afsa
JF-Expert Member
- Dec 6, 2012
- 1,986
- 1,592
Kwa nini CCM inashindwa kutengeneza mazingira sawa ya ushindani ili tujue hayo unayojinasibu nayo yapo au ni porojo? Kwa nini CCM inaua watu wanaoonekana kujenga hoja thabiti mbadala? Kwa nini CCM iko tayari kwa machafuko kuliko kuwakabidhi nchi wapinzani nchi kwa amani?Ccm ni chama kikongwe kinamuda mrefu katika utawala. Kipo kila kata kitongoji vijijini na mijini. Vyama vya upinzani venyewe viongozi wao wametokana na Ccm. Muundo wa serikali ya nchi umetokana na Ccm. Upinzani wanahitaji rasmali ya watu na uchumi kuifikia Ccm ndio maana Nccr ilivuma sasa almost hakipo wakaja Cuf nao ndio hivyo tena. Sasa Chadema na wao bado wana tatizo kubwa la uchumi na ubunifu. Ndio maana upinzani upo zaidi baadhi miji mikuu hapa nchini ndipo kidogo wana mafanikio. Ccm ina mizizi ndani ya nchi hii viongozi wengi wamepitia Ccm iwe wa kijeshi au kiserikali n.k. tutambue hilo. Ccm kuondoka madarakani sio upinzani ushinde hapana kabisa tena hadi pale Ccm yenyewe ipate migogoro tena mikubwa ndipo viongozi wa ndani ya Ccm tena wawe wengi wajitenge na kuanzisha siasa zenye nguvu za watu kiuchumi n.k. na wajijenge kabla kuanzia kwenye mashina ndipo Ccm inaweza ikashindwa. Illa kwa hali ya sasa Ccm ni chama tawala na kinafaa kuongoza japo kinamapungufu mengi lakini kwa upinzani ulivyo bora ya Ccm. Mwenye kufahamu siasa na historia ya nchi hii atatambua na kuujua ukweli.