Mag3,
Mkuu hakuna maneno mengi ila tuzungumzie facts, Kwani hiyo katiba ya Zanzibar inatukwaza nini haswa? Toka wameandika ni shughuli gani za serikali ya Muungano imeshindwa kuzitekeleza kama zamani?
Mkuu wangu hakuna sababu ya kutukana, hoja yako itafika pasipo matusi maana nikianza hatutafika popote ila kuvuana nguo. Hapa tunajadili mambo ya Muungano na sio katiba ya Zanzibar, ukitaka anzisha ukumbi wake na tukutane huko.Wewe Mkandara ni bogus kabisa
Kwa hiyo akitokea mtu akavunja katiba so long as shughuli za serikali haziathiriwi kwako wewe sawa.
Huu ni Upunguani wa hali ya juu.
Ni sawa na wale wanaotuaminisha kuwa hatuna haja ya katiba mpya,haja yetu ni maji,matibabu na umeme.
Wewe si uliponda madai ya UKAWA na kusema hukuona hoja ya wao kutoka nje.
Mkuu wewe ni mmoja kati ya Vijana wa hovyo kwa kiwango ambacho hakiwezi kuelezeka.
Mkandara, naomba tu unipe jibu halafu tuendelee na huu mnakasha kuhusu mfumo huu unaoupendekeza wa mambo yooote kuwa ya Muungano. Nauliza tena, je mfumo huo unawezekana bila kuathiri Katiba ya sasa ya Zanzibar? Hilo tu.Mag3,
Mkuu hakuna maneno mengi ila tuzungumzie facts, Kwani hiyo katiba ya Zanzibar inatukwaza nini haswa? Toka wameandika ni shughuli gani za serikali ya Muungano imeshindwa kuzitekeleza kama zamani?
Mkuu wangu unaniuliza swali ambalo jibu lake liko wazi kabisa. Chochote kinachokubaliwa katika uandishi wa katiba hii mpya na kikapitishwa na wananchi kitabadilisha katiba zote mbili. Tukikubali ushirika wa SHIRIKISHO utabadilisha katiba ya Muungano na ya Zanzibar. Tukipitisha serikali 3 itakuwa hivyo hivyo, tukisema rais atakuwa mmoja na kadhalika, haya ni maamuzi yetu sote na sio swala la kuathiri katiba fulani ama tuna chuki bali ni katika kuboresha mahusiano yetu.Mkandara, naomba tu unipe jibu halafu tuendelee na huu mnakasha kuhusu mfumo huu unaoupendekeza wa mambo yooote kuwa ya Muungano. Nauliza tena, je mfumo huo unawezekana bila kuathiri Katiba ya sasa ya Zanzibar? Hilo tu.
Mkuu yote hiyo ni kutaka kufunika hoja ya muundo wa S3 na hasa kuzinduka kwa Tanganyika. Ni jitihada za kutaka kuona Tanganyika haitajwi na wala haisikiki. Haiingii akilini kuwa tunaweza kuwa na mambo yote wakati kuna waliyo nayo.Mkandara, naomba tu unipe jibu halafu tuendelee na huu mnakasha kuhusu mfumo huu unaoupendekeza wa mambo yooote kuwa ya Muungano. Nauliza tena, je mfumo huo unawezekana bila kuathiri Katiba ya sasa ya Zanzibar? Hilo tu.
MAONI KUHUSU KATIBA MPYA
Kwanini mambo yote yawe ya Muungano
Kufuatia mgogoro uliopo baina ya pande mbili za kisiasa kushindwa kufikia muafaka juu ya muundo wa serikali ningependa kusema tatizo la nchi yetu lipo ndani zaidi ya swala la idadi ya serikali zetu iwe 1, 2 au 3 kwa sababu serikali huundwa kwa minajiri ya kugawana mamlaka ya utekelezaji wa shughuli za maendeleo. Na ifahamike tu kwamba hakuna muundo maalum wa serikali ziwe ngapi ktk mfumo wa washirika ktk utawala wowote iwe ule wa Muungano (union), Shirikisho (federation), Jumuiya (Confederation/Community) kwa sababu ushirika haujengwi kwa idadi ya serikali bali hali halisi ya matakwa ya wananchi ktk ushirika wao kwa masharti na malengo walotaka kuyafikia ndio hujengwa serikali zake ili kuwafikia wananchi haraka na wepesi zaidi.
Mgogoro wa kisiasa
Sintojikita ktk mgogoro wa kisiasa ulofuatia bunge maalum la katiba kuvunjika kwa sababu huo ni mjadala mrefu sana pengine tutaugusia pale inapopaswa isipokuwa nitakwenda moja kwa moja katika kutoa maoni yangu kuhusiana na mapungufu ya kiutawala ndani ya katiba iliyopo ambayo wananchi walikusudia kufanywa na sio mgogoro juu ya Muungano wetu ama serikali ngapi zinafaa kwa sababu kati ya wananchi walochangia sana mjadala huu wa katiba na kuufuatilia kwa ukaribu sana toka mwaka 2002 hapa JF mimi nilikuwa mmoja wapo.
Kwa mtazamo wangu, baada ya kutazama kwa kina malalamiko ya pande zote mbili ambazo zingependa sana kuishi pamoja kwa amini na utulivu lakini wameshindwa kufikia muafaka wowote juu ya Mustakabali wa taifa hili ndani ya UTAIFA huu imetokana na wote kushindwa kuingia ndani zaidi kutazama kiini cha matakwa ya wananchi bali wametumia siasa zaidi kupanua wigo la hoja za Muungano wenyewe jambo ambalo wangeweza kuwakilisha hoja hiyo katika vikao vya bunge na kadhalika pasipo kuathiri uandishi wa katiba tuitakayo. Hivyo nimekuja na mapendekezo ambayo nina hakika yatagusa hisia za wananchi wa sehemu zote za JMT ikiwa ni kuanza na muundo wa UTAWALA na mamlaka yake.
Ni imani yangu kwamba kutokana na hoja za pande mbili zote ambazo zimejikita zaidi ktk Muungano na serikali ukiwasoma kwa undani utagundua kwamba wanahitilafiana zaidi ktk kugawana MAMLAKA ya utekelezaji wa shughuli za serikali hivyo matatizo hayapo ktk aidha kwenye Muungano wenyewe ama idadi ya serikali. Lakini hata utawala huu umejaribu sana kuongeza hesabu za mikoa, wilaya na hata majimbo lakini kwa vile mabadiliko hayo hayatoi mamlaka kamili kwa vyombo vya serikali hizo ili kutekeleza majukumu yao na kuwajibishwa na wananchi, mabadiliko hayo hayakuleta mafanikio zaidi ama kupunguza kero za wananchi.
Hivyo katiba yetu bado inapwaya sana ktk kutoa mamlaka kwa wananchi na serikali, serikali na halmashauri zake kwa sababu bado mfumo mzima wa utawala wa nchi hii upo bado ktk mageuzi (transition) ya Kisiasa na kiuchumi na ilitakiwa hatua kwa hatua kuweza kufikia mageuzi kamili ikiwa KATIBA ya nchi yetu hii itabadilishwa na kutoa mamlaka hayo kwa vyombo vinavyostahili kuleta mabadiliko yanayokusudiwa. Sheria mama ndiyo dira na mwongozo wa mabadiliko yote na sii kutegemea muundo wa washirika ama idadi ya serikali ndizo hupelekea kupata maendeleo.
Hivyo kwa kuwa naamini kwamba mgogoro mkubwa wananchi wa pande zote mbili unahusiana na maslahi ya nchi hizo inaonyesha wazi kwamba katiba iliyopo ina mapungufu ambayo hayakomei ktk washirika wa muungano wa nchi hizi mbili bali mgogoro huo unashuka hadi ktk tawala za mikoa, wilaya na miji yake kwa madai ya kutopewa huduma bora kulingana na mahitaji yao. Mapungufu haya ya muda mrefu yamezua kero nyingi sana toka Halmashauri za mitaa, miji, wilaya, mikoa, serikali 2 hadi imefikia watu kutokuwa na imani na viongozi ama serikali zao kwa sababu ya muundo mzima wa Utawala wa nchi yetu ulijengwa ktk misingi ya Kijamaa.
Chama tawala kilikuwa na mamlaka yote ya kiutawala toka uchaguzi wa wajumbe wa nyumba kumi, viongozi wa halmashauri, wabunge, mawaziri, baraza kuu la Mawaziri (executive council), mahakimu, uteuzi wa viongozi wote wa taasisi serikali, mashirika ya umma, vyoombo vya serikali, vyama vya ushirika, uteuzi wa watendaji wakuu wa ngazi zote za serikali, nafasi za kazi kwa waajiriwa na kadhalika. Chama tawala pia kilikuwa ndicho chombo pekee kilichomiliki njia kuu za uchumi ambazo ni pamoja na Ardhi, maji, madini, misitu, mafuta, nguvu za umeme, usafiri, njia za habari, bishara za nje, mabenki, bima, viwanda vya chuma, silaha, simenti, mbolea, viwanda, ugawaji na mambo mengi makubwa ambayo kwa wakati ule ndio ilikuwa msingi mkubwa wa ujenzi wa UTAIFA wetu.
Haya yote ni mambo yalokuwa ktk siasa ya Ujamaa na Kujitegemea chini nya chama kimoja na haya hayawezi kuondoka kwa kubadilisha ushirika wetu iwe kwa kuvunja muungano ama kujadili idadi ya serikali zetu, ititiri wa vyama vya siasa na mahitaji yao bali yanahitaji mabadiliko makubwa ya katiba yetu ili Mamlaka hayo yote yapelekwe katika sehemu zinazohusika ili kurahisisha utekelezaji wa shughuli zote za serikali, taasisi na na vyombo vya kijamii ambavyo ndivyo pekee leo hii vinavyotakiwa kuwajibika ktk kushiriki katika kutoa huduma, haki na usawa wa jamii hii. Hatuwezi kuendelea na mfumo ule ule tukitegema kubadilika kwa serikali ndio muarobaini wa mapungufu makubwa ya kikatiba uwajibikaji na mamlaka ya vyombo vya utekelezaji.
Ni Imani yangu kwamba Watanzania wengi wameitaka katiba mpya ambayo italenga kuondoa mapungufu ya katiba yetu ya mwaka 1977. Wananchi wanaitaka katiba ambayo inayojitosheleza ktk maswala yote UTAWALA, KISIASA, KIJAMII na KIUCHUMI kulingana na mazingira ya dunia tuishiyo, hivyo basi
Napendekeza MUUNGANO na sio SHIRIKISHO uendelee kuwepo isipokuwa ktk sehemu ya kwanza ibara ya 4 (3) ya katiba ya JMT ya mwaka 1977 pamoja na rasimu ya katiba ya tume ya Warioba ziyaweke MAMBO YOTE YAWE YA MUUNGANO isipokuwa Ushuru wa bidhaa na mapato yasokuwa ya kodi kama liseni na sheria. Kwa kufanya hivo Serikali zetu, Manispaa, Mashirika ya Umma, na vyombo vya serikali kama TISS, NEC, na kadhalika yote yapewe mamlaka kamili ya kupanga Utekelezaji wa shughuli zao kama itakavyo ainishwa pasipo kuvunja masharti ya katiba na hivyo kuwajibika moja kwa moja na sheria mama ilotungwa kwa manufaa ya wananchi ili kukuza amani na utulivu.
Mambo yote yakiwa ya Muungano yataweza vipi kuondoa mapungufu na kufuta kero za wananchi? Hili nitalizungumzia baada ya kujibu hoja za wanabodi ambao watakuwa na haja ya kulizungumzia hili.
Nawasilisha
Invisible, Mzee Mwanakijiji, Kibunango, Pasco, Mdondoaji, lynxeffect22, JokaKuu Mag3 Mchambuzi Nguruvi3 Barubaru, Waberoya, AshaDii, Zakumi, Mama Mdogo, Ngongo, Nyamizi, Mimibaba, Katavi, bona, Janjaweed, zumbemkuu, TUJITEGEMEE, Mwelewa, MTAZAMO, amkawewe, gfsonwin, Englishlady, Sikonge, Mgaya D.W
Mkuu wangu hatushindani ila tunabadilishana mawazo. Hakuna kati yetu anayetaka madaraka kwa sababu hatupo ktk uongozi ngazi yoyote pengine wewe mwenzetu. Ila ningependa sana unieleze Utafiti upi waliufanya maana nijuavyo walikusanya maoni ya wananchi na wao wakatunga rasimu kutokana na maoni hayo au ilikuwa tofauti?ulafi wa madaraka utakuja watokea watu puani na kusababisha machafuko .... vile vichwa vya hekima vilivyoleta rasimu vilifanya utafiti sana kulingana na hali yetu ya sasa .... bado naona umehimu wa kufuata muundo uliopendekezwa na rasimu ya tume na kujikita katika kuimarisha madaraka ya serikali ya jamhuri wa muungano (hivi ndivyo serikali ya marekani na states zinazounda marekani zinazidi kushamiri kulinganisha na nchi nyingine duniani)
Mkandara, hii ya kwako ni usanii at its best! Wazanzibari walikaa pamoja wakajadiliana kuhusu hatma yao na wakaamua kwa pamoja kujenga msingi imara utakaostahimili changamoto na mikiki mikiki iliyokuwa ikisababishwa na kero za Muungano wa serikali mbili katika nchi moja. Msingi huo imara, Katiba, ulipitishwa na Wazanzibari wote bila kujali itikadi, dini, rangi, jinsia wala kabila iliunda nchi ya Zanzibar ndani ya Muungano yenye mipaka na mamlaka ya juu yasiyoweza kuhojiwa na mamlaka yoyote nyingine ndani na nje ya Muungano. Katiba hiyo pia ilisisitiza kuwa haiwezi kufanyiwa marekebisho isipokuwa na Wazanzibari wenyewe kupitia vyombo vyao walivyojiwekea kulingana na maelekezo ya Katiba hiyo.
Mkandara, unaweza kutudokeza japo kidogo ni njia ipi itatumika kuhakikisha mambo yote yanakuwa ya Muungano bila kuathiri Katiba ya Zanzibar kama ilivyo sasa? Kumbuka kuwa pamoja na kuwa na Katiba ya Muungano bado Zanzibar peke yao waliweza kukaa, wakajadili na kupitisha Katiba inayopingana na ya Muungano na hakuna aliyewajibishwa. Kumbukumbu ziko kwamba hii ni hoja mojawapo iliyowapa wakati mgumu sana Tume ya Mabadiliko ya Katiba; sasa kama si mawazo ya kilaghai na kujaribu kuondoa watu kwenye hoja ya maana na ya msingi, naomba uwe mkweli utuambie mbinu gani ya kisheria itatumika kuwapokonya Wazanzibari haki yao ya Kikatiba ya kujiamulia mambo yao wenyewe...jeshi?
Mkuu wangu nadhani nyote humu mumewahi kuishi nje, nawaomba sana nambieni moja tu. Ni nchi gani ya kidemokrasia ndani ya Muungano ambayo haina mamlaka walojichukulia Zanzibar.Mkuu Mag3 hili nanlo neno,unajua kuna makada wa CCM walikuwa wakimimina dhihaka tume ya Jaji Warioba wasijie tume ile ilifikia udhaifu mkubwa wa serekali ya Kikwete ambayo ilishindwa kuidhibiti Zanzibar ilipokuwa ikivunja katiba wazi wazi tena pasipo kificho.Ni ukweli usio na shaka kwamba baadhi ya mapendekezo ya tume ya Jaji Warioba yaliangalia ugumu wa kuipokonya Zanzibar mamlaka waliojinyakulia.
Kuna wakati najiuliza maswali mengi nakosa majibu hasa wale wanaolazimisha serekali mbili ikiwa wanajua wanachokipigania kinapingana na hali halisi.
Kwanini mambo yote yawe ya Muungano
Kufuatia mgogoro uliopo baina ya pande mbili za kisiasa kushindwa kufikia muafaka juu ya muundo wa serikali ningependa kusema tatizo la nchi yetu lipo ndani zaidi ya swala la idadi ya serikali zetu iwe 1, 2 au 3 kwa sababu serikali huundwa kwa minajiri ya kugawana mamlaka ya utekelezaji wa shughuli za maendeleo. Na ifahamike tu kwamba hakuna muundo maalum wa serikali ziwe ngapi ktk mfumo wa washirika ktk utawala wowote iwe ule wa Muungano (union), Shirikisho (federation), Jumuiya (Confederation/Community) kwa sababu ushirika haujengwi kwa idadi ya serikali bali hali halisi ya matakwa ya wananchi ktk ushirika wao kwa masharti na malengo walotaka kuyafikia ndio hujengwa serikali zake ili kuwafikia wananchi haraka na wepesi zaidi.
Mag3,
Mkuu hakuna maneno mengi ila tuzungumzie facts, Kwani hiyo katiba ya Zanzibar inatukwaza nini haswa? Toka wameandika ni shughuli gani za serikali ya Muungano imeshindwa kuzitekeleza kama zamani?
Mkuu wangu hatushindani ila tunabadilishana mawazo. Hakuna kati yetu anayetaka madaraka kwa sababu hatupo ktk uongozi ngazi yoyote pengine wewe mwenzetu. Ila ningependa sana unieleze Utafiti upi waliufanya maana nijuavyo walikusanya maoni ya wananchi na wao wakatunga rasimu kutokana na maoni hayo au ilikuwa tofauti?
Hiyo Marekani uloitolea mfano ina mahusiano gani na mada hii pengine nifahamishe wapi nafanya makosa maana sikuelewi. Pili, unaweza kunambia hili swala la kuvunja Muungano (Union) na kuunda Shirikisho (federation) wamelipata wapi?
Shuukran sana kwa maswali haya maana naona watu wote hapa wanaishambulia Zanzibar kama vile wao ndio wakosa. lakini ukweli ni upi? Nakuombeni sikilizeni hotuba ya makamu wa rais wa Zanzibar mwaka 2011 wakati wa maandimisho ya miaka 50 ya Uhuru wa Tangayika ambayo wengi tunajiuliza iko wapi, lakini hawa hawa wanataka Muungano. Jamani mwee, tumetumia katiba ya Tanganyika kwa miaka 50 ya muungano na hata wimbo wetu wa Taifa ni wa Tanganyika lakini tunachokiona ni Wazanzibar ndio tu wakosa kutaka mabadiliko kwa upande wao, bado tunataka kuipa Tanganyika mkono wa juu ilihali sasa hivi tupo ktk mfumo wa demokrasia ambao lazima kwanza tuepuke mgawanyiko.Mkandara asante sana kwa bandiko zuri lililojaa uchambuzi yakinifu.............
mie nina swali moja tu kwako, ivi kama Zanzibar mambo haya 22 yaliyoko kwenye Muungano kwa sasa, hawayataki na mpaka apo wameyaongeza kuwa 47 yanaleta utata je tukifanya yote yawe ya muungano unafkiri kitakubalika??
ivi je kuna shida gani basi kukawa kuna S3 labda na rais mmoja ila mawaziri wakuu wa 3 nikiwa na maana kwamba kila serikali iwe na waziri mkuu wake??
na je hatuon ili kukata mzizi wa fitina basi ni afadhal kuirudisha Tanganyika yetu, na Zanzibar ikawepo kisha tukawa na serikal ya Muungano?? at least ikawepo fareness kwenye distribution ya resources?
Kwangu mimi naamini serikali moja ndiyo jibu la matatizo yote ikiwa tu wananchi wataridhia. Ila was iwasi na pia jinsi maoni ya waZnZ wengi alivyo hawatakubali kuwa na nchi moja maana yake Zanzibar inakuwa mkoa au jimbo. Mwisho issue ya aina ya Muungano ndio inaamua mifumo yote ya utawala na matumizi ya rasilimali kwa hiyo ni vizuri referundum kwanza bila kuleta uchakachuzi.