Karibuni wadada/wamama

Mi nikimpata my love wangu, nitamfanyia kilakitu bila kuambiwa wala kulalamika kwani itakua moja ya jukumu langu la kila siku. Eeh mwenyezi mungu nisaidie.
 
Akipendeza anamvutia kila mtu, halafu anavutika kwa kila anayemvutia. Ha ha ha!!!
 
Maisha yanavyochanganya haya mambo itafika mahali hayatatekelezeka yote. Mama naye anafanya kazi, anafanya majukumu haya na ya nyumbani na ya kazini pengine na mtoto mchanga.

Hebu vuta picha, saa 11 asubuhi anakupa halafu anakuacha hapo kitandani unajisikilizia utamu. Anahakikisha Hgirl ameamka, mtoto amejiandaa kuwahi shule, chai iko mezani, usafi umefanyika kidogo. Ajiandae kwenda kazini, akukumbushe uamke usichelewe kazini, anyonyeshe mtoto, apange utaratibu wa kutwa chakula na mtoto.

Akifika kazini kuna document za kusoma, mikutano, email za kujibu, ripoti, n.k. Usisahau foleni asubuhi na jioni. Akiwa kazini anapigiwa simu nyama yote imeharibika kwa sababu umeme. Yaani mambo mengiiii.

Haya sasa hebu nieleze hayo mambo ya kufua chupi na soksi sijui itakuwaje. Kama anafanya mara moja moja kwa mapenzi sawa lakini.
 
Maisha yanavyochanganya haya mambo itafika mahali hayatatekelezeka yote. Mama naye anafanya kazi, anafanya majukumu haya na ya nyumbani na ya kazini pengine na mtoto mchanga.

Hebu vuta picha, saa 11 asubuhi anakupa halafu anakuacha hapo kitandani unajisikilizia utamu. Anahakikisha Hgirl ameamka, mtoto amejiandaa kuwahi shule, chai iko mezani, usafi umefanyika kidogo. Ajiandae kwenda kazini, akukumbushe uamke usichelewe kazini, anyonyeshe mtoto, apange utaratibu wa kutwa chakula na mtoto.

Akifika kazini kuna document za kusoma, mikutano, email za kujibu, ripoti, n.k. Usisahau foleni asubuhi na jioni. Akiwa kazini anapigiwa simu nyama yote imeharibika kwa sababu umeme. Yaani mambo mengiiii.

Haya sasa hebu nieleze hayo mambo ya kufua chupi na soksi sijui itakuwaje. Kama anafanya mara moja moja kwa mapenzi sawa lakini.

Mmmmmh acha tu kaka angu, maisha mengine siyo yakutamani, labda niseme huo ni utumishi na ni wito. Maanake kuna kujitoa sadaka hapo kwa kweli.
 
Enzi za utumwa zimeisha bwana. watu ni bize bize. Ninachoona mimi kama mama hana kazi za kutoka nje ya house basi anaweza kufanya hizo shughuli kufua, kumpasia, kubrush viatu etc. Lakini maisha yenyewe watu mnarudi full mchoko nianze kumfulia, kumpasia, brush viatu aaa wapi. Kila mtu afue nguo zake na kupasi. Ama zamu za kufua. Labda ninafua zangu na zake wiki hii na yeye wiki ijayo afue yeye. Ama laa nikifua yeye anapasi. Lakini kudekezana karne hii wapi na wapi? huu utumwa no more. Mimi napenda mtu wangu awe smart lakini pia kuwa mtumwa no! wote ni binadamu tunachoka ati1 sio kwamba basi mwanamke ndo afanye tu.
 
Samahani, nahisi huyu mwanamke unayemuongelea hapa ni mama wa nyumbani, hivi na hizi foleni za bongo naamka asubuhi naanza kumuandaa mwenzangu badala ya kujiandaa mimi au mi kazi yangu ni ya night shift kila siku. Na hiyo ya kumuandalia maji sasa kuna nyumba nyingine wanatumia shower, wengine nguo wanapeleka dry cleaner sasa inakuwaje hapo ndugu mshauri, tena mimi watu kama hawa naona ndio wanauwezekano mkubwa wa kuboresha penzi maana wakati wote mke hajachoka na vishughuli vya hapa na pale, nawasilisha!
 
Mmmmmh acha tu kaka angu, maisha mengine siyo yakutamani, labda niseme huo ni utumishi na ni wito. Maanake kuna kujitoa sadaka hapo kwa kweli.

Kwa mtindo huu lazima mwanamke azeeke mapema.
 
Kwa mtindo huu lazima mwanamke azeeke mapema.

Umeona ee!! Halafu akizeeka na kuchakaa baba anavuta kabiti huko nje. Huku mama bado anakomaa na kumtunzia bibi mdogo. Daaa Mungu saidia mama zetu na utupe watu wanaotupenda tu. Daaa yani hata vitu vidogo vidogo lazima tufanye jamani. Kwa nini ukienda kuoga usifue huko huko hizo naniliu? Aaah mi sijui bwana lakini, Haya maisha ya hivo hayatamanishi hata kidogo.
 
Nakubaliana nawe mtoa mada, ila na hao wanaume nao wanatakiwa watuoneshe na siye upendo kulisha family na kuacha matumizi haitoshi. Watu wanaopendana huwa wanashirikiana kwa kila kitu na si kunyenyekeana, ushirikiano unatoka ndani ya moyo. Kwani hata mwanamke wakati mwingine anakuