Kati ya Magamba na M4C nani zaidi Jangwani

mfumo wa ccm uliotengenezwa kwa miaka mingi, unawafanya wanachama na viongozi wa ngazi za chini kufanya lolote watakaloambiwa na viongozi wao wa juu ili waweze kuingia ktk uongozi wa ngazi za juu, utawawezesha viongozi wa chama hiki kuendelea kuwanyonya wananchi wa kawaida ambao hawana fedha kwa kipindi kirefu zaidi, huku viongozi hawa wa chini wakiwa na ndoto ya siku moja nao kutapata nafasi ya kushika madaraka ya juu ktk chama na serikali. Wanachama wa kawaida wanahangaika na shilingi elfu tatu tatu wanazopewa wakihudhuria mikutano au vikao vya chama. Kwa muda mrefu wanaotetea chama hiki wana uvivu wa kufikiri, wanadhani wakipata ugali wa siku moja unatosha, kumbe wanaacha deni kubwa kwa watoto wao ambao hawana shule za kueleweka, huduma mbovu za hospitali, usafiri, na vingi tu nk.

Kwa wapenda mabadiliko hawana budi kuangalia mbinu mpya, hasa ya kutafuta volunteers wa kutosha kutoa elimu maeneo ya vijijini kwa wanawake na wanaume maskini wa nchi hii, na baadhi ya vijana ambao bado wanashabikia ccm, nadhani ni kwa ajili ya njaa au bongo lala. Kijiji kwa kijiji, mtaa kwa mtaa, kijiwe kwa kijiwe mpaka elimu ya ukombozi itambae kwa wote, waondoe chama hiki dhalimu. Wanamabadiliko wasipopata ushindi mkubwa ktk uchaguzi wa mwaka 2015, ccm watafanya ujanja wao na kuendelea kubaki madarakani kimabavu! Kila la kheri wapenda mabadiliko!
 
wakati unawaza hivyo, jiulize kwa nini cdm ina wafuasi wengi kutoka mikoa ya mara, mwanza, shinyanga, mbeya, kagera na kigoma kuliko hata hiyo mikoa unayotaka kuaminisha watu kuwa ni ya cdm zaid. Then jiulize tabora ilikuwaje! Alafu utafiti watu wa hiyo mikoa pamoja na hiyo ya kaskazini unayoshupalia elimu yao ipoje? Misimamo yao ipoje? Vip kimaendeleo wapoje? Je waliowahi kupata nafasi za uongozi japo za kawaida kutoka mikoa hiyo kama kina sokoine, mrema, nyerere, lugakingira, waitara, marando na wengineo walikuwaje? Je bila ya hao wenye maduka unaosema serikali itapata wapi kodi yake? Hebu elimika na ondokana na fikra mgando ambazo hazitokaa zikusaidie popote duniani!
hoja si kuwa ni nani zaidi. Hebu tujiuliuze ni nani mhalifu kati yao. Maana kuwadanganya wananchi kwa ahadi kemkem za maisha bora kwa KILA mtz kwa kasi zidi , ari zaidi na nguvu zaidi haikuwa kweli bali kurubuni watz badala yake wameiibia nchi kwa kasi zaidi, ari zaidi na kwa nguvu zaidi WAKIFAIDIKA WAO NA FAMILIA ZAO TU WATZ TUKO HOI BIN TAABANI. Ktk hali kama hii watz tuache kubaguana kwa ukanda kwani sera kama za kuongeza bei ya vitu kama mafuta ya taa na nishati ya umeme zina mrengo wa kuwafaidisha watawala na wafanyabiashara uchwara wenye ushirika na serkali hii. Kwa hakika hatuwezi kugawanyika kuwakamata wezi kwa kuangalia ukanda. Umoja ni nguvu utengano ni udhaifu. Hima tuondoe utawala mbovu wa ccm na serkali iliyojaa viraka vya maovu miaka 50 sasa . HUWEZI KUTOKA UKIWA UMEVAA SURUALI NA SHATI LILILOJAA VIRAKA. CCM IMEJAA VIRAKA VYA KILA UOVU . Hatuwezi kuvUmilia kwani madhara yake yanaendelea the next 1000 years to our descendants hata vizazi 20 . naam nawapatiliza wao wana wao na wana wana wao hata kizazi cha nne kwa maovu yao. Angalia corruption ilivyoidhibiti italia dola iliyokuwa imara hapo kale
 
Back
Top Bottom