Kashfa ndani ya Kashfa, Uozo ndani ya Uozo: Mwema, Chagonja, Manumba need to go! (Lowassa pia yumo!)

Chama,

Hata haujui unakataa nini na unakubali nini. Mwanakijiji amesema kuna udhaifu mkubwa kwenye mfumo wa jeshi la polisi, wewe unasema usaili unachukua hadi siku tatu. Hivi kujua kama huyu mtu anatakiwa kuwa pale chuoni ni zaidi ya siku moja basi huo ni uozo wa hali ya juu. Kuna siku wataingia magaidi pale wakilipue chuo nadhani ndiyo utajua polisi si wakulaumiwa!

Mkuu umeelewa nilichokisema? Kama kuna udhaifu toa mapendekezo ya nini kifanyike; hapa hoja yangu iliegemea zaidi kwa hao makuruta waliotapeliwa; sikuwahi kusema au kudai utaratibu unaotumika CCP ni bora; kuzuia ugaidi bado intelijensia yetu ni kiwango cha chini sana na kuzuia ugaidi ni kazi kubwa sana kinachofanyika ni kupunguza athari za ugaidi; mkuu wa chuo mwenyewe anaweza kujigeuza gaidi je utamzuia vipi?

Chama
Gongo la mboto DSM
 
Mwanakijiji
Utalilaumu vipi jeshi la polisi kwa watu waliotaka kutapeliwa wenyewe? Taratibu za kujiunga na jeshi zipo wazi; zinaanzia wilayani; mkoani hapo ndipo unapofanyika uteuzi wanaokwenda CCP; sasa ikiwa wahusika wenyewe kwanza waliombwa kutoa rushwa hapo peke yake ni kosa; jeshi la polisi halitozi ada ya kuchukua makuruta; kwa maana hiyo wahusika walijiingiza kwenye uvunjaji wa sheria; kujiunga na jeshi kama nilivyosema awali kuna taratibu za mchujo ambao huanzia wilayani hadi mkoani; wahusika walipaswa kushtuka harufu ya utapeli ilikuwepo tangu mapema; Na unakilaumu vipi chuo? wanafunzi waliopokelewa watakuwa ni zaidi ya 200 inawezekana hata 1000 walikuwepo; usaili wa wanafunzi wapya haufanyiki kwa siku moja na hilo liligunduliwa sasa tatizo ni nini? Kama wangemaliza mafunzo hapo hoja yako ingekuwa na mshiko; bado najiuliza jinsi gani mh. Lowassa ameingia vipi pamoja ya kwamba yupo kwenye kamati ya bunge; hapa sioni unamuunganisha vipi au yeye ndiye alihusika na uandikishwaji wa hao makuruta wapya? Kama ni suala la mgeni unayemuongela yeye ndiye aliyetoa mualiko kama mwenyekiti wa kamati? Nadhani ulichopaswa nikushauri mh.Lowassa kama mwenyekiti wa tume alichunguze hilo na si kumpaka matope; Mwanakijiji usiandike vitu kama mwanaharakati umebobea kwenye hii fani haya unanaharakati wenyewe waachie kina Mtoi wao ndio wanaoandika vitu bila kujiuliza maswali ya msingi. Mwanakijiji mtu anapotafuta kitu kwa kutumia misingi ya kuvunja sheria usilaumu vyombo husika akitapeliwa hilo ni funzo; wao walijua tangu awali wanatumia mlango wa uani kuingilia sasa hapakuwa na kukosa kuwatoa kwa kutumia mlango wa mbele; na wala hupaswi kuwasikitikia

Chama
Gongo la mboto DSM
Mwanakijiji majibu ya maswali yako yanaweza kupatikana katika huu mchango wa Mtanzania halisi, chama.. chama ni mmoja katika Watanzania ambao wamefanikiwa kupata exposure ndani na nje ya nchi, anayo komputa na ni memba maarufu wa jukwaa hili! Kama chama anao ujasiri wa kuongea haya, hebu fikiria masikini mkereketwa ambaye hata Dar es Salaam anaisikia tu kama anavyoisikia New York! Na hapa bado havijaingia kina zomba (duh!), Rejao (mmhh!), genius Brain (aarrghh!), Ritz (masikini!), Njiwa (oh!) na vikereketwa (poor Tanzania!) vingine dazani kidogo.

