MchunguZI
JF-Expert Member
- Jun 14, 2008
- 4,009
- 2,173
Katiba yetu inasema mtu anayetaka kugombea u-Rais ni lazima awe ametimiza umri wa miaka 40. Umri wa juu wa kugombea kuwa Rais haukutajwa!!
Baada ya kuangalia yanayotokea Senegal nimekuwa na tamaa ya katiba yetu kuweka kikomo cha umri wa juu kwa mtu kugombea u-Rais. Naona si rahisi kuwa na mzee wa kiafrika anayeweza kutuendeleza. Wengi wanatafuta kufa vizuri badala ya kuishi vizuri.
Napendekeza miaka 65 uwe ni umri wa juu kwa m-TZ kugombea kuwa Rais. Hii itampa fursa ya kutimiza vipindi viwili kabla ya kustaafu (miaka 75) angalau akiwa na ubongo salama kwa maisha yetu. Hiyo 65 tayari ni nje ya wastani wa maisha ya m-Tz. Akistaafu akiwa 75 pia itatupunguzia wastaafu wanaotaka kulishwa bure bila faida kwa nchi.
Naomba jopo la katiba litakapowatembelea popote Tz, tuwe pamoja kusisitiza hili.
Naomba samahani kwa wale ambao munamuunga mkono yule jamaa yetu aliyejaa ‘kihelehele' cha kutafuta u-Rais wa 2015.
Baada ya kuangalia yanayotokea Senegal nimekuwa na tamaa ya katiba yetu kuweka kikomo cha umri wa juu kwa mtu kugombea u-Rais. Naona si rahisi kuwa na mzee wa kiafrika anayeweza kutuendeleza. Wengi wanatafuta kufa vizuri badala ya kuishi vizuri.
Napendekeza miaka 65 uwe ni umri wa juu kwa m-TZ kugombea kuwa Rais. Hii itampa fursa ya kutimiza vipindi viwili kabla ya kustaafu (miaka 75) angalau akiwa na ubongo salama kwa maisha yetu. Hiyo 65 tayari ni nje ya wastani wa maisha ya m-Tz. Akistaafu akiwa 75 pia itatupunguzia wastaafu wanaotaka kulishwa bure bila faida kwa nchi.
Naomba jopo la katiba litakapowatembelea popote Tz, tuwe pamoja kusisitiza hili.
Naomba samahani kwa wale ambao munamuunga mkono yule jamaa yetu aliyejaa ‘kihelehele' cha kutafuta u-Rais wa 2015.