Mugishagwe
JF-Expert Member
- Apr 28, 2006
- 300
- 58
Ni ilani hii hii ya Mchapakazi kama anavyo itwa na tafiti inataka kutupeleka pabaya wachilia mbali bajeti kuchwangiwa kuna mengi ya kiini macho hapa na yatafumuka siku ndoa na waandishi wa habari ikifa kwa sasa ni sisi tunayaona wananchi wanaona mazuri tuu na haya ngalawa kwenda upande hawaoni maana hakuna wa kuwaripotia . Ilani inatumaliza hii sasa .
Kanisa lamuonya Kikwete
KKKT yaungana na TEC kupinga Ofisi ya Kadhi Mkuu
na Mwandishi Wetu
KANISA la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) limeionya serikali iachane kabisa na mpango wa kuanzisha Mahakama ya Kadhi Mkuu.
Kwa kauli laini lakini zenye msimamo thabiti, kanisa hilo limesema uanzishwaji wa mahakama hiyo ni jambo la hatari, na unaweza kuchochea udini.
Kanisa hilo limetoa onyo pia kwa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuepuka kutunga sheria ya kuanzishwa kwa Ofisi ya Kadhi Mkuu, kwa maelezo kuwa mahakama hiyo itadhoofisha Katiba ya nchi.
KKKT pia imevionya vyama vya siasa vinavyotumia hoja ya Kadhi Mkuu kujinadi kwa masilahi ya kisiasa, kwamba vitahatarisha amani, umoja na mshikamano wa kitaifa uliotukuka tangu nchi hii ipate uhuru.
Msimamo huo wa kanisa hilo kubwa nchini umetolewa mwezi huu katika Baraza la Maaskofu wa KKKT, lililokutana Chuo Kikuu Kishiriki cha Makumira, Arusha.
Tamko hilo lilisainiwa na Mkuu wa Kanisa hilo, Askofu Dk. Samson Mushemba. Linasema wazi kwamba faida za kutenganisha dini na serikali zimeonekana tangu nchi ipate uhuru; na limehoji sababu zinazowafanya watawala waone kuwa faida hizo hazilifai taifa hili sasa.
Tunatambua kwa dhati na fahari kubwa, kuwa serikali yetu haina dini na kwamba huu umekuwa msingi imara wa kuimarisha umoja na mshikamano wa kitaifa. Aidha, tunatambua kuwa serikali yetu na mihimili yake yote muhimu inao wajibu wa kuhakikisha kuna kutenganisha mambo ya dini na mambo ya serikali ili kulinda mshikamano wa kitaifa, inasema sehemu ya tamko hilo.
Kwa hatua hii, KKKT linakuwa kanisa la pili kubwa nchini kutoa tamko dhidi ya jitihada za serikali kuanzisha Mahakama ya Kadhi Mkuu.
Tayari Kanisa Katoliki limeonyesha upinzani mkali dhidi ya mahakama hiyo kwa sababu zile zile zinazotolewa na KKKT, kwamba ofisi hiyo itakuwa chanzo cha vurugu na ubaguzi wa kidini, na mambo ya madhehebu ya dini hayahitaji kutungiwa sheria inayowahusu Watanzania wote.
Zimekuwapo pia hoja nyingi dhidi ya jitihada hizo za serikali, zikisema iwapo sheria itatungwa kuwaruhusu Waislamu kuwa na mahakama yao, itakuwa imeruhusu utitiri wa mahakama za kidini zinazotambuliwa katika madhehebu mbalimbali ya kidini; na kwamba hali hiyo itadhoofisha mahakama zilizopo zinazotambulika kisheria.
Wengine wamedai kwamba hili ni jaribio la kuigeuza Tanzania kuwa nchi ya Kiislamu hatua kwa hatua, jambo ambalo wasingependa Rais Kikwete ahusishwe nalo.
Katika msimamo wao kuhusu Mahakama ya Kadhi, maaskofu wa KKKT wamehoji msukumo wa serikali inayoongozwa na Rais Kikwete, wakasema unaibua shaka na maswali matatu ya msingi:
Tangu tupate uhuru serikali imesisitiza kutokuwa na dini na faida zake tumeziona. Ni kwa faida gani leo, tunalishawishi Bunge letu kutunga sheria ya kuunda Mahakama ya Kadhi?
Vyombo vilivyoundwa kwa mujibu wa sheria, huendeshwa kwa kodi ya Watanzania wa dini zote. Ni kwa nini leo hii tunadiriki kujaribu kujadili kuruhusu kisheria, kundi moja la kidini, kuendesha ofisi yake na mahakama yake, kwa kutumia fedha za walipa kodi wote?
Je, kuwaundia Waislamu mahakama yao hakutaweka mwanya unaoweza kuwafanya kudai nafasi ya pekee katika utawala wa nchi hii? Na je, mahakama hii itatuhakikishiaje kuwa haki za wanawake zitahifadhiwa? inasema sehemu ya hitimisho la tamko la maaskofu hao.
Suala la kuanzishwa kwa Mahakama ya Kadhi Mkuu hapa nchini limekuwa likiibuka na kupotea katika medani za siasa kwa zaidi ya muongo mmoja sasa tangu kurejeshwa kwa mfumo wa vyama vingi vya siasa.
Wapo wanasiasa walioitumia hoja hiyo kama ngazi ya kupandia ili kuvuta hisia za Waislamu.
Aliyekuwa Mbunge wa Bagamoyo, marehemu Kanali Mohamed Ramia na aliyekuwa Mbunge wa Temeke, Augustine Mrema, waliwahi kurusha kete zao kwa kutumia hoja hii.
Serikali, katika awamu tatu zilizopita, imekuwa inaipuuza hoja hiyo tangu miaka ya 60. Lakini zipo habari kwamba Awamu ya Nne, chini ya Rais Jakaya Kikwete, imedhamiria kuanzisha Mahakama ya Kadhi Mkuu, kuwaridhisha Waislamu. Alipokuwa anagombea urais mwaka jana, Kikwete aliifanya hoja ya Kadhi Mkuu kuwa mojawapo ya ajenda zake muhimu.
Bidii hii ya serikali kuanzisha ofisi ya Kadhi Mkuu imewagusa wananchi wengi na kuibua mijadala ya makundi mbalimbali ya wasomi, wanasiasa, viongozi wa dini na wanahabari.
Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), lilikuwa la kwanza kutoa msimamo wa kupinga na kuionya serikali kuhusu hatua ya kuanzishwa kwa Mahakama ya Kadhi Mkuu nchini.
TEC iliitahadharisha serikali kuwa makini na hoja hiyo, ilimtaka Rais Kikwete aiangalie kwa makini na atoe muda kwa jamii kuijadili kwa kina kabla ya kuitekeleza.
Siku chache baada ya TEC kutoa msimamo huo, Naibu Mufti, Sheikh Abubakar Zubeir, alikaririwa na vyombo vya habari akieleza kuwa mtu au kikundi chochote kinachopinga kuanzishwa kwa mahakama hiyo, hawatakii mema Waislamu.
Tamko la Sheikh Zubeir lilifuatiwa na kauli nzito ya viongozi waandamizi watatu wa kanisa walioungana na TEC kupinga kuanzishwa kwa mahakama hiyo huku wakikilaumu Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa kuliweka suala hilo katika ilani yake ya uchaguzi.
Viongozi hao waliinyooshea kidole CCM kuwa ni chama chenye wanachama wa dini mbali mbali, hivyo kitendo cha kuingiza katika ilani yake ya uchaguzi suala linalopendelea kikundi kimoja cha dini ni kuhatarisha umoja wa kitaifa na linaweza kuchochea migogoro ya kidini.
Pia walipinga kuwapo kwa mjadala wowote unaohusu suala hilo bungeni na baadaye kuingizwa kwenye katiba na sheria za nchi.
Walipendekeza masuala yanayohusu dini yaachwe mikononi mwa waumini wa dini kuyajadili na kufikia muafaka.
Walieleza wasiwasi wao kuwa iwapo serikali inayoongozwa na CCM italikumbatia suala hilo, itakuwa inajigeuza kundi la madikteta, kwani historia inaonyesha kuwa serikali nyingi zilizojitumbukiza katika mambo ya kidini zimezaa udikteta wa ajabu.
Agosti 23, Baraza la Ulamaa la Bakwata, nalo liliibuka na kuwashambulia wanaopinga kanzishwa kwa Mahakama ya Kadhi Mkuu nchini.
Katika tamko la Baraza hilo lililosomwa kwa waandishi wa habari na Sheikh Mkuu, Issa bin Shaaban Simba, linasema kitendo cha kumzuia mtu au kikundi kutekeleza ibada au kudai na kupata haki yake ni cha uchochezi ambao unaweza kuvunja amani ya nchi.
Simba alisema baraza hilo linaamini kuwapo kwa Mahakama ya Kadhi Mkuu nchini ni miongoni mwa haki za kimsingi ambazo Waislamu kwa mujibu wa kitabu chao cha Kurani Tukufu, lazima wazipate.
Mufti Simba alisema kwa muda mrefu Waislamu wamekuwa wakiwavumilia wasiokuwa Waislamu kwa kutowaingilia katika mambo yao na taratibu zao za dini.
Aliwataka wasiokuwa Waislamu kujenga heshima kwa wenzao na kutambua kuwa Waislamu pia ni sehemu katika jamii ya Watanzania ambao wana haki pia ya kusema, kusikilizwa na kupewa huduma katika nchi yao.
Lakini hoja ya wanaopinga hoja hii ni kwamba suala hilo libaki kuwa la Waislamu, liwahusishe Waislamu katika taratibu zao za dini, na kama inavyosisitiza KKKT, hoja ya Kadhi Mkuu isitungiwe sheria na Bunge na kulipiwa kodi na Watanzania wote wanaotegemea mfumo wa kisheria uliopo, na unaomhusisha kila mmoja.
KKKT inasema: Ufafanuzi uliotolewa kuhusu kazi na wajibu wa Mahakama ya Kadhi umeonyesha kuwa Mahakama hii itashughulikia kufunga ndoa za Kiislamu na kuzihakiki uhalali wake, masuala ya talaka, mirathi, dini (tawheed), ibada na hadhi ya Waislamu.
Mambo haya ni ya msingi katika ustawi wa familia na jamii kwa ujumla. Hata kwa ufafanuzi huu, tunatambua kuwa jamii ya Watanzania inazo ndoa mseto, familia mseto na mali zinazomilikiwa kwa misingi ya imani mseto. Mseto huu ni msingi wa mshikamano katika jamii. Uanzishwaji wa Mahakama ya Kadhi utabomoa kwa hakika nguzo hii muhimu ya maridhiano pale matatizo yatakapotokea katika familia husika.
Tayari Rais Kikwete anashutumiwa kwa kulibeba suala hili, na kwamba katika miezi michache aliyokaa madarakani, mwenendo wa utendaji wake umeonyesha dalili za kukumbatia udini, huku yeye mwenyewe akiukemea udini katika hotuba zake majukwaani.
Kanisa lamuonya Kikwete
KKKT yaungana na TEC kupinga Ofisi ya Kadhi Mkuu
na Mwandishi Wetu
KANISA la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) limeionya serikali iachane kabisa na mpango wa kuanzisha Mahakama ya Kadhi Mkuu.
Kwa kauli laini lakini zenye msimamo thabiti, kanisa hilo limesema uanzishwaji wa mahakama hiyo ni jambo la hatari, na unaweza kuchochea udini.
Kanisa hilo limetoa onyo pia kwa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuepuka kutunga sheria ya kuanzishwa kwa Ofisi ya Kadhi Mkuu, kwa maelezo kuwa mahakama hiyo itadhoofisha Katiba ya nchi.
KKKT pia imevionya vyama vya siasa vinavyotumia hoja ya Kadhi Mkuu kujinadi kwa masilahi ya kisiasa, kwamba vitahatarisha amani, umoja na mshikamano wa kitaifa uliotukuka tangu nchi hii ipate uhuru.
Msimamo huo wa kanisa hilo kubwa nchini umetolewa mwezi huu katika Baraza la Maaskofu wa KKKT, lililokutana Chuo Kikuu Kishiriki cha Makumira, Arusha.
Tamko hilo lilisainiwa na Mkuu wa Kanisa hilo, Askofu Dk. Samson Mushemba. Linasema wazi kwamba faida za kutenganisha dini na serikali zimeonekana tangu nchi ipate uhuru; na limehoji sababu zinazowafanya watawala waone kuwa faida hizo hazilifai taifa hili sasa.
Tunatambua kwa dhati na fahari kubwa, kuwa serikali yetu haina dini na kwamba huu umekuwa msingi imara wa kuimarisha umoja na mshikamano wa kitaifa. Aidha, tunatambua kuwa serikali yetu na mihimili yake yote muhimu inao wajibu wa kuhakikisha kuna kutenganisha mambo ya dini na mambo ya serikali ili kulinda mshikamano wa kitaifa, inasema sehemu ya tamko hilo.
Kwa hatua hii, KKKT linakuwa kanisa la pili kubwa nchini kutoa tamko dhidi ya jitihada za serikali kuanzisha Mahakama ya Kadhi Mkuu.
Tayari Kanisa Katoliki limeonyesha upinzani mkali dhidi ya mahakama hiyo kwa sababu zile zile zinazotolewa na KKKT, kwamba ofisi hiyo itakuwa chanzo cha vurugu na ubaguzi wa kidini, na mambo ya madhehebu ya dini hayahitaji kutungiwa sheria inayowahusu Watanzania wote.
Zimekuwapo pia hoja nyingi dhidi ya jitihada hizo za serikali, zikisema iwapo sheria itatungwa kuwaruhusu Waislamu kuwa na mahakama yao, itakuwa imeruhusu utitiri wa mahakama za kidini zinazotambuliwa katika madhehebu mbalimbali ya kidini; na kwamba hali hiyo itadhoofisha mahakama zilizopo zinazotambulika kisheria.
Wengine wamedai kwamba hili ni jaribio la kuigeuza Tanzania kuwa nchi ya Kiislamu hatua kwa hatua, jambo ambalo wasingependa Rais Kikwete ahusishwe nalo.
Katika msimamo wao kuhusu Mahakama ya Kadhi, maaskofu wa KKKT wamehoji msukumo wa serikali inayoongozwa na Rais Kikwete, wakasema unaibua shaka na maswali matatu ya msingi:
Tangu tupate uhuru serikali imesisitiza kutokuwa na dini na faida zake tumeziona. Ni kwa faida gani leo, tunalishawishi Bunge letu kutunga sheria ya kuunda Mahakama ya Kadhi?
Vyombo vilivyoundwa kwa mujibu wa sheria, huendeshwa kwa kodi ya Watanzania wa dini zote. Ni kwa nini leo hii tunadiriki kujaribu kujadili kuruhusu kisheria, kundi moja la kidini, kuendesha ofisi yake na mahakama yake, kwa kutumia fedha za walipa kodi wote?
Je, kuwaundia Waislamu mahakama yao hakutaweka mwanya unaoweza kuwafanya kudai nafasi ya pekee katika utawala wa nchi hii? Na je, mahakama hii itatuhakikishiaje kuwa haki za wanawake zitahifadhiwa? inasema sehemu ya hitimisho la tamko la maaskofu hao.
Suala la kuanzishwa kwa Mahakama ya Kadhi Mkuu hapa nchini limekuwa likiibuka na kupotea katika medani za siasa kwa zaidi ya muongo mmoja sasa tangu kurejeshwa kwa mfumo wa vyama vingi vya siasa.
Wapo wanasiasa walioitumia hoja hiyo kama ngazi ya kupandia ili kuvuta hisia za Waislamu.
Aliyekuwa Mbunge wa Bagamoyo, marehemu Kanali Mohamed Ramia na aliyekuwa Mbunge wa Temeke, Augustine Mrema, waliwahi kurusha kete zao kwa kutumia hoja hii.
Serikali, katika awamu tatu zilizopita, imekuwa inaipuuza hoja hiyo tangu miaka ya 60. Lakini zipo habari kwamba Awamu ya Nne, chini ya Rais Jakaya Kikwete, imedhamiria kuanzisha Mahakama ya Kadhi Mkuu, kuwaridhisha Waislamu. Alipokuwa anagombea urais mwaka jana, Kikwete aliifanya hoja ya Kadhi Mkuu kuwa mojawapo ya ajenda zake muhimu.
Bidii hii ya serikali kuanzisha ofisi ya Kadhi Mkuu imewagusa wananchi wengi na kuibua mijadala ya makundi mbalimbali ya wasomi, wanasiasa, viongozi wa dini na wanahabari.
Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), lilikuwa la kwanza kutoa msimamo wa kupinga na kuionya serikali kuhusu hatua ya kuanzishwa kwa Mahakama ya Kadhi Mkuu nchini.
TEC iliitahadharisha serikali kuwa makini na hoja hiyo, ilimtaka Rais Kikwete aiangalie kwa makini na atoe muda kwa jamii kuijadili kwa kina kabla ya kuitekeleza.
Siku chache baada ya TEC kutoa msimamo huo, Naibu Mufti, Sheikh Abubakar Zubeir, alikaririwa na vyombo vya habari akieleza kuwa mtu au kikundi chochote kinachopinga kuanzishwa kwa mahakama hiyo, hawatakii mema Waislamu.
Tamko la Sheikh Zubeir lilifuatiwa na kauli nzito ya viongozi waandamizi watatu wa kanisa walioungana na TEC kupinga kuanzishwa kwa mahakama hiyo huku wakikilaumu Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa kuliweka suala hilo katika ilani yake ya uchaguzi.
Viongozi hao waliinyooshea kidole CCM kuwa ni chama chenye wanachama wa dini mbali mbali, hivyo kitendo cha kuingiza katika ilani yake ya uchaguzi suala linalopendelea kikundi kimoja cha dini ni kuhatarisha umoja wa kitaifa na linaweza kuchochea migogoro ya kidini.
Pia walipinga kuwapo kwa mjadala wowote unaohusu suala hilo bungeni na baadaye kuingizwa kwenye katiba na sheria za nchi.
Walipendekeza masuala yanayohusu dini yaachwe mikononi mwa waumini wa dini kuyajadili na kufikia muafaka.
Walieleza wasiwasi wao kuwa iwapo serikali inayoongozwa na CCM italikumbatia suala hilo, itakuwa inajigeuza kundi la madikteta, kwani historia inaonyesha kuwa serikali nyingi zilizojitumbukiza katika mambo ya kidini zimezaa udikteta wa ajabu.
Agosti 23, Baraza la Ulamaa la Bakwata, nalo liliibuka na kuwashambulia wanaopinga kanzishwa kwa Mahakama ya Kadhi Mkuu nchini.
Katika tamko la Baraza hilo lililosomwa kwa waandishi wa habari na Sheikh Mkuu, Issa bin Shaaban Simba, linasema kitendo cha kumzuia mtu au kikundi kutekeleza ibada au kudai na kupata haki yake ni cha uchochezi ambao unaweza kuvunja amani ya nchi.
Simba alisema baraza hilo linaamini kuwapo kwa Mahakama ya Kadhi Mkuu nchini ni miongoni mwa haki za kimsingi ambazo Waislamu kwa mujibu wa kitabu chao cha Kurani Tukufu, lazima wazipate.
Mufti Simba alisema kwa muda mrefu Waislamu wamekuwa wakiwavumilia wasiokuwa Waislamu kwa kutowaingilia katika mambo yao na taratibu zao za dini.
Aliwataka wasiokuwa Waislamu kujenga heshima kwa wenzao na kutambua kuwa Waislamu pia ni sehemu katika jamii ya Watanzania ambao wana haki pia ya kusema, kusikilizwa na kupewa huduma katika nchi yao.
Lakini hoja ya wanaopinga hoja hii ni kwamba suala hilo libaki kuwa la Waislamu, liwahusishe Waislamu katika taratibu zao za dini, na kama inavyosisitiza KKKT, hoja ya Kadhi Mkuu isitungiwe sheria na Bunge na kulipiwa kodi na Watanzania wote wanaotegemea mfumo wa kisheria uliopo, na unaomhusisha kila mmoja.
KKKT inasema: Ufafanuzi uliotolewa kuhusu kazi na wajibu wa Mahakama ya Kadhi umeonyesha kuwa Mahakama hii itashughulikia kufunga ndoa za Kiislamu na kuzihakiki uhalali wake, masuala ya talaka, mirathi, dini (tawheed), ibada na hadhi ya Waislamu.
Mambo haya ni ya msingi katika ustawi wa familia na jamii kwa ujumla. Hata kwa ufafanuzi huu, tunatambua kuwa jamii ya Watanzania inazo ndoa mseto, familia mseto na mali zinazomilikiwa kwa misingi ya imani mseto. Mseto huu ni msingi wa mshikamano katika jamii. Uanzishwaji wa Mahakama ya Kadhi utabomoa kwa hakika nguzo hii muhimu ya maridhiano pale matatizo yatakapotokea katika familia husika.
Tayari Rais Kikwete anashutumiwa kwa kulibeba suala hili, na kwamba katika miezi michache aliyokaa madarakani, mwenendo wa utendaji wake umeonyesha dalili za kukumbatia udini, huku yeye mwenyewe akiukemea udini katika hotuba zake majukwaani.