Orodha ya viongozi wapya wa CCM ni dalili tosha ya taifa linakoelekea...nani alijua CCM itarudi kwenye dampo kuokoteza vilivyochoka na vilivyochokwa au vilivyochuja na vilivyochujwa...aah, recycling technology ambayo kama kawaida yetu hatuna utaalamu nao kama taifa. Jeshi la polisi kwa sasa ni kioo cha utawala chini ya CCM, utawala usio na dira, utawala usiojua unatoka wapi na unaenda wapi. Tofauti na popote duniani kuliko na ustaarabu, jeshi letu la polisi limeimarika na linaendelea kuimarika siku hadi siku, kwa shughuli zipi? Kupambana na raia wema huku wakiwalinda wezi, wauaji na wapuuzi.

Kwamba wapo Watanzania wanaowatetea hawa majambazi ni jambo ambalo raia mwema wa nchi hii hawezi kulielewa achilia mbalo kuliunga mkono. Lakini wapo...vijana kwa wazee, wake kwa waume, masikini na tajiri na watu wa dini zote, kwao malalamiko yetu ni kelele tu kama za mpangaji...Kikwete hakosi usingizi, sana sana kwake kelele zetu ni kama dawa tu za kumwongezea usingizi. Nape na Kinana, hivi sasa wanazunguka nchini wakifuatana na mawaziri si chini ya watano, kisa? Kufufua na kuimarisha chama, kuimarisha CCM! Mwanakijiji, hatuna jeshi la polisi, tunalo genge la vibaka na wauaji.
 
Ndugu watanzania tuache woga tuingie mitaani tulianzishe kama vipi.

Hakuna ubaya wa hoja yako ila ukilianzisha limalize usije ukatafuta ukimbizi Somalia! Ndugu zetu visiwani walilianzisha ila matokeo yake unayajua walikimbilia Somalia kutafuta ukimbizi. Yapime mwenyewe!!

Chama
Gongo la mboto DSM
 
wana JF kuna mengi ndani ya majeshi yetu usishangae kuona wamo Wahabeshi, al shabaab, na hata M23 walioajiliwa kama mnyarwada aliyefikia rank ya A/inspect akiwa ktk nchi hii na alipochoka akarudi kwao Rwanda na ni boss ktk polisi yao.

Katika topic hii waliodhulumika na mdhulumaji WOTE wanahitajika kujibu kortini kupita kwa Hosea.

Kaka fafanua hiyo ya mnyarwanda,
Anaitwa nani?
 
Wa Kulaumiwa ni Mimi na Wewe na Wananchi na WaTanzania. Hakuna Mchawi hapo.
Umoja ni Nguvu Utengano ni Udhaifu. Inasikitisha Kusikia na Inatia Uchungu sana.


Nadhani legacy ya serikali hii ya awamu ya nne ni kashfa, ufisi,ufisadi,uroho, roho mbaya, uzembe, wizi, ujambazi--- haina jema hata moja na kama lipo limetokea kwa bahati mbaya. Wamekula pesa yetu, raslimali zetu na mwisho watatula sisi. Je nani wa kulaumiwa iwapo watanzania tumepata ubingwa wa kulalamika huku tukiambulia patupu kwenye mapambano? Ni kama taifa zima limechakachuliwa hasa vichwani kuanzia chini hadi juu.
 
chama Goodness me! Hivi nimekuelewa ama nimelewa..So what do you want to say? Kwamba raia wa tanzania usalama wake hauihusu serikali iliyopo hata kama yeye mwenyewe kwa ujinga wake atajipeleka kwenye matatizo? Kwanini wanaotaka kujinyonga wanashitakiwa na jamhuri basi iwapo mauti haitawafika, pale wanapojaribu na kushindwa? Si wangeachwa tu kwakua walitaka kuondoa uhai wao binafsi hivyo is up to them?

Ulinzi wa raia na mali zao ni pamoja na kuweka mazingira ambapo raia hata pata incentive ya kutoa rushwa na wale watendaji hawataweza kupata mazingira rahisi ya kupokea rushwa kwa mambo waliyoajiriwa kuyafanya katika jamii...Nadhani ndiyo maana ya sheria kuwa msumeno unaokata kuwili....Hata kama mnapenda kutetea angalieni mambo mnayotetea maana ni hatari kwa usalama wa kila mtu serikali inaposhindwa kutimiza jukumu lake la kuwalinda raia ambalo ni haki ya msingi. Sheria inaposhindwa kulinda raia kwaajili ya ufisadi lawama ni ya serikali na vyombo vinavyoisimamia hiyo serikali na huu ndiyo msingi wa lawama za Mwanakijiji kwa jeshi lenyewe kama moja ya vyombo vya ulinzi na mwenyekiti wa kamati husika ambayo ilipasa kung'amua mapema mambo kama haya hasa kwakua lawama za jinsi hii si za mara ya kwanza kama MMM alivyozi document hapo.
 
Last edited by a moderator:
ifike mahali huu uoga na utulivu feki kidogo tuufikirie mara mbili je unastahili kuwepo ama la kama unastahili je nn kifanyike kubadili hali ya sura ya nchi hii maana inaudhi sana na kusononesha as ingekuwa ni maandamano wangesema kunataarifa ya kiintelejensia imefika kwaiyo hayaruhusiwi ingekuwa ni madktari wanadai haki zao ......... ili je waliotapeliwa wanawasaidiaje?
 
Ame Tatizo la nyie wanaharakati mnakurupuka kama mliyetoka usingizini! Hapa kwa jinsi ulivyojibu utakuwa umelewa, ulinzi na usalama wa raia unaanzia kwa raia wenyewe; serikali kwa kutumia vyombo vya dola kama polisi ni katika kuhahakisha usalama unadumishwa ili vyombo vya dola vifanye kazi yake kwa ufanisi ni wajibu wa raia kutoa ushirikiano wa kutosha; tukirudi kwa Mwanakijiji alipaswa kufanya uchunguzi wa kina kabla hatupa lawama kwa polisi; hakuna usalama wa raia uliotishiwa na nawapa pongezi viongozi wa CCP kwa kuwagundua wale wote waliotaka kujipenyeza ndani ya jeshi la polisi kwa njia zisizo sahihi. Mkuu rushwa ni kati ya mtoaji na mpokeaji unachotakiwa ni kufuata njia sahihi hawa jamaa walitapeliwa ni mfano halisi kama wangefuata njia inawezekana wengine wangepata wangine wale ambao wangekosa wasingepata hasara ya kutapeliwa

Chama

Sent from my BlackBerry 9900 using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
mie nahisi labda wamerushana mshiko ndio maana imegundulika .....siku hizi police waliopo huwezi amini kama amesomea na kupitia vigezo jamani angalieni police walivyo maumbo yao kama watoto wa darasa la saba wadogo kweli hata kukamata mtu kwa nguvu hawezi
 
Nadhani inawezekana kuwa viongozi wetu wanajua kuwa akili za watanzania zinahamia upande mmoja kila wakati.
Kwa mfano sasa hivi tumeacha kashfa za madini tunakodolea macho gesi, kwa hiyo kwenye madini wakiendelea kuiba hatuoni tena.
 
Tatizo la nyie wanaharakati mnakurupuka kama mliyetoka usingizini! Hapa kwa jinsi ulivyojibu utakuwa umelewa, ulinzi na usalama wa raia unaanzia kwa raia wenyewe; serikali kwa kutumia vyombo vya dola kama polisi ni katika kuhahakisha usalama unadumishwa ili vyombo vya dola vifanye kazi yake kwa ufanisi ni wajibu wa raia kutoa ushirikiano wa kutosha; tukirudi kwa Mwanakijiji alipaswa kufanya uchunguzi wa kina kabla hatupa lawama kwa polisi; hakuna usalama wa raia uliotishiwa na nawapa pongezi viongozi wa CCP kwa kuwagundua wale wote waliotaka kujipenyeza ndani ya jeshi la polisi kwa njia zisizo sahihi. Mkuu rushwa ni kati ya mtoaji na mpokeaji unachotakiwa ni kufuata njia sahihi hawa jamaa walitapeliwa ni mfano halisi kama wangefuata njia inawezekana wengine wangepata wangine wale ambao wangekosa wasingepata hasara ya kutapeliwa

Chama

Sent from my BlackBerry 9900 using JamiiForums

mie binafsi sijakuelewa yaani watu watoke wanakotoka mpaka ...kuna mkuu wa chuo mkuu wa police wa mkoa na makamanda wengine kibao watu waingie kwenye kambi kuu kama ile chuoni ccp .........wamepokelewa wamelala,wamenyolewa wameoga wamekunya wamekula chakula wamefanya kila kinachotakiwa halafu wewe unasema eti hawajafuata njia sahihi nafikiri ubongo wako umeshachoka kufikiri kama secretariet mpya ya magamba

 
mzee MMK nimeuenda sana mtazamo wako na ni waaiz kwamba webgi waliwaza kwa stahili hii ila nakupongeza sana kwamba wewe umeweza kuliandika hapa wengine tumekauka nayao moyoni.

ninalo swali moja kwako nalo ni "" hivi kwanini Lowassa umemuweka hapo juu??"" nauliza kwasabbu huku ndani sioni mahali alipohusika na swala hili la hawa vijana anyways labda ninaakili fupi, lkn pia ni kwanini Huyu Lowassa aonekane kutupa shida sana sana na linapookea kosa lolote basi awe linked nalo hali tukitambua kwamba yeye si mtumish wa umma tena. naomba unijibu tu hapo nipate mwanga tafadhali.
 
Viongozi wetu wanataka nini kwa kufumbia macho uozo kama huu? Au wanategemea Mungu ashuke mahali hapa ndipo wajue kuwa kuna umuhimu wa kutatua matatizo lukuki yanayowakumba watanzania? These people are totally rotten.
 
Duh! huyo PolisCCM mwenye sanduku kama "Safe" ya kuwekea pesa akikukamata atakuachia kweli!!??
 
Mwanakijiji
Utalilaumu vipi jeshi la polisi kwa watu waliotaka kutapeliwa wenyewe?

Chama
Gongo la mboto DSM

Kwa maneno machache, unataka kusema kuwa jeshi la Polisi lipo safi kwa hili kwa sababu "walitaka" kutapeliwa wenyewe?
 
Kinachonishangaza ni kusoma baadhi yetu wakiamini kuwa ni halali kabisa kwa eneo kama la Jeshi la Polisi kupokea watu wasiojulikana na kukaa nao siku tatu.
Yaani ndani ya kambi ya jeshi la Polisi siku tatu bado kuna mtu anatetea ujinga wa namna hiyo! Dah! inasikitisha.

Yaani hata kibaka anaweza kuingia na kulipua chuo cha kijeshi bila kipingamizi, halafu wapo watu na akili zao wanadhani hilo ni sahihi kabisa!
 
Halafu kwa inteligensia hii bado kuna Watanzania wanasema tuko tayari kupigana vita na Malawi!! Kwa inteligensia hii kama tukipigana vita na Malawi, Rais Joyce Banda anaweza kutoka Blantyle hadi Magogoni (Ikulu) akamkojolea Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama wakati yeye akiwa amelala fofofo usingizi wa pono na bado akarudi Blantyle bila inteligensia yetu kujua.

CCM mmeifikisha pabaya nchi yetu! Ni punguani tu atatetea hii kashfa!
 
mwana wa mtemi Kweli kuna uozo mwingi! kama hata kambi ya Oysterbay anapewa muwekezaji! yote haya yanafanyika chini ya uongozi wa huyu Mangi! ye anawaza hela tu!
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom