa mkuu. Tumemsikia msemaji wa yanga kwenye kipindi cha sports round up cha kila jumapili kiukweli kaonyesha umbumbumbu wa hali ya juu. Alikua anaongelea akibishana bila ustaarabu. Alikua hajibu hoja bali alitaka wakubaliane na anachokielewa wewe.. Kiukweli nimeshindwa kufaid kipindi cha leo Kwa sababu ya upuuzi alokua anaongea huyu jamaa. Kuna mda aridiriki kusema yanga ni zaid ya CAF. There is something wrong with this guy
 
Katika hali inayoonyesha kuwa sasa kuna uwezekano mkubwa wa kutokea mtafaruku mkubwa kama siyo uadui mkubwa baina ya Shirikisho la Soka Tanzania ( TFF ) na Klabu ya Yanga.

Muda si mrefu katika Kipindi cha michezo cha Clouds fm cha leo Jumapili mchana huu huu Mtangazaji alianza kumuhoji Katibu Mkuu wa TFF Mwesiga kuwa nini kilitokea hadi Yanga ikashindwa kusikilizwa na CAF huku TFF ikiwepo? Majibu ya Katibu Mkuu wa TFF yalikuwa kama yafuatavyo nayanukuu " Ndugu Mwandishi wa Habari sijui mnataka sisi TFF tufanye nini ili hivi Vilabu viridhike. Tuliwataarifu Yanga mapema sana juu ya taratibu za CAF na hadi tukaenda mbele kuwataka Viongozi wa Yanga na hasa kupitia Msemaji wao waende kuhudhuria Kozi za Uongozi na Mawasiliano ambazo huandaliwa na kuratibiwa na CAF lakiki Yanga hawakuenda. Ni suala la aibu sana Mtu ambae hata hajafanya utafiti wa kutosha na hana ufahamu wa kutosha kukurupuka kwenda kubwabwaja katika vyombo vya habari kuonyesha umbumbumbu wake " mwisho wa kumnukuu Katibu Mkuu wa TFF Mwesiga.

Baada ya Mtangazaji huyo kumalizana kumuhoji Katibu Mkuu wa TFF alimgeukia Msemaji wa Yanga Jerry Muro ambae leo alikuwa studioni juu ya hili na majibu ya Jerry Muro yalikuwa hivi namnukuu " Ndugu Mtangazaji kwanza nianze kwa masikitiko makubwa kwa kusema kuwa ni jambo la aibu na la kukera sana kumsikia Mtu mzima kama Katibu Mkuu wa TFF Mwesiga akionyesha jinsi gani yeye sasa alivyo mbumbumbu. Kwanza nimwambie tu kuwa Mimi nina Masters Degree tena ya kutoka USA, Sweden na South Africa na sijasoma na kupata Vyeti vyangu katika hivi Vyuo vyenu vya Manzese. Na si tu kwamba nimesoma sana lakini pia kama Mwesiga anaweza alete hapa Vyeti vyake na Mimi nitoe vyangu kisha tuviweke na muweze kuona Mimi Jerry Muro na yeye Katibu Mkuu wa TFF Mwesiga nani ana akili kumzidi mwenzie na tena anikome kwani naweza kuzidi kumuumbua zaidi ya haya kwani siogopi chochote kwakuwa Yanga ni Timu ya Wananchi na ni wa Kimataifa " mwisho wa kumnukuu Jerry Muro.

Kuna wale ambao huwa mnadhani nakurupuka hivyo basi kwa yoyote aliyesikiliza Kipindi cha Michezo cha Clouds fm cha kila Jumapili ambacho kimemalizika muda si mrefu atakuwa ni shahidi yangu kwa haya niliyoyaorodhesha hapa ila kwa atakayetaka kujiridhisha zaidi anaweza kwenda Clouds fm wakampe audio insert ya Kipindi hicho na haya maneno yao ya shombo yalianza kusikika Saa saba ( 7 ) na dakika 37 na kumalizika Saa saba ( 7 ) na dakika 43 na ukiona bado mgumu kuamini nenda TCRA ambao huwa wanarekodi hivi Vipindi wakupe " mzigo " kamili.

