Nimeipitia katiba kipengere kwa kipengere.
Hakika imekaa vizuri sana. nimekuwa nikijiuliza wale wanaoipinga wanapinga kwa hoja zipi!!?
Ailimia kubwa mambo yaliyopendekezwa na tume ya Warioba yamo.
Eti kwa sababu tu kwamba serikali tatu haipo.
Asilimia kubwa ya watu wanaisoma kwa mrengo wa kuipinga. Hawako na free mind.
Kuna mambo mazuri sana mengi. Mfano:
Na kuna mambo mengi sana nitaendelea kuya toa.
Sasa mambo ya kupigiwa mizinga yako kwenye sheria sio kwenye katiba. Kumbuka hapa tunaongelea Katiba please tofautisha. Halafu mambo mengine ni ya itifaki tu sawa kaka. Jaribuni basi kupinga kwa hoja. Unaona sasa.Amir jeshi wa Tanzania ni nani? Je Rais wa Zanzibar anapigiwa mizinga kama nani? Sherehe za Mapinduzi nani anatangulia uwanjani?
Mimi sijakuelewa. Hivi neno TUNU kwako lina maana gani?Wewe pimbi unatakiwa kujua haki bila uwajibikiji ni 0 katibaa hii imetoa uwajibikiji kama tunu na viongozi hawaajibiki kabisa so sahau haya mambo ya kisiasa
Kwenye tatizo ni huko kwenye uongozi wa nchi. Kwa nini waliondoa vipengele muhimu kama wananchi kuwawajibisha wabunge na wanabunge kuwa watu wenye elimu ya form four? ndiyo maana bunge letu litaendelea kuwa substandard na lisilokuwa na viwango. Pia muundo huu wa muungano ni wa ovyo sana haijawai tokea. Kwa nini tusiwe na serikali moja au tatu ili muungano ueleweke? Sasa hivi Tanganyika inaminywa tu na wazanzibar wanadandia tu!
Hii katiba yetu huwezi kusimama hata kuilinganisha na katiba za nchi kama Kenya au SA au Ghana......haina viwango na ni ya kuundwa kimagendo kwa maslahi ya chama kimoja! Huu mpasuko wa kisiasa uliojitokeza lazima utaadhiri utekelezwaji wa katiba mpya pindi itakapokubaliwa na wananchi. Ila CCM kwa vile wanadhani watabaki madarakani milele, ndio maana wamepitisha katiba ya ovyo kama hii! Katiba inafaaa kuwa chama chochote kikishika dola kinaridhika na muundo wa serikali uliopo na si vinginevyo!
6.-(1) katika utekelezaji wa mamlaka au shughuli zozote kwa mujibu
wa katiba hii au sheria za nchi, misingi ya utawala bora katika ibara hii ni
lazima izingatiwe na kufuatwa na taasisi ya serikali, ofisa wa serikali au mtu
yeyote aliyepewa dhamana ya:
(a) kutumia au kutafsiri katiba hii;
(b) kutunga, kutumia au kutafsiri sheria yoyote; na
(c) kufanya au kutekeleza maamuzi ya sera za kitaifa.
(2) misingi ya utawala bora katika jamhuri ya muungano itajumuisha:
(a) uadilifu;
(b) demokrasia;
(c) uwajibikaji;
(d) utawala wa sheria;
(e) ushirikishwaji wa wananchi;
(f) haki za binadamu;
(g) usawa wa jinsia;
(h) umoja wa kitaifa;
(i) uwazi; na
(j) uzalendo.
Akishika dola CHADEMA au CUF au UKAWA wanavyojiita huoni kama kutakuwa na crisis? Lazima wataifanyia hiyo katiba fundamental changes na hiyo itakuwa katiba gani inayobadilishwa ovyo? Angalia nchi kama marekani akishika huyu au yule huwezi kubadilisha muundo wa serikali lakini hapa kila mtu ana lake kwa vile hakuna maridhiano kwa sababu CCM hakikusikiliza sauti za vyama vya upinzaniKwa nini ulinganishe na Nchi hizo?
Hujui kuwa UNITED Countris in Africa ni moja tu.
Duniani hazizidi Tano?
Nimejaribu kuweka vipengere vingi tu, vilivyo sahihishwa na kutoa vitu ambavyo vinabadilika.
Huwezi ukaweka maelezo marefu ya miiko ya watumishi wa umma kwenye katiba. sasa sheria zitafanya nini?
Huwezi ukaelezea kila kitu kwenye katiba ila katiba itatoa mwelekeo, kama hii ya sasa.
Tatizo lako ndugu yangu unacomment tuuuuuuu. Hutoi ni vipengere vipi vitakavyo badilishwa? Sijui hata kama umeisoma hii Rasimu.Hebu nakuomba tujadili pointi kwa point. Niambie kifungu kipi kinacho weza kubadilishwa kwenye katiba wakiingia hao unaowasema?Akishika dola CHADEMA au CUF au UKAWA wanavyojiita huoni kama kutakuwa na crisis? Lazima wataifanyia hiyo katiba fundamental changes na hiyo itakuwa katiba gani inayobadilishwa ovyo? Angalia nchi kama marekani akishika huyu au yule huwezi kubadilisha muundo wa serikali lakini hapa kila mtu ana lake kwa vile hakuna maridhiano kwa sababu CCM hakikusikiliza sauti za vyama vya upinzani
56.-(1) Kila mtu atakuwa na uhuru wa kushiriki kwenye mambo
yanayoendeleza na kukuza sanaa, taaluma, ubunifu na ugunduzi.
(2) Kila mtu atakuwa na uhuru wa kujifunza, kufundisha, kutafiti na
kueneza matumizi ya matokeo ya utafiti kulingana na kanuni za kitaaluma na za
kiutafiti.
(3) Serikali itakuza na kuendeleza utafiti, ubunifu na ugunduzi katika
sanaa, sayansi na teknolojia kwa kutunga sheria ambazo:
(a) zitalinda hakimiliki na hataza na haki za wabunifu, watafiti na
wasanii;
(b) zitawezesha taasisi za elimu na za utafiti kutumia ugunduzi wao kwa
manufaa ya taifa;
(c) zitasimamia uhamishaji wa sayansi na teknolojia;
(d) zitawezesha kukuza rasilimali watu kwenye nyanja za kitaaluma,
sayansi, teknolojia na ubunifu;
(e) zitalinda na kusimamia ubora wa taaluma, utafiti na matumizi ya
ugunduzi na ubunifu; na
(f) zitafafanua mambo mengine yanayohusu hakimiliki na hataza.
Utaonaje ubaya wake na wewe ni gamba?
Hapa tunaenda kwa vitendo nipe kifungu kinacho ongelea rais kuteua kuku plz.
Akishika dola CHADEMA au CUF au UKAWA wanavyojiita huoni kama kutakuwa na crisis? Lazima wataifanyia hiyo katiba fundamental changes na hiyo itakuwa katiba gani inayobadilishwa ovyo? Angalia nchi kama marekani akishika huyu au yule huwezi kubadilisha muundo wa serikali lakini hapa kila mtu ana lake kwa vile hakuna maridhiano kwa sababu CCM hakikusikiliza sauti za vyama vya upinzani
Pili, hamjajifundisha chochote kutokana na kura ya maoni ya scotland? Sasa hivi England wanalalamika wabunge wa scotland iweje wanajadili mambo yasiyowahusu. Huo ni muungano wa zaidi ya miaka 300. lakini it was inevitable. na hapa pia mpende msipende lazima Tanganyika itadai haki yake at some point, iwe sa hivi au baadaye tukiwa hatupo, iwe kwa amani au fujo. Lakini CCM hamjali vizazi vijavyo mnachokiona ni hapa na sasa hivi na vitambi vyenu.
Tatizo lako ndugu yangu unacomment tuuuuuuu. Hutoi ni vipengere vipi vitakavyo badilishwa? Sijui hata kama umeisoma hii Rasimu.Hebu nakuomba tujadili pointi kwa point. Niambie kifungu kipi kinacho weza kubadilishwa kwenye katiba wakiingia hao unaowasema?
Unataka nikuwekee sura nzima ya saba hapa? Inaanza hivi;
SURA YA SABA
MUUNDO WA JAMHURI YA MUUNGANO
Muundo wa Muungano
70. Jamhuri ya Muungano wa Tanzania itakuwa na muundo wa Serikali
mbili ambazo ni:
(a) Serikali ya Jamhuri ya Muungano; na
(b) Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Ukibadilisha hapo umeshaibadilisha katiba nzima maanake msingi wa katiba ni muundo wa muungano. Hii katiba tunayo wote na nakuhakikishia kwamba nimeisoma mara mbili juu chini!
Angalia hapa tena.
Mbona mkalia kutuambia masuala ya haki za wavuvi ,wakulima,wafugaji kwa nini hamsemi kama mbuge anaruhusiwa kugombea mpaka atakapochoka yeye! Mtu anayejua kusoma na kuandika anaweza kuwa mbuge determination ya mtu anayejua kusoma na kuandika unaijuaje? Manake hata STD VII wanamaliza hawajui kusoma na kuandika?kwa nini mumewaondolea wananchi mamlaka ya kumwajibisha Rais? Mmesema idadi ya wabunge ktk bunge iwe 50 kwa 50 bila hata kuonesha hyo inapatikanaje nakwambia hvi hii katiba endapo itapita mungu nijalie uzima ktk kipindi cha miaka 10 tu itafanyiwa amendment kwanza hatutakuwa na wazee kama wewe Bungeni
Hayo mambo yote ya wananchi bado yangepatikana iwe kwa serikali moja, mbili au tatu. Hiyo tu ni danganya toto ambayo CCM wanaitumia kuwahadaa wananchi kama wewe. Hivi unadhani kwa serikali tatu 50/50 ya wanawake isingepatikana? Au mambo ya wakulima, wavuvi, wachimba madini na kadhalika yasingezingatiwa? Mambo hayo yanatekelezeka kwa muundo wowote wa serikali kwa hiyo hoja yako haina mashiko!Kwahiyo hapa hoja ya UKAWA ni serikali 3, mambo mengine ya wananchi wao hayawahusu.
Mbona mkalia kutuambia masuala ya haki za wavuvi ,wakulima,wafugaji kwa nini hamsemi kama mbuge anaruhusiwa kugombea mpaka atakapochoka yeye! Mtu anayejua kusoma na kuandika anaweza kuwa mbuge determination ya mtu anayejua kusoma na kuandika unaijuaje? Manake hata STD VII wanamaliza hawajui kusoma na kuandika?kwa nini mumewaondolea wananchi mamlaka ya kumwajibisha Rais? Mmesema idadi ya wabunge ktk bunge iwe 50 kwa 50 bila hata kuonesha hyo inapatikanaje nakwambia hvi hii katiba endapo itapita mungu nijalie uzima ktk kipindi cha miaka 10 tu itafanyiwa amendment kwanza hatutakuwa na wazee kama wewe Bungeni
Hayo mambo yote ya wananchi bado yangepatikana iwe kwa serikali moja, mbili au tatu. Hiyo tu ni danganya toto ambayo CCM wanaitumia kuwahadaa wananchi kama wewe. Hivi unadhani kwa serikali tatu 50/50 ya wanawake isingepatikana? Au mambo ya wakulima, wavuvi, wachimba madini na kadhalika yasingezingatiwa? Mambo hayo yanatekelezeka kwa muundo wowote wa serikali kwa hiyo hoja yako haina mashiko!
Kwajinsi ulivyo comment unaonekana hujaisoma hii rasimu. Nakuomba nivyema ukaisoma badala ya kuleta bra bra hapa. hebu nipe kifungu kinachosema mbunge asiwe na kikomo.
Katiba ya warioba haingeongelea mambo hayo kwa sababu kwenye mfumo wa serikali tatu, hayo siyo mambo ya muungano! Hayo mambo yote yangetajwa kwenye katiba ya Tanganyika na katiba ya Zanzibar. CCM wamewatupia changa la macho tena wananchi kama wewe kwa kuwaambia eti mzisome rasimu zote mbili mzilinganishe wakati siyo sahihi kufanya hivyo! Ya warioba ilijikita kwenye yale mambo ya muungano tu! Mambo ya ardhi, vijana, wakulima, wavuvi na kadhalika yote yangetajwa kwenye katiba za nchi washirika. Sijui umeelewa?!Katiba ya warioba haikusema hayo.
Nakuomba ndugu unijibu maswali yangu mengi tu nimekuuliza unayakwepa kwepa tu.