Yan kila mtu anaelewana n mwenzie...!!ht kusaidiana tunasaidiana kulingana na namba...!!usiombe ukopeshwe na namba sio..atalalamika sio kdg....!!Hii imekaa poa sana mkuu..na bila shaka mnajuana....
😂😂😂Dah nyieKiukweli hakuna ndugu yangu nae mpenda wala anaenipendaa yaani ni taflani!!
They always say, a sister is a deputy mother. First born akiwaga mdada kwenu ni bora kuliko akiwa kakaMy big sister, rafiki yangu kweli kweli, natamani angekuwa first born tu yani....mabraza michosho tu yaani.
Kweli kabisa, yuko peke yake lakini she plays a massive role!They always say, a sister is a deputy mother. First born akiwaga mdada kwenu ni bora kuliko akiwa kaka
Kweli kabisa, yuko peke yake lakini she plays a massive role!
Mkuu wewe upo kama mimi.Alizaliwa miaka 8 baada yangu. Nikiwa mtoto wa 3 kuzaliwa kati ya watoto 5, huyu yeye ndie kitinda mimba cha Mama Fohadi na ndiye kaka wa mwisho wa familia. Japokuwa nina upendo wa dhati kwa ndugu zangu wa damu wote ila upendo kwa huyu jamaa naona kabisa umepitiliza. Hajui na hakuna anejua ila mimi binafsi ndiye ninaejua.
Nikiwa na miaka 11, yeye alikuwa na miaka 3. Kipindi hicho nilikuwa kila nikitoka shule lazima niende uwanjani kucheza chandimu na watoto wenzangu. Mara nyingi kati ya hizo, nilikuwa nambeba mgongoni naenda nae hadi uwanjani, namkalisha sehemu mimi nacheza mpira nikimaliza tunarudi wote home. Nilikuwa napenda sana kutembea nae popote pale na siku zote nilitamani kumfanya awe proud na sisi wakubwa zake.
Nikiwa kama Kaka mkubwa katika familia nilitamani kumuonesha upendo na raha ya kuwa na kaka mkubwa kwani sikubahatika kuwa na kaka mkubwa. Mimi ndiye mtoto wa kiume wa kwanza katika familia yetu. Kwetu sisi, mtoto wa kwanza na wapili wote ni wakike na sisi tuliobaki (3,4,5) wote ni wakiume huku mimi nikiwa ndiye 'brother kaka'.
Wakati fulani nimemaliza NECTA ya form two, nilikuwa siendi shule hivyo kila siku nilikuwa namsindikiza asubuhi hadi shule kule alikokuwa anasoma chekechea. Sio kwamba asingeweza kufika peke yake hapana, ila nilitamani nimuoneshe kuwa mimi ni mmoja wa kaka zake na anapaswa kujivunia mimi/sisi.
Sikumbuki kama kwenye maisha yangu ya kujitambua nimewahi kumpiga yule dogo. Sikuwahi kumdekeza ila sikuwahi kuwa katili kwake. Pengine kutokana na gap kubwa la umri kati yetu, kadri miaka ilivyokuwa inasonga ndivyo tulivyozidi kuwa sio watu wa story nyingi.
Miaka imekatika, leo dogo amemaliza kidato cha nne na anajitambua. Pamoja na kukua kiumri, ila bado namchukulia kama yule yule niliyekuwa nambeba mgongoni. Kwa wakati huu ndipo nimegundua nampenda sana huyu jamaa kuliko ndugu zangu wengine japo wote nawathamini na kuwapenda. Juzi dogo kanipigia simu akanambia anatamani sana nimpeleke kwa mkapa tukaangalie Derby ya kariakoo. Sikuweza kukataa ila pia kwa sababu zilizo nje ya uwezo wetu (mimi na yeye) hatukuweza kwenda uwanjani na pengine Mungu alitaka hela zetu za viingilio zipone. Hakuna ombi ambalo amewahi kuniomba nikakataa. Ila ile request yake ilinifanya nifikilie zaidi jinsi gani mkubwa anabeba tumaini la wadogo zake when they face imposibilities.
Mara nyingi kila nikimuangalia huwa najiona nipo responsible kwa ajili ya kesho yake. Hajui kina cha upendo wangu kwake kilivyo na sitataka hata siku moja ajue. Ila kiukweli harakati zangu zote za kimaisha ambazo huwa nazifanya kwa kutokata tamaa yeye huwa ni mmoja wa watu wanaonipush kuzidi kupambana zaidi ili siku moja niwe funguo ya dunia yake awe anachotaka.
Hata mimi sijui kwanini nampenda sana, sifahamu labda kwakuwa ni last born nampa upendo ulio jaa huruma ndani yake.. Kitu pekee ninachojua ni kuwa huyu nampenda sana kuliko ndugu zangu wengine. Wale ndugu zangu 3 upendo wangu kwao ni 100% ila huyu ni zaidi ya 100%.
Ninamshukuru Mungu sina ndugu ninaemchukia kati ya ndugu zangu. Wewe unampenda nani zaidi kati ya ndugu zako wa damu? Kwanini huyo?
BIG UP MKUUMkuu wewe upo kama mimi.
Mimi mdogo wangu wa mwisho kwa mama tumepishana miaka 9.
Huyu dogo nampenda kama mdogo wangu kwa sababu mimi ndio kaka yake kwa mama tupo watatu wa kiume wawili wa kike mmoja,na mimi ndo kaka.
Ila mama huwa ananiambia kwamba mdogo wako anakupenda na kukukubali sana.
Dogo nampa lesson mbalimbali na zinamuingia,nikikaa nae tunaongea majirani wanasema wale jamaa mambo yao kama wazee.
Lakini mimi dogo namfundisha mambo ya ulimwengu,namfundisha kuwa hii sasa ni dunia ya hoja na uthubutu na dunia ya kuidhibiti nafsi yako.
Kiukweli dogo nimemsaidia sana kuwa mtu jasiri hata shuleni alikuwa anaongoza kiufaulu baada ya kumtia ujasiri wa kuthubutu,na hayo ndo katika mambo dogo ananikubali mnoo.
Mpaka sasa hivi tuko maeneo mbalimbali lakini tunawasiliana kwa simu.
Nilichojifunza kuhusu hawa wadogo zetu ni kuwa motivation quotations zinasaidia kwao