Unaona eh, one minute you make sense the next unakurupuka na mihemko. Naona umeanza kuishiwa pumzi, sidhani kama umesoma nilicho andika. Unauliza statistics, hukuona kwamba wapiga kura millioni 7 mlio wategemea hawakujitokeza kupiga kura? Namba zote za matokeo nimekuwekea mpaka za serikali za mitaa nimeweka, sasa unataka statistics gani ambazo wewe mwenyewe huwezi kizitafuta? Find them and prove me wrong
Unanishangaza sana na sidhani hata unasomaga takwimu za aina za nchi hii. Hivi unajuwa kama Zanzibar peke yake ilipata watalii wengi zaidi kuliko Kenya? Achilia mbali Tanzania nzima ambayo tumapata watalii millioni 2 kwa mwaka huku kenya wakipata laki 8 kwa mwaka. FDI ya Tanzania imeipita Kenya mara mbili , $2 bln kwa Tanzania compare to $1bln kwa Kenya. Hakuna nchi yoyote ya EAC iliyoifikia Tanzania kwa FDI. Mwaka huu tunaifukuza $4 bln, wewe unaona tumezubaa ila Kenya wenye madeni mpaka yana watokea puwani ndio unaona wana maana. Kwajinsi unavyo elewa wewe, rasilimali zetu hatuzitumii vizuri. Unafikiri $4bln FDI inatoka wapi? $30bln FDI ya kwenye gesi inatoka wapo? $2bln ya utalii inatoka wapi? hizo sio rasilimali zetu?
Yani nasoma unayoyaandika na baki kucheka tuu, through you naona kilicho ndani ya Chadema. Mmezowea kulishana maneno ya uwongo usio na kifani mwisho wasiku mkishindwa manasema mmeibiwa. Hakuna Exit Poll? What? Hivi unajuwa maana ya exit poll? kwani kulikuwa hakuna wajumbe wa kila chama kwenye kila kituo cha kupiga kura, hawakuusika na zowezi la kuhesabu kura. NEC haikutowa takwimu kwa kila chama? Repoti ya uchaguzi 2015 Chadema haikupata copy? Anyway mlikataa matokeo labda na repoti mlisusa.
Haha, eti kilicho wamaliza ni NEC. Kilicho wamaliza ni harakati, badala ya mikakati, nyinyi mlikimbilia kwenye harakati za kuhamasisha vijana mkasahau kuwa vijana watabaki kuwa vijana. Watakuja kwenye mikutano watazungusha mikono wakitoka hapo hawajasikia hata neno moja. Huku mnamgombea ambaye anakwenda kwenye maeneo ya mijini tuu na kidogo karudi Dar, mara napotea kwenye kampeni wiki nzima. Sasa sijuwi muujiza wa kushinda ingetatoka wapi? Mlitaka kufanya shortcut kupitia vijana hilo bomu limewalipukia mikonini, kitengo cha kuchakachua matokeo kilizimwa. Kwanini usiwachukie TISS.
Ni aibu kuona Chadema inamkashifu Dr. Slaa kama hivi ulivyo msema hapa. Maybe haya ni maneno yako binafsi lakini ni aibu kubwa kwa mtu aliyejitolea vile. Lakini kwanini nishangae ikiwa mtu kama Zitto unaetumia jina lake hapa na yeye mlimwita msaliti. SMH
Kuna mambo unaandika ya maana with a lot of political correctness. Uwe mkweli pia, si unataka kutuaminisha unachosema ni cha kweli na unatoa takwimu? Maana kwa maelezo yako hapo juu, Tanzania iko vizuri sana kiuchumi, si ndiyo? unataka kila mtu aamini hivyo? na aamini kwa kuzingatia takwimu ulizozitoa hapo juu?? Mkuu, umesomea chuo gani uchumi??? si huyo tu jamaa unayejadilia naye hapo juu, unatushangaza watu wengi tunaosoma unachokiandika hapa!