Kituko kikubwa cha aibu ambacho Msemaji wa Yanga amekifanya leo na ambacho hata Watangazaji wa zamu waliokuwepo studioni walikishangaa ni pale ambapo Jerry Muro aliposema kuwa Klabu ya Yanga ni kubwa kuliko Shirikisho la Soka barani Afrika ( CAF ) na kwamba wao Yanga kama Yanga hawatishwi kwa lolote na CAF hivyo basi maamuzi ya Yanga lazima yaheshimiwe na CAF.

Vituko vingine alivyovifanya ni vya kawaida kama vile:

  • Alikuwa anang'ang'ania kuongea bila hata mpangilio hadi kuboa kipindi chote.
  • Alikuwa anapata ugumu sana kuyatamka maneno ya Kiingereza japo yeye ni wa Kimataifa.
  • Amelowesha sana Mic za Studio za Clouds fm hadi sasa wanahangaika kuzikausha japo hawajafanikiwa kwani alikuwa " anapovuka " sana.
  • Kila akiongea alikuwa akiwasukuma na kuwapigapiga wenzie hadi kuwa " kero " kwao.
Ni hayo tu na naomba kuwasilisha.

Kwenye red hizo za mwisho mwisho umeweka 'unazi' au 'ushabiki' wako jambo ambalo siyo zuri. hujawa objective kwa habari hii...hata hivyo pamoja na hayo, naisikitikia sana YANGA...sina comments zaidi...
 
Huyu

Haya yanarudiwa tu hapa mkuu. Tumemsikia msemaji wa yanga kwenye kipindi cha sports round up cha kila jumapili kiukweli kaonyesha umbumbumbu wa hali ya juu. Alikua anaongelea akibishana bila ustaarabu. Alikua hajibu hoja bali alitaka wakubaliane na anachokielewa wewe.. Kiukweli nimeshindwa kufaid kipindi cha leo Kwa sababu ya upuuzi alokua anaongea huyu jamaa. Kuna mda aridiriki kusema yanga ni zaid ya CAF. There is something wrong with this guy


YANGA iko matatizoni, Umaskini ndio unaoitesa YANGA, ni umaskini wa pesa na uelewa...Hofu yangu ya dhati kwa YANGA ni kutokea yale yaliyotokea mwaka 1975/76 ambapo YANGA ilisambaratika na kuzaa Nyota ya Morogoro na baadaye PAN AFRICAN ....
 
Kama akiwa ni yeye au si yeye Wewe utafaidika na nini? Na labda ukishamjua umasikini wako wa akili na mali ndiyo utakwisha au?
pole Sana inaonekana muro anakuumiza Sana kichwa sijui unatamani nafasi yake au la,hakuna siku inakupita bila kumuwaza huyu jamaa.hao clouds fm wamemualika ila kumpa nafasi ya kuongea hamna shaffih kila saa anaingilia yote hujayaona.nashawishika kuamini kuwa Una chuki zaidi na Jerry muro
 
pole Sana inaonekana muro anakuumiza Sana kichwa sijui unatamani nafasi yake au la,hakuna siku inakupita bila kumuwaza huyu jamaa.hao clouds fm wamemualika ila kumpa nafasi ya kuongea hamna shaffih kila saa anaingilia yote hujayaona.nashawishika kuamini kuwa Una chuki zaidi na Jerry muro
Kwa hatua mliyofikia, hata siku akisema yanga tunataka kucheza mechi uchi, mtamshangilia tu! hii ni aina ya ushabiki wa kipumbavu tuliyofikia. Ndiyo maana tusapoti hata upumbavu! Mtaalam wa CAF amefafanua kila kitu, lakini mtu bado anatoa povu! Sijui tatizo ni lugha?!
 
Hata Mimi nimeshangaa na kujiuliza maswali " lukuki " Mkuu. Labda nyie Wasomi wenzake mtusaidie kutufumbua hapo kuwa Je kuna Masters Degree inayotolewa katika nchi tatu? Mimi nafurahi tu anavyotenda kwani namtumia kama reference kwa Wanafunzi wangu WEREVU, WATIIFU na WAAMINIFU wa Mass Com and Journalism kuwa wasije kukosea na wao wakawa HOPELESS kama huyu Mswahili wa Yanga na nashukuru Mwenyezi Mungu kuwa wamenielewa.

Kama na wewe unawanafunzi basi wako katika hasara na unataka wawe watiifu? itakuwa sio UDSM haki ya mungu. Jerry yuko sahihi simamia katika haki na ukweli CAF si ndio hawa wana chaguaga raisi wa FIFA kwa kulazimisha misaada mamelody sundowns ilileta team B kwa Azam sababu walisema ligi ya SA ni bora kuliko kombe la washindi. Akina SHafih daduda wanapenda safari hawawezi kuwa na msaada kwa yanga. Yanga lazima wajisemee ile wanayoona inafaa kwa maslahi yao, mikataba ya CAF ni Zaidi ya ukoloni.
 
Anawaharibia wanayanga kama anataka mipasho aombe kipindi naye warumbane kwa mada yao ya Mani msomi kuliko mwenzake waweke kando kazi zao maana wanatutia kichefuchefu kwani ni viongozi
 
Watanzania tujizoeshe tabia ya kukaa kimya zinapokuja thread za kipumbavu kama hizi,nawapa taarifa tu ndugu zangu.
 
Katika hali inayoonyesha kuwa sasa kuna uwezekano mkubwa wa kutokea mtafaruku mkubwa kama siyo uadui mkubwa baina ya Shirikisho la Soka Tanzania ( TFF ) na Klabu ya Yanga.

Muda si mrefu katika Kipindi cha michezo cha Clouds fm cha leo Jumapili mchana huu huu Mtangazaji alianza kumuhoji Katibu Mkuu wa TFF Mwesiga kuwa nini kilitokea hadi Yanga ikashindwa kusikilizwa na CAF huku TFF ikiwepo? Majibu ya Katibu Mkuu wa TFF yalikuwa kama yafuatavyo nayanukuu " Ndugu Mwandishi wa Habari sijui mnataka sisi TFF tufanye nini ili hivi Vilabu viridhike. Tuliwataarifu Yanga mapema sana juu ya taratibu za CAF na hadi tukaenda mbele kuwataka Viongozi wa Yanga na hasa kupitia Msemaji wao waende kuhudhuria Kozi za Uongozi na Mawasiliano ambazo huandaliwa na kuratibiwa na CAF lakiki Yanga hawakuenda. Ni suala la aibu sana Mtu ambae hata hajafanya utafiti wa kutosha na hana ufahamu wa kutosha kukurupuka kwenda kubwabwaja katika vyombo vya habari kuonyesha umbumbumbu wake " mwisho wa kumnukuu Katibu Mkuu wa TFF Mwesiga.

Baada ya Mtangazaji huyo kumalizana kumuhoji Katibu Mkuu wa TFF alimgeukia Msemaji wa Yanga Jerry Muro ambae leo alikuwa studioni juu ya hili na majibu ya Jerry Muro yalikuwa hivi namnukuu " Ndugu Mtangazaji kwanza nianze kwa masikitiko makubwa kwa kusema kuwa ni jambo la aibu na la kukera sana kumsikia Mtu mzima kama Katibu Mkuu wa TFF Mwesiga akionyesha jinsi gani yeye sasa alivyo mbumbumbu. Kwanza nimwambie tu kuwa Mimi nina Masters Degree tena ya kutoka USA, Sweden na South Africa na sijasoma na kupata Vyeti vyangu katika hivi Vyuo vyenu vya Manzese. Na si tu kwamba nimesoma sana lakini pia kama Mwesiga anaweza alete hapa Vyeti vyake na Mimi nitoe vyangu kisha tuviweke na muweze kuona Mimi Jerry Muro na yeye Katibu Mkuu wa TFF Mwesiga nani ana akili kumzidi mwenzie na tena anikome kwani naweza kuzidi kumuumbua zaidi ya haya kwani siogopi chochote kwakuwa Yanga ni Timu ya Wananchi na ni wa Kimataifa " mwisho wa kumnukuu Jerry Muro.

Kuna wale ambao huwa mnadhani nakurupuka hivyo basi kwa yoyote aliyesikiliza Kipindi cha Michezo cha Clouds fm cha kila Jumapili ambacho kimemalizika muda si mrefu atakuwa ni shahidi yangu kwa haya niliyoyaorodhesha hapa ila kwa atakayetaka kujiridhisha zaidi anaweza kwenda Clouds fm wakampe audio insert ya Kipindi hicho na haya maneno yao ya shombo yalianza kusikika Saa saba ( 7 ) na dakika 37 na kumalizika Saa saba ( 7 ) na dakika 43 na ukiona bado mgumu kuamini nenda TCRA ambao huwa wanarekodi hivi Vipindi wakupe " mzigo " kamili.

Kituko kikubwa cha aibu ambacho Msemaji wa Yanga amekifanya leo na ambacho hata Watangazaji wa zamu waliokuwepo studioni walikishangaa ni pale ambapo Jerry Muro aliposema kuwa Klabu ya Yanga ni kubwa kuliko Shirikisho la Soka barani Afrika ( CAF ) na kwamba wao Yanga kama Yanga hawatishwi kwa lolote na CAF hivyo basi maamuzi ya Yanga lazima yaheshimiwe na CAF.

Vituko vingine alivyovifanya ni vya kawaida kama vile:

  • Alikuwa anang'ang'ania kuongea bila hata mpangilio hadi kuboa kipindi chote.
  • Alikuwa anapata ugumu sana kuyatamka maneno ya Kiingereza japo yeye ni wa Kimataifa.
  • Amelowesha sana Mic za Studio za Clouds fm hadi sasa wanahangaika kuzikausha japo hawajafanikiwa kwani alikuwa " anapovuka " sana.
  • Kila akiongea alikuwa akiwasukuma na kuwapigapiga wenzie hadi kuwa " kero " kwao.
Ni hayo tu na naomba kuwasilisha.
nimecheka sana mkuu
 
Kama na wewe unawanafunzi basi wako katika hasara na unataka wawe watiifu? itakuwa sio UDSM haki ya mungu. Jerry yuko sahihi simamia katika haki na ukweli CAF si ndio hawa wana chaguaga raisi wa FIFA kwa kulazimisha misaada mamelody sundowns ilileta team B kwa Azam sababu walisema ligi ya SA ni bora kuliko kombe la washindi. Akina SHafih daduda wanapenda safari hawawezi kuwa na msaada kwa yanga. Yanga lazima wajisemee ile wanayoona inafaa kwa maslahi yao, mikataba ya CAF ni Zaidi ya ukoloni.

Akhsante kwa kuja.
 
Kwa hatua mliyofikia, hata siku akisema yanga tunataka kucheza mechi uchi, mtamshangilia tu! hii ni aina ya ushabiki wa kipumbavu tuliyofikia. Ndiyo maana tusapoti hata upumbavu! Mtaalam wa CAF amefafanua kila kitu, lakini mtu bado anatoa povu! Sijui tatizo ni lugha?!

Safi sana Mkuu ila usisahau pia kuwa Yanga ndiyo timu pekee hapa duniani inayoongoza kuwa na " vilaza " waliotukuka wengi huku Simba ikiwa katika top 5 ya Klabu yenye intellectuals wengi. Jerry Muro anawakilisha AKILI na UPEO wa Wana Yanga wote duniani kwa 100%.
 
Kitu cha muhimu ni kushinda mechi ya kesho mengine yatapita kama upepo
 
fuatilieni na
Mzee akilimali aliyoyasema,ndo mjue jery muro aliyoyaongea yaana ukweli kiasi gani, bila kupepesha macho Tff ndo tatizo kubwa , yanga wanaposema haki za matangazo tff wameuza ,ni kweli why only Azam TV? wakati ilitakiwa wawe TBC
 
Back
Top Bottom