Ungejua unyeti na umuhimu wa hao mabwana wa mstari , hakika usingekuja kubwabwaja maneno mbofu mbofu hapa jamvini namna hiyo.
Kukaa kwako , kulala kwako, kusatehe kwako, kujikuna kwako, kubarizi kwako, kusoma kwako, kuuza kwako genge, kuingia kwako JF muda wowote , kuangalia kwako taarifa ya habari saa 2 usiku, kwenda kwako msibani, harusini, n.k koooteeeee huko kunafanikishwa na kazi iliyotukuka ya hao mabwana either direct or indirect , either in a visible or invisible manner. Siku ukiwakosa wazalendo kama hawa hakika utalia na kusaga meno.
Ila kwasababu Watanzania ni watu wa style ya kinyonga , leo hii tutawaona kama hawafahi ila siku wakiingia hao wengine mnao dhani watakuja kuwaletea maziwa , asali na siagi. ndipo mtajuuuuta kukutwa na bwana pepsi na kubaki kusema " Tungejua......" .
Asiye sikia la mkuu .