Kashfa ya Richmond: Lowassa, Karamagi na Dkt. Msabaha Wajiuzulu

Anaandika Baba Askofu Rev.Dr.Benson Bagonza (PhD), Mkuu wa KKKT Dayosisi ya Karagwe.
___
Edward Ngoyai Lowasa ameondoka. Yuko mahali salama pasipo na mgao wa umeme wala usanii wa treni za umeme. Amepumzika baada ya kazi ngumu. Anapokufa mtu mzito kama Lowassa, kuna makundi matatu hujitokeza;
1. Wanaolia
2. Wanaofurahia
3. Wasiojua kama walie au wafurahie.

Makundi yote matatu tunayo katika kifo cha Edward Lowasa. Mimi sijui nipo kundi gani lakini niseme mambo manne ninayokumbuka:

1. Dola yetu ina mihimili mitatu: Bunge, serikali na mahakama. Lakini Lowassa alisababisha kuzaliwa kwa mihimili mitatu ndani ya mhimili wa bunge:
  • Wa kwanza ni Spika Samwel Sitta
  • Wa pili ni Wabunge mitume wakiongozwa na Mwakyembe
  • Mhimili wa 3 ulikua Edward Lowasa mwenyewe.
Hakika Bunge la 9 halitasahaulika kwa WEMA na UBAYA wake.

2. Alikuwa mtetezi asiye na mtetezi. Alikitetea chama chake, kikamtelekeza. Alimtetea Rais wake akamsaliti. Aliitetea nchi lakini nchi ikawatetea watesi wake.

3. Aliwapenda Wamasai, lakini Watesi wake wakamchonganisha na Wamasai. Wakahoji umasai wake na kudai Lowassa ni Mmeru. Lakini upendo wake kwa Wamasai ukawa na nguvu kuliko fitina za watesi wake. Akiwa hai na akiwa maiti Edward amebaki kuwa Mmasai.

4. Alisalitiwa na wengi aliowasaidia. Baada ya kumtumia kwa maslahi yao na kumtelekeza alibaki na Regina. Tujifunze kujali familia zetu. Mwisho wa yote, mzigo unabebwa na familia. Mambo ya “Pengo halitazibika” ni ulaghai mtupu. Kufa uone watakavyoziba pengo hata kabla ya mazishi.

LOWASSA KATIKA UBINADAMU WAKE:
A. Aliwaamini watu kuliko walivyomuamini.

B. Aliuchukia umaskini kwa vitendo. Watesi wake wakatumia hoja hii kumchonganisha na wananchi maskini. Wakasahau kuwa hata maskini wanauchukia umaskini wao na wanatamani kutoka.

C. Aliamini uzalendo si umaskini. Unaweza kuwa tajiri na ukawa mzalendo.

D. Alitumikia vyama 2 vikubwa. Vikamchafua na kumsafisha. Vikambeza na kumtukuza. Ameondoka akiwa mshindi kwa vyama vyote viwili.

E. Ameishi duniani miaka 70. Lakini Historia yake ni ndefu kuliko miaka yake. Ni mfupi wa umri lakini mrefu wa historia. Nenda Edward. Pole kwa Mama Regina, Watoto na wajukuu.!

Sent using Jamii Forums mobile app
 




Ni kuwa mjadala wa Richmond ndio unaanza japo mbunge wa Kigoma Mjini ndugu Peter Serukamba alimtaka spika kumpa ufafanuzi kwanza kuwa ni kwanini Waziri mkuu hakupewa nafasi ya kujitetea kwenye kamati husika.

Waziri mkuu kaamua kujitoa kwenye meza na amekuwa mchangiaji wa kwanza kuchangia, nitawaambia kile ambacho yeye amechangia binafsi.

A Mchango wa Waziri Mkuu*

Ameanza kwa kumpongeza Mwakyembe na kusema amekuwa na mbwembwe nyingi sana .

Anasema hakuridhika na jinsi kazi hiyo ilivyofanywa na anamponda sana mwakyeme kwa yeye ni mwqanasheria na hakumfanyia Natural Justice, yeye binafsi kwani hawakumhoji hata siku moja.

Analalamika Waziri Mkuu kuwa hakupewa Natural Juctice kwani hakuitwa na anasema kuwa alikuwa tayari kwenda hata kwa miguu kwenye kamati husika za bunge.

Anasema kuwa ameonewa sana na amedhalilishwa sana na kamati na kuwa ametuhumiwa bila hata ya kuulizwa hata jambo moja.

Anasema kuwa yeye ameonewa na anasema kuwa kwenye taarifa yao hakuna hata taarifa moja iliyotoka kwenye ofisi ya waziri mkuu , na anasema kuwa ingekuwa heshima kama angepewa nafasi ya kujitetea.

Analaumu kuwa kama wanaweza kumponda Waziri Mkuu kiasi hicho je?mwananchi wa kawsaida anaweza kutendewa haki?

Waziri mkuu ametangaza kuwa amejiuzulu na amemwandikia barua Rais Kikwete.

Zitto anataka mwongozo wa spika juu ya Waziri Mkuu kujiuzulu na anasema kuwa kama Waziri Mkuu amejiuzulu basi na baraza zima lazima lijiuzulu kwani Rais aliteua baraza kwa kushauriana na Waziri Mkuu.

Spika anakataa kuwa baraza zima haliwezi kujiuzulu , mpaka apate barua ya Rais.

Ni kuwa bunge bado linajikanganya sana na hali inawatisha hata wabunge na kwa sasa spika anajiuliza anawezaje kuliendesha bunge kaomba kupewa ushauri na wabunge .

Kuna hali ngumu sana kwa spika na haswa baada ya Zitto kutaka baraza zima lijiuzulu ili kuwweza kumpa rais muda wa kutangaza baraza jipya la mawaziri .

Mbunge wa CCM masilingi anasema kuwa jambo hilo lipelekwe kwenye kamati ya wabuinge wa kamati ya CCM ili wakajadili sijui kama hapo kuna mwelekeo kwa sasa .

Masilingi anatak bunge liahirishwe ili wakajadili kwenye kamati ya CCM .

Zitto anatoa hoja kuwa bunge liahirishwe kwa muda kwanza ili kuweza kuijadili hoja hiyo hapo baadae ,kamnyima mdee halima nafasi ya kutoa taarifa .

Ni kuwa bunge limeahirishwa hadi saa kumi na moja jioni na wabunge wa CCM wameenda kujipanga sijui watakuja na ajenda ipi na rais bado hajajibu barua ya Lowassa ya kujiuzulu.

Naitafuta barua hapa nikiipata tuu naiweka wakuu kaeni mkao wa kula humu leo.

Hakuna waziri ambaye ameenda kumpa pole isipokuwa Batilda tu, hapa kuna ujumbe mzito sana na umejificha.

Nitaendelea kuwapa yanayojiri hapa

B. Hotuba Kamili ya Mheshimiwa Edward Lowassa





==================
C. Vyombo vya Habari vya Kimataifa


D. Rais wa JMT aridhia maombi ya Waziri Mkuu Kujiuzulu



E ****************** Maoni ya wanaJF *******************






F


G. Naziri Karamagi na Dr. Msabaha nao wajiuzulu


H
Alionewa, issue hii ilipikwa kwa sababu za kisiasa.. Rais naye alitakiwa kujiuzuru kama ni hivyo
 
Augustoons said:
Hapo ndio haja ya kuwepo waziri asiye na wizara maaalum au naibu waziri mkuu inakuwepo. Ila ni washenzi tu hakuna haja ya kuweweseka nani aongoze shughuli za serikali bungeni Batilda Buriani si yupo? yeye si ndio mwakilishi wa waziri mkuu bunge?

Naam mi ndio maana hapa JF niliwahi kuwaambia kile kitabu cha UONGOZI WETU NA HATIMA YA TANZANIA alichoandika nyerere kina unabii mule,hakuna mtu anayekichambua lakini ipo siku,tusipoangalia mambo haya yalosemwa mule yatatimia.

Lowassa hana haja ya kusema hakupewa nafasi ya kujitetetea. Kamati haikuwa imemtuhumu mtu wala kuform chaji zozote,kamati ilialika watu kwenda mbele yake na kujieleza au kueleza lolote wanalolijua mbona hakwenda? Kisheria kujiuzulu kwa waziri mkuu hakutokani tu na kwamba yeye anahusika na hilo sakata bali ni ministerial responsibility, yeye kama kiranja wa baraza na mawaziri wake wameboronga bado alipaswa kujiuzulu hata kama asingehusika moja kwa moja.

Kama anadai hakupewa nafasi ya kujitetea ama kama anavyodai kuhojiwa? hakupaswa kuwasilisha barua ya kujiuzulu badala yake angewasilisha maelezo ya kujiteteta ili bunge lililomuidhinisha kuwa waziri mkuu lijadili utetezi wake na hatimaye litoe maamuzi,kwa nini kakimbilia kujiuzulu?

Afahamu kamati haikupendekeza aondoke ilimwambia atumie busara zake,sasa kama kujiuzulu na kulalamika ndio busara basi poa
 
20240221_212714.jpg
 
Back
Top Bottom