Katiba isiyompa rais mamlaka haitufai.

Mwakaboko King

JF-Expert Member
Apr 22, 2015
1,099
207
image.jpg
Kuna baadhi ya watu fulani wamekuwa na hasira kuhusu mamlaka ya Rais yaliyoanishwa kwenye Katiba Inayopendekezwa ile Sura ya nane,Kuanzia Ibara ya 80 mpaka 98. Watu hao wamefikia hatua ya kutaka apunguziwe mamlaka huku wengine hasira zao zikipitiliza wakitaka hata yale aliyonayo yaondolewe yote kabisa abaki kama mtumishi wa kawaida!

Jambo la kunishangaza ni pale watu hao wanaposhindwa kuelewa kuwa mamlaka au heshima ya mfalme ni wingi wa watu wake!wanashindwa kuelewa kuwa Mamlaka ya Rais ni wingi wa kura zake,hawezi kulinganishwa na mtu yeyote katika nchi na Katiba Inayopendekezwa ambayo wananchi wataipigia kura imelizingatia hili.

Kwa mujibu wa Katiba ya 1977 Tanzania tunao utaratibu wa kumpata Rais kupitia sanduku la kura (nguvu ya umma) ambazo humpa Mamlaka ya kuongoza na kutawala.Rais ni Mkuu wa Nchi,kiongozi wa Serikali na Amiri Jeshi Mkuu.

Kwa Tanzania Rais ni alama na taswira ya Jamhuri ya Muungano na watu wake na pia ni alama ya umoja ,uhuru wa nchi na mamlaka yake!

Sasa inawezekanaje Kiongozi Mkuu wa nchi na Amiri Jeshi Mkuu wa vyombo vya ulinzi na Usalama vya nchi ukataka alinganishwe na mjumbe au mbunge au waziri? Hilo haliwezekani fuatilia nchi zote ambazo wamekubali upuuzi huu utaona marais wao ni kama mapambo tu na wana jina lao eti wanabaki kuwa Ceremonial hawana mamlaka ya maamuZi ya nchi wapo wapo tu, hili halikubaliki Tanzania Rais ni MAMLAKA hata UKAWA wanalijua hili ndo maana wanajaribu jaribu kuungana wakiamini kuwa watashinda nafasi ya Urais nao wawe na kiongozi mwenye mamlaka katika nchi.

Mungu Ibariki Tanzania!

Nawasilisha!
 
Kuna baadhi ya watu fulani wamekuwa na hasira kuhusu mamlaka ya Rais yaliyoanishwa kwenye Katiba Inayopendekezwa ile Sura ya nane,Kuanzia Ibara ya 80 mpaka 98. Watu hao wamefikia hatua ya kutaka apunguziwe mamlaka huku wengine hasira zao zikipitiliza wakitaka hata yale aliyonayo yaondolewe yote kabisa abaki kama mtumishi wa kawaida!

Jambo la kunishangaza ni pale watu hao wanaposhindwa kuelewa kuwa mamlaka au heshima ya mfalme ni wingi wa watu wake!wanashindwa kuelewa kuwa Mamlaka ya Rais ni wingi wa kura zake,hawezi kulinganishwa na mtu yeyote katika nchi.

Tanzania tunao utaratibu wa kumpata Rais kupitia sanduku la kura (nguvu ya umma) ambazo humpa Mamlaka ya kuongoza na kutawala.Rais ni Mkuu wa Nchi,kiongozi wa Serikali na Amiri Jeshi Mkuu.

Kwa Tanzania Rais ni alama na taswira ya Jamhuri ya Muungano na watu wake na pia ni alama ya umoja ,uhuru wa nchi na mamlaka yake!

Sasa inawezekanaje Kiongozi Mkuu wa nchi na Amiri Jeshi Mkuu wa vyombo vya ulinzi na Usalama vya nchi ukataka alinganishwe na mjumbe au mbunge au waziri? Hilo haliwezekani fuatilia nchi zote ambazo wamekubali upuuzi huu utaona marais wao ni kama mapambo tu na wana jina lao eti wanabaki kuwa Ceremonial hawana mamlaka ya maamuZi ya nchi wapo wapo tu, hili halikubaliki Tanzania Rais ni MAMLAKA hata UKAWA wanalijua hili ndo maana wanaungana wakiamini kuwa watashinda nafasi ya Rais mwenye ambaye atakuwa na mamlaka!

Mungu Ibariki Tanzania!

Nawasilisha!

Ni kweli, mamlaka ndiyo majukumu yenyewe. Mungu Ibariki Tanzania na Watu wake.
 
Jifunzeni acheni mambo ya kurukia! Huyo Rais wenu wa Serikali 3 ataondolewa with one year
 
Raisi si mfalme.

ipo tofauti kubwa kati ya raisi katika mfumo wa demokrasia na mfalme na ukijua hiyo tofauti utasema kweli raisi apunguziwe madaraka.

wafalme ni viongozi katika mifumo ya zamani ambayo watu hawa walichaguliwa na miungu na sio wanadamu. kwa maneno mengine viombe wanaowadanganya wanadamu mpaka wakawaua maalbino ndio hao hao waliwachagua wafalme.

enzi hizo liaminika wafalme wanawakilisha miungu hivyo wao walikuwa wakuu juu ya wananchi na wao hawa wafalme walibeba uungu kwa anachosema mfalme ni final. akiamua kukunyanganya mke, shamba au mali au kitu chochote hakuna wa kuhoji bali amri ya mfalme ilitekelezwa bila kupinga.

lakini wanadamu walikuja kubaini kuwa utawala wa wafalme ulikuwa un justice na waliwakilisha vitu ambavyo vilijigamba kuwasaidia wanadamu lakini vilikuwa vinawatesa tu bila msaada wowote na hivi ndio miungu.

lakini raisi anabeba dhana ya mkurugenzi wa kampuni ya umma.

watanzania hawa kwa umoja wao wanamiliki mali na wakaamua kuunda chombo cha kusimamia mali zao nacho ni serikali.

hii ni sawa na watu hamsini au zaidi kuamua kuunganisha mali zenu sasa mnaamua kuunda chombo cha kusimamia mali hizo na kumteua mkurugenzi mkuu.

hivi ndivyo dhana ya raisi ilivyo kwa maana wananchi ni wakurugenzi katika serikali kwa maana wao ndio wamiriki na wanamteua raisi kwa kura ili akaunde serikali.

hivyo raisi anawajibika kwa wananchi na hatakiwa kuwa na mamlaka ya kifalme ya kufanya chochote anachotaka.

mantiki ya kumpunguzia raisi madaraka inakuja hapohapo kwa kutambua kuwa madaraka makubwa yaliyowekwa kwa raisi yanamrudisha katika mfumo wa miungu na sio mfumo wa kuwa mtendaji anayewajibika kwa wananchi.

Kuna baadhi ya watu fulani wamekuwa na hasira kuhusu mamlaka ya Rais yaliyoanishwa kwenye Katiba Inayopendekezwa ile Sura ya nane,Kuanzia Ibara ya 80 mpaka 98. Watu hao wamefikia hatua ya kutaka apunguziwe mamlaka huku wengine hasira zao zikipitiliza wakitaka hata yale aliyonayo yaondolewe yote kabisa abaki kama mtumishi wa kawaida!

Jambo la kunishangaza ni pale watu hao wanaposhindwa kuelewa kuwa mamlaka au heshima ya mfalme ni wingi wa watu wake!wanashindwa kuelewa kuwa Mamlaka ya Rais ni wingi wa kura zake,hawezi kulinganishwa na mtu yeyote katika nchi.

Tanzania tunao utaratibu wa kumpata Rais kupitia sanduku la kura (nguvu ya umma) ambazo humpa Mamlaka ya kuongoza na kutawala.Rais ni Mkuu wa Nchi,kiongozi wa Serikali na Amiri Jeshi Mkuu.

Kwa Tanzania Rais ni alama na taswira ya Jamhuri ya Muungano na watu wake na pia ni alama ya umoja ,uhuru wa nchi na mamlaka yake!

Sasa inawezekanaje Kiongozi Mkuu wa nchi na Amiri Jeshi Mkuu wa vyombo vya ulinzi na Usalama vya nchi ukataka alinganishwe na mjumbe au mbunge au waziri? Hilo haliwezekani fuatilia nchi zote ambazo wamekubali upuuzi huu utaona marais wao ni kama mapambo tu na wana jina lao eti wanabaki kuwa Ceremonial hawana mamlaka ya maamuZi ya nchi wapo wapo tu, hili halikubaliki Tanzania Rais ni MAMLAKA hata UKAWA wanalijua hili ndo maana wanaungana wakiamini kuwa watashinda nafasi ya Rais mwenye ambaye atakuwa na mamlaka!

Mungu Ibariki Tanzania!

Nawasilisha!
 
Ego naona hujamuelewa mtoa hoja,wewe umeganda kwenye issue ya ufalme,huo ni mfano tu ila hakuna tofauti ya Rais wetu,kwaniupatikanaji wake unajulikana ni kupitia nguvu ya umma,ballot power sasa usichokijua ni nini,akipigiwa kura na watu milioni 7 kati ya milioni 10 hii si inaonyesha kukubalika kwake?Je hii si ndo nguvu yake na mamlaka yake pia ya kiutawala?katiba lazima impe mamlaka makubwa yeye ndo tunamkabidhi nchi na majeshi yote sasa atakuaje na mamlaka madogo,just kuelewa tu hata baba katika familia ana mamlaka makibwa sembuse Rais?
 
mimi nadhani hujanielewa nilichokisema.

haijalishi raisi anachaguliwa na watu wangapi bali hoja hapa ni tunawezaje kudhibiti viongozi wasipore madaraka ya wananchi.

ni sawa na watu watatu kuwa na duka mkaamua kumchagua mtu wa kuendesha duka lenu. huyu mnatakiwa muwe na nguvu ya kumthibiti ninyi wenye duka ili asiwapore madaraka yenu ya kufanya anavyotaka.

mnaweza kumpa mtu madaraka kuendesha duka lenu mpaka mkashindwa kufuatilia mwenendo wa duka lenu akaligeuza kuwa lake na kwa katiba yenu akaonekana yuko sahihi kwani yote anayoyafanya ni kwa mujibu wa katiba yenu ya ushirikiano inavyosema.

ni katika dhana hiyo ya kuhakikisha viongozi wanaochaguliwa hawafanyi mambo wanavyotaka hata mkimchagua mtu kuwa raisi akaifanya familia yake kuwa kama wafalme wenu kwa maana kuchukua ukoo wake, ndugu zake na mengine kuwaweka KWENYE nafasi za kitaifa.

tuweke mifumo ambayo raisi wetu tunamheshimu ndio na anatuongoza lakini hatakiwi kuwa na madaraka makubwa ya kufikia hatua ya kuvunja sheria na hakuna wa kuhoji.

bali tunataka mifumo kama ya ulaya kuwa raisi anaweza kuwa madarakani na akapelekwa mahakamani, na lengo hapa si kumfunga raisi bali kufanya mifumo inayoangalia taifa.

Ego naona hujamuelewa mtoa hoja,wewe umeganda kwenye issue ya ufalme,huo ni mfano tu ila hakuna tofauti ya Rais wetu,kwaniupatikanaji wake unajulikana ni kupitia nguvu ya umma,ballot power sasa usichokijua ni nini,akipigiwa kura na watu milioni 7 kati ya milioni 10 hii si inaonyesha kukubalika kwake?Je hii si ndo nguvu yake na mamlaka yake pia ya kiutawala?katiba lazima impe mamlaka makubwa yeye ndo tunamkabidhi nchi na majeshi yote sasa atakuaje na mamlaka madogo,just kuelewa tu hata baba katika familia ana mamlaka makibwa sembuse Rais?
 
