JamboJema
JF-Expert Member
- Jun 14, 2011
- 1,143
- 209
Uraia wa Tanzania utamkwe pasina kuweka mashaka. Sina tatizo na aina zote za 'uraia' tulizonazo...ila ningependa ule wa kuandikishwa kigezo kimoja kiwe mwombaji awe na moja ya sifa kuwa ameoa/ameolewa na Mtanzania wa kuzaliwa. Kama hawezi hili na hata kama anamanufaa vipi na nchi yetu, basi apewe Hadhi ya Ukaazi ya Kudumu ila sio uraia. Mgeni mwenye Hati ya Ukaaji atenganishwe kabisa namna ya kupata huduma mbalimbali...ie. mashuleni, mahospitalini na hata kwenye kupata bidhaa mbalimbali. Hili litasaidia kupunguza na kuzuia uzalishaji wa wahamiaji haramu.