Kati ya BABA na MAMA nani bora zaidi

Kati ya BABA na MAMA nani bora zaidi

ladyfurahia

JF-Expert Member
Joined
May 10, 2011
Posts
14,758
Reaction score
9,592
Habari wanajamvi

Ni matumaini yangu kuwa mko wazima wa afya njema na mnaendelea vizuri na shughuili
zenu, wengine mko katika shamrashamra za weekend na wengine katika hafla mbalimbali
za weekend. na wengine mmepata na mambo ya huzuni na mko katika huzuni mbalimbali
wote hawa nawatakia kheri na faraja kwa wote wapitiao matatizo/mapito mbalimbali. Na
kwa wale waliopoteza wazazi wao awe mmoja au wote pokeeni faraja ya upendo toka
kwangu Lady Mungu awape NGUVU na changamko la furaha tele maishani mwenu awakumbuke
katika mambo yenu yote.

Leo tena nimetoka jambo hili ambalo nimeona nishirikiane nanyi kwa kutoa madukuduku, maoni
hata kuuleta changamoto humu mjengoni, Wapendwa leo nimetoa mada hii inayosema kuwa
'Kati ya BABA na MAMA yupi bora zaidi au yupi umemwona anatekeleza wajibu wake kwa makini
kwa uwajibikaji wake kama kiongozi katika familia. Na je anaweza kuleta mapinduzi katika familia
yake?.

Wapendwa wenzangu leo nimeona niwape changamoto ya aina yake hapa nanyi mtoe yale
yaliyojaa mioyoni mwenu kuhusu ni nani anatakiwa kuwa wa pekee kwako au ninani
unayependa zaidi kuliko mzazi mwingine? na ni nani anayetelekeza wajibu wake kwa usahihi?

Kwa upande wangu mm naona anayefaa zaidi kuwa bora ni MAMA kwani mama anafanya
majukumu kwa uthabiti na kiongozi wa kuigwa kwa watoto kwani ndiye anayejali, kupenda
na kutunza familia kwa makini zaidi kuliko BABA kwani mababa wengi siku hizi hawatunzi
familia zao wengine wamediriki hata kukimbia familia zao kutokana na ugumu wa maisha,
Wengine wamewasaliti wake zao na wengine wameona kuwa familia zinawachosha na kuto
kutaka kutekeleza yale majukumu yao yani ulezi wa watoto na hatimaye watoto wengi
wanakuwa watoto wa mitaani kutokana na kukosa malezi ya pande zote mbili. Wengine
wamejiingiza katika mambo mabaya kutokana na BABA kutokuwapenda, kuwalinda na kutojali
familia zao. hivi ni kwanini jamani inakuwa hivi?

Ni nani anatakayeweza kuleta mapinduzi katika familia ni nani anayeweza kuleta mageuzi
ndani ya familia? wapendwa marafiki zangu Je ni nani unayedhani kuwa ni bora zaidi kwako
kuliko mwingine, ni mzazi gani bora kati ya BABA na MAMA ambaye ni mtunzaji wa familia kwa
makini na anayependa familia? Kwa mtazamo wako ni nani ambaye kwako rafiki waona ni wa
muhimu sana kwako? Hiyo ni changamoto kwako mpendwa rafiki yangu, Je ni nani?

Nawatakia baraka, furaha, na upendo na amani tele kwa weekend njema hii.

Angalia ni nani kati ya MAMA na Baba ambaye ni bora zaidi huyu ni Mama ambaye yuko
na mtoto wake akiwa anamjali na kuonesha Upendo wa familia yake mother baby.jpg Hapa ni BABA ambaye anaonesha kutokujali familia yake angalia hapa father read newspaper.jpg KWA MTAZAMO WAKO WEWE UNAONA YUPI AMBAYE ANAJALI FAMILIA YAKE NA KUITUNZA

Mimi Lady naona MAMA ni bora na wa muhimu kwangu ila hata kwa BABA naye ni bora kwani pasipo yeye kwani ningetokea mjengoni hapa ila kwa mtazamo wote ni bora sijui wewe mwenzangu rafiki yangu KATI YA BABA NA
MAMA NANI NI BORA ZAIDI?
 
Hakuna kama mama ktk viumbe bhana!!
Kuanzia tumboni mpaka kukutawaza/kukuogesha achilia mbali kuvumilia usumbufu wa kutwa nzima na usiku.
Nani kama mama????
 
Dini ya kiislam inampa mama asilimia sabiini na tano. 75% so kiislam mama ni bora kuliko baba
 
Sijui kwa nini tunasema kati ya baba na mama nani zaidi! Mtizamo wangu, nimelelewa na Baba, mama yangu alifariki nikiwa 2yrs old lkn baba alitulea watoto 5 bila ubaguzi wala niniktk situation km hii mnasemaje wadau! kuna waliotupwa na kutelekezwa na mama zao! bado mama is the best?
 
ila mkumbuke baba akikataa mimba mama atamtupa mtoto kwa kutambua umuhimu wa baba
 
Wote ni bora ila mom is the best........
 
Mom is the best of the best ila sometime moms get too emotional then you need the DINGI to take control n restore oder!
 
hii issue iko very personal!kwa sababu moja kubwa kwamba kunavitu vingi vinatokea wakati mtoto hayupo(yaani ikiwa mimba)mfano:mimi nina mke na mtoto mmoja mtoto anampenda sana mama yake kwa sababu wako wote muda mwingi sana na mimi muda mwingi nawaza pesa ili nikirudi nyumbani wife na mtoto wafurahi.lakini kuna siri kubwa sana nimeificha juu ya huyu mtoto na mama ake ameniambia kamwe nisije kumwambia mtoto it very painfull!inshort nilipigana mimi peke yangu kufanya juu chini wife hatoi mimba !kwani huo ndo ulikuwa msimamo wake toka siku ya kwanza alipogundua ana mimba!
 
siku ukifanikiwa kufahamu mbegu yako imetoka wapi itakuwa vyema. japo mama ndo mbebaji lakini na anaweza dhulumu baba akijisikia
 
baba ni baba na mama ni mama.
baba wote hawako sawa kama vile mama wote hawako sawa.
kila mtu ahukumiwe kwa makosa yake mwenyewe na kamwe asihukumiwe kwa jinsia yake.
Mama yangu ni tofauti na mama yako, kama alivyo baba yako tofauti na baba yangu.
Mungu ambaye ni mjuvi wa kila kitu angemuumba mama pekee au baba pekee kama kati yao mmoja angekuwa bora zaidi.
 
Baba na Mama wote ni bora ila wamepewa majukumu tofauti. Ni upumbavu kusema kuwa mama ni bora zaidi eti kwa vile anabeba mimba, ananyonyesha, anafua nepi n.k. Hayo majukumu mama hakujipa pengine eti ana huruma na familia ila alijikuta ameumbwa hivyo. Mungu alikuwa na makusudi. Kwani baba angekuwa ana uwezo wa kubeba mimba angekataa kufanya hivyo???

Haya masuala ya siku hizi ya ''nani kama mama'' yamekuwa yakichochewa zaidi na harakati za kuondoa mfumo dume. Kumbukeni hakuna Mwanamke bila mwanamume kwa sababu lazima mbegu ya baba itoke iende ikarutubishe yai la mama ili mtoto apatikane. Lakini mwanamume alikuwepo kabla ya mwanamke kuumbwa.

Suala la mama kuwa karibu zaidi na watoto kuliko baba aliwezi ku-justify ubora wa mama kwa sababu baba ameumbwa kuwa mtafutaji, so mara nyingi yuko nje ya familia anatafuta.

Pale Eden Garden, mwanadamu alipewa adhabu. Mwanamume aliambiwa atapata chakula chake kwa jasho tena chakula chenyewe atakipata kwa kukitafuta kwenye miiba- no easy task. Mwanamke yeye aliambiwa atazaa kwa uchungu.

Hivi, nauliza tu: Mwanzoni Mungu alikuwa na lengo la kumuumba mwanamke au mwanamume peke yake. Kwa wale wanaosoma maandiko Mungu alisema na tumuumbe mtu kwa mfano wetu. Kutoka mavumbi ya ardhi akamuumba mtu mwanamume. Baadaye akamwangalia mtu aliyemuumba. Akaona si vema awe peke yake, Nitamfanyia msaidizi wa kusaidiana naye. Akampa Adamu nusu kaputi, akamfanyia operesheni akatoa ubavu mmoja akaufanya kuwa mtu mwanamke. Wanatheolojia tusaidieni, Hivi kwa niniMungu amtoe Adamu ubavu kwa ajili ya kumuumba mwanamke asichukue mavumbi ya ardhi kama alivyofanya kwa Adamu???

Baba ni Bora ndo maana Mungu akamuumba kwanza tena akitegemea peke yake anatosha lakini mama ni bora pia kwa sababu Mungu aliona Baba hajakamilika bila kumuumba Mama. Need I say more???
 
Baba na Mama wote ni bora ila wamepewa majukumu tofauti. Ni upumbavu kusema kuwa mama ni bora zaidi eti kwa vile anabeba mimba, ananyonyesha, anafua nepi n.k. Hayo majukumu mama hakujipa pengine eti ana huruma na familia ila alijikuta ameumbwa hivyo. Mungu alikuwa na makusudi. Kwani baba angekuwa ana uwezo wa kubeba mimba angekataa kufanya hivyo???

Haya masuala ya siku hizi ya ''nani kama mama'' yamekuwa yakichochewa zaidi na harakati za kuondoa mfumo dume. Kumbukeni hakuna Mwanamke bila mwanamume kwa sababu lazima mbegu ya baba itoke iende ikarutubishe yai la mama ili mtoto apatikane. Lakini mwanamume alikuwepo kabla ya mwanamke kuumbwa.

Suala la mama kuwa karibu zaidi na watoto kuliko baba aliwezi ku-justify ubora wa mama kwa sababu baba ameumbwa kuwa mtafutaji, so mara nyingi yuko nje ya familia anatafuta.

Pale Eden Garden, mwanadamu alipewa adhabu. Mwanamume aliambiwa atapata chakula chake kwa jasho tena chakula chenyewe atakipata kwa kukitafuta kwenye miiba- no easy task. Mwanamke yeye aliambiwa atazaa kwa uchungu.

Hivi, nauliza tu: Mwanzoni Mungu alikuwa na lengo la kumuumba mwanamke au mwanamume peke yake. Kwa wale wanaosoma maandiko Mungu alisema na tumuumbe mtu kwa mfano wetu. Kutoka mavumbi ya ardhi akamuumba mtu mwanamume. Baadaye akamwangalia mtu aliyemuumba. Akaona si vema awe peke yake, Nitamfanyia msaidizi wa kusaidiana naye. Akampa Adamu nusu kaputi, akamfanyia operesheni akatoa ubavu mmoja akaufanya kuwa mtu mwanamke. Wanatheolojia tusaidieni, Hivi kwa niniMungu amtoe Adamu ubavu kwa ajili ya kumuumba mwanamke asichukue mavumbi ya ardhi kama alivyofanya kwa Adamu???

Baba ni Bora ndo maana Mungu akamuumba kwanza tena akitegemea peke yake anatosha lakini mama ni bora pia kwa sababu Mungu aliona Baba hajakamilika bila kumuumba Mama. Need I say more???

...NO...
 
Baba na Mama wote ni bora ila wamepewa majukumu tofauti. Ni upumbavu kusema kuwa mama ni bora zaidi eti kwa vile anabeba mimba, ananyonyesha, anafua nepi n.k. Hayo majukumu mama hakujipa pengine eti ana huruma na familia ila alijikuta ameumbwa hivyo. Mungu alikuwa na makusudi. Kwani baba angekuwa ana uwezo wa kubeba mimba angekataa kufanya hivyo???

Haya masuala ya siku hizi ya ''nani kama mama'' yamekuwa yakichochewa zaidi na harakati za kuondoa mfumo dume. Kumbukeni hakuna Mwanamke bila mwanamume kwa sababu lazima mbegu ya baba itoke iende ikarutubishe yai la mama ili mtoto apatikane. Lakini mwanamume alikuwepo kabla ya mwanamke kuumbwa.

Suala la mama kuwa karibu zaidi na watoto kuliko baba aliwezi ku-justify ubora wa mama kwa sababu baba ameumbwa kuwa mtafutaji, so mara nyingi yuko nje ya familia anatafuta.

Pale Eden Garden, mwanadamu alipewa adhabu. Mwanamume aliambiwa atapata chakula chake kwa jasho tena chakula chenyewe atakipata kwa kukitafuta kwenye miiba- no easy task. Mwanamke yeye aliambiwa atazaa kwa uchungu.

Hivi, nauliza tu: Mwanzoni Mungu alikuwa na lengo la kumuumba mwanamke au mwanamume peke yake. Kwa wale wanaosoma maandiko Mungu alisema na tumuumbe mtu kwa mfano wetu. Kutoka mavumbi ya ardhi akamuumba mtu mwanamume. Baadaye akamwangalia mtu aliyemuumba. Akaona si vema awe peke yake, Nitamfanyia msaidizi wa kusaidiana naye. Akampa Adamu nusu kaputi, akamfanyia operesheni akatoa ubavu mmoja akaufanya kuwa mtu mwanamke. Wanatheolojia tusaidieni, Hivi kwa niniMungu amtoe Adamu ubavu kwa ajili ya kumuumba mwanamke asichukue mavumbi ya ardhi kama alivyofanya kwa Adamu???

Baba ni Bora ndo maana Mungu akamuumba kwanza tena akitegemea peke yake anatosha lakini mama ni bora pia kwa sababu Mungu aliona Baba hajakamilika bila kumuumba Mama. Need I say more???

Pamoja na ukweli wa uliyoandika. To me My Mother is the best..!
 
mama mama mama! mama huyo mama! mama huyo mama! kwakweli wababa wengi wanakwepa majukumu ya familia na kuwaachia wamama. binafsi mama ni zaidi.
 
Swali linarudi kwako mleta mada, kuku na yai kipi kilianza? Ukiweza kujibu hili, basi hata swali lako litaweza kupata jibu sahihi.
 
Back
Top Bottom