Lakini pia hatutaki katiba km ya kwetu ambayo inamfanya rais kuwa dampo la madaraka!!!!
 
mimi nadhani hujanielewa nilichokisema.

haijalishi raisi anachaguliwa na watu wangapi bali hoja hapa ni tunawezaje kudhibiti viongozi wasipore madaraka ya wananchi.

ni sawa na watu watatu kuwa na duka mkaamua kumchagua mtu wa kuendesha duka lenu. huyu mnatakiwa muwe na nguvu ya kumthibiti ninyi wenye duka ili asiwapore madaraka yenu ya kufanya anavyotaka.

mnaweza kumpa mtu madaraka kuendesha duka lenu mpaka mkashindwa kufuatilia mwenendo wa duka lenu akaligeuza kuwa lake na kwa katiba yenu akaonekana yuko sahihi kwani yote anayoyafanya ni kwa mujibu wa katiba yenu ya ushirikiano inavyosema.

ni katika dhana hiyo ya kuhakikisha viongozi wanaochaguliwa hawafanyi mambo wanavyotaka hata mkimchagua mtu kuwa raisi akaifanya familia yake kuwa kama wafalme wenu kwa maana kuchukua ukoo wake, ndugu zake na mengine kuwaweka KWENYE nafasi za kitaifa.

tuweke mifumo ambayo raisi wetu tunamheshimu ndio na anatuongoza lakini hatakiwi kuwa na madaraka makubwa ya kufikia hatua ya kuvunja sheria na hakuna wa kuhoji.

bali tunataka mifumo kama ya ulaya kuwa raisi anaweza kuwa madarakani na akapelekwa mahakamani, na lengo hapa si kumfunga raisi bali kufanya mifumo inayoangalia taifa.


Hao viongozi wanaopora madaraka yako wewe mwananchi umewaona wapi TAnzania?wanayapora kutoka wapi?kwani mamlaka ya viongozi wa Tanzania especially rais wetu yanatoka kwa nani?hivi mpaka sasa hujajua tu Wananchi ndo mamlaka yenyewe!Madaraka na mamlaka ya hao viongozi tunawapa sisi kikatiba kama hujui hiyo ni kazi nyingine ukisema wamekupora sikuelewi?Pia kuna Bunge/ wananchi ambalo linafanya kazi yake kutunga sheria na kupitisha mambo mbalimbali,Rais lazima awe na mamlaka yaliyoainishwa Kikatiba na si vinginevyo na ndiyo maana anaitwa Rais asipokuwa na mamlaka sio Rais huyo!!! Sasa wewe unaposema hatuna mfumo wa kushughulikia uvunjaji wa sheria za nchi kwa kiongozi endapo amethibitika kutenda makosa ya kuvunja Katiba nchi ambayo aliapa kuilinda na kuitetea sikuelewi, Tatizo lako unaendeshwa kwa hisia hapa!
 
Aise... Yaan watanzania wengine akili zao cjui wanatumia kufanyia nini??...

Wakati nchi nyingi duniani zinajitahidi kurudisha mamlaka kwa wananchi.. cha kushangaza Tanzania kuna mijitu inataka Rais awe na Mamlaka ambayo wakati mwingine ndiyo yanachangia ukiritimba na urasimu kwenye maendeleo ya taifa letu..
 
Aise... Yaan watanzania wengine akili zao cjui wanatumia kufanyia nini??...

Wakati nchi nyingi duniani zinajitahidi kurudisha mamlaka kwa wananchi.. cha kushangaza Tanzania kuna mijitu inataka Rais awe na Mamlaka ambayo wakati mwingine ndiyo yanachangia ukiritimba na urasimu kwenye maendeleo ya taifa letu..

Toa mifano ya nchi hizo na madaraka yaliyorudishwa na nchi hizo pia useme mfumo wa utawala wa nchi husika sio ukurupuke tu hapa na kuongea ovyo!
 
Toa mifano ya nchi hizo na madaraka yaliyorudishwa na nchi hizo pia useme mfumo wa utawala wa nchi husika sio ukurupuke tu hapa na kuongea ovyo!

Ukisharuhusu kufikiri kwa kutumia makalio huwezi kuelewa.. Maana we unachofikiri ni kuwasifia tu wale wanaokutuma..

Nataka nikwambie hata Katiba ya Tanzania ya mwaka 1977 inatambua.. 'Mamlaka ya Utawala yatatoka kwa wananchi'

Sasa kama wananchi ndiyo wanamamlaka juu ya utawala ndiyo maana kuna haja ya kumpunguzia huyu Rais ili mamlaka zaidi yarudi kwa wanaoyatoa

Mburura kasome tena.. sio unakurupuka tu.. huhitaji mifano ya nchi nyingine.. wakati Katiba yetu yenyewe inaelekeza hivyo
 
Ukisharuhusu kufikiri kwa kutumia makalio huwezi kuelewa.. Maana we unachofikiri ni kuwasifia tu wale wanaokutuma..

Nataka nikwambie hata Katiba ya Tanzania ya mwaka 1977 inatambua.. 'Mamlaka ya Utawala yatatoka kwa wananchi'

Sasa kama wananchi ndiyo wanamamlaka juu ya utawala ndiyo maana kuna haja ya kumpunguzia huyu Rais ili mamlaka zaidi yarudi kwa wanaoyatoa

Mburura kasome tena.. sio unakurupuka tu.. huhitaji mifano ya nchi nyingine.. wakati Katiba yetu yenyewe inaelekeza hivyo

Nilidhani unakuja na hiyo mifano kumbe unaongea kitu usichokijua ha ha ha ha pole sana majibu yako yanaonyesha ukomo wa uwezo wako wa kufikiri na inaonyesha umezoea kucopy na kupaste mawazo ya watu ukibanwa mbavu unakimbilia kutukana Ua not independent kwa hoja unazozitoa!nimekuambia toa reference ya hizo nchi badala yake unatokwa povu! Kama unajua Mamlaka ya utawala yanayoka kwa wananchi kelele za nini?Lazima utambue pia mamlka aliyonayo Rais yametoka kwa wananchi maana ndo waliomuweka madarakani,haiwezekani Rais akalingana na diwani wako never!
 
Mleta mada ungetoa mifano ya nchi ambazo kwa mfumo huu wa kupunguza madaraka kwa raisi zimeathirika na upunguzaji huo.. No research no right to speak..

Halafu msidhani kwamba raisi atakuwa ni wa ccm milele.. Atakapokuja raisi toka kwa chama kingine ndo mtakuja kulia na kusaga meno maana kwa katiba mlioipitisha wenyewe itaanza kuwala wenyewe..
 
Mleta mada ungetoa mifano ya nchi ambazo kwa mfumo huu wa kupunguza madaraka kwa raisi zimeathirika na upunguzaji huo.. No research no right to speak..

Halafu msidhani kwamba raisi atakuwa ni wa ccm milele.. Atakapokuja raisi toka kwa chama kingine ndo mtakuja kulia na kusaga meno maana kwa katiba mlioipitisha wenyewe itaanza kuwala wenyewe..

Naona hujaelewa debate inayoendelea hapa kasome vizuri topic ndo uje aisee!
 
Ukisharuhusu kufikiri kwa kutumia makalio huwezi kuelewa.. Maana we unachofikiri ni kuwasifia tu wale wanaokutuma..

Nataka nikwambie hata Katiba ya Tanzania ya mwaka 1977 inatambua.. 'Mamlaka ya Utawala yatatoka kwa wananchi'

Sasa kama wananchi ndiyo wanamamlaka juu ya utawala ndiyo maana kuna haja ya kumpunguzia huyu Rais ili mamlaka zaidi yarudi kwa wanaoyatoa

Mburura kasome tena.. sio unakurupuka tu.. huhitaji mifano ya nchi nyingine.. wakati Katiba yetu yenyewe inaelekeza hivyo

Hapa matusi sio eneo lake kama huelewi mada uliza!
 
Naona hujaelewa debate inayoendelea hapa kasome vizuri topic ndo uje aisee!

Hii sio debate.. Utakuwa na tatizo kama utaiita hii ni debate.. Ndo maana ckupata shida kuandika niliyoyaandika.. Ungemsaidia kumjibia kwa kutaja hizo nchi ambazo zimeathirika kwa mfumo huu wa kupunguziwa madaraka..

Vinginevyo huna sababu ya msingi ya kuandika ulichoandika..
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom