Kashfa ya Richmond: Lowassa, Karamagi na Dkt. Msabaha Wajiuzulu

Mpaka Kieleweke

JF-Expert Member
Feb 27, 2007
4,132
1,571


Ni kuwa mjadala wa Richmond ndio unaanza japo mbunge wa Kigoma Mjini ndugu Peter Serukamba alimtaka spika kumpa ufafanuzi kwanza kuwa ni kwanini Waziri mkuu hakupewa nafasi ya kujitetea kwenye kamati husika.

Waziri mkuu kaamua kujitoa kwenye meza na amekuwa mchangiaji wa kwanza kuchangia, nitawaambia kile ambacho yeye amechangia binafsi.

A Mchango wa Waziri Mkuu*

Ameanza kwa kumpongeza Mwakyembe na kusema amekuwa na mbwembwe nyingi sana .

Anasema hakuridhika na jinsi kazi hiyo ilivyofanywa na anamponda sana mwakyeme kwa yeye ni mwqanasheria na hakumfanyia Natural Justice, yeye binafsi kwani hawakumhoji hata siku moja.

Analalamika Waziri Mkuu kuwa hakupewa Natural Juctice kwani hakuitwa na anasema kuwa alikuwa tayari kwenda hata kwa miguu kwenye kamati husika za bunge.

Anasema kuwa ameonewa sana na amedhalilishwa sana na kamati na kuwa ametuhumiwa bila hata ya kuulizwa hata jambo moja.

Anasema kuwa yeye ameonewa na anasema kuwa kwenye taarifa yao hakuna hata taarifa moja iliyotoka kwenye ofisi ya waziri mkuu , na anasema kuwa ingekuwa heshima kama angepewa nafasi ya kujitetea.

Analaumu kuwa kama wanaweza kumponda Waziri Mkuu kiasi hicho je?mwananchi wa kawsaida anaweza kutendewa haki?

Waziri mkuu ametangaza kuwa amejiuzulu na amemwandikia barua Rais Kikwete.

Zitto anataka mwongozo wa spika juu ya Waziri Mkuu kujiuzulu na anasema kuwa kama Waziri Mkuu amejiuzulu basi na baraza zima lazima lijiuzulu kwani Rais aliteua baraza kwa kushauriana na Waziri Mkuu.

Spika anakataa kuwa baraza zima haliwezi kujiuzulu , mpaka apate barua ya Rais.

Ni kuwa bunge bado linajikanganya sana na hali inawatisha hata wabunge na kwa sasa spika anajiuliza anawezaje kuliendesha bunge kaomba kupewa ushauri na wabunge .

Kuna hali ngumu sana kwa spika na haswa baada ya Zitto kutaka baraza zima lijiuzulu ili kuwweza kumpa rais muda wa kutangaza baraza jipya la mawaziri .

Mbunge wa CCM masilingi anasema kuwa jambo hilo lipelekwe kwenye kamati ya wabuinge wa kamati ya CCM ili wakajadili sijui kama hapo kuna mwelekeo kwa sasa .

Masilingi anatak bunge liahirishwe ili wakajadili kwenye kamati ya CCM .

Zitto anatoa hoja kuwa bunge liahirishwe kwa muda kwanza ili kuweza kuijadili hoja hiyo hapo baadae ,kamnyima mdee halima nafasi ya kutoa taarifa .

Ni kuwa bunge limeahirishwa hadi saa kumi na moja jioni na wabunge wa CCM wameenda kujipanga sijui watakuja na ajenda ipi na rais bado hajajibu barua ya Lowassa ya kujiuzulu.

Naitafuta barua hapa nikiipata tuu naiweka wakuu kaeni mkao wa kula humu leo.

Hakuna waziri ambaye ameenda kumpa pole isipokuwa Batilda tu, hapa kuna ujumbe mzito sana na umejificha.

Nitaendelea kuwapa yanayojiri hapa

B. Hotuba Kamili ya Mheshimiwa Edward Lowassa




==================
C. Vyombo vya Habari vya Kimataifa

D. Rais wa JMT aridhia maombi ya Waziri Mkuu Kujiuzulu


E ****************** Maoni ya wanaJF *******************




F

G. Naziri Karamagi na Dr. Msabaha nao wajiuzulu

H
 
Last edited by a moderator:
Amesema sababu, hakuhojiwa na kamati teule. Katika report ya Dr Mwakyembe hakuna ushahidi hata mmoja kutoka ofisi za waziri mkuu.
 
Naona jamaa ameanza kwa jazba sana na kukandia report mwishoni kaishia kubwaga manyanga!!!
 
Bunge sasa limesimama, wanatafuta mwongozo nani aongoze shighuli za serikali Bungeni. Baada za mweshimiwa Lowasa Kujiuzulu.
 
Wakuu,
Naomba wenye ndikali, banana na vijoge watuletee hapa sokom kuu Bukoba.

Tunaanza maandalizi ya Rubisi ya kutosha kwa ajili ya sherehe ya kumng'oa karamagi na Lowassa.

Dokezo kwa JK: Tunaomba usimpe uwaziri Balozi Sued Kagasheki hata kama utakosa mtu toka Kagera anayefaa. Huyu ni fisadi wa Kimataifa WIPO wanamfahamu.
 
Mzee wa viwango ameshtuka na ameomba mwongozo wa wabunge jinsi za kuongoza Bunge. Kinachojadiliwa sasa je baada ya Lowasa kujiuzulu je mjadala uendelee au la?

Masilingi anashauri Bunge liahirishwe na waende kutafakari.
 
Hata akiponda ripoti ya tume,yeye apumzike tu kwa amani.Enough is enough.Haya tunakusubiri karamagi,msabaha rostam na wengine.
 
Wajumbe Bunge limehairishwa ghafra mpaka Saa 5pm. Spika ameomba kwenda kutafuta mwongozo wa Kisheria.
 
Waziri mkuu Edward Lowassa katangaza kujiuzulu.

Masilingi kamtetea hataki ajiuzulu.

Bunge limeahirishwa hadi saa 11 jioni.

Siasa imeanza kuingizwa kupindisha hali halisi.

AIBU AIBU AIBU......

UFISADI ...UFISADI ....UFISADI...
 
Bado Karamagi,Msabaha,na Wengineo.

Cha Msingi Ni Namna Atakavyoweza Kurudisha hizo hela.
 
Hata akiponda ripoti ya tume,yeye apumzike tu kwa amani.Enough is enough.Haya tunakusubiri karamagi,msabaha rostam na wengine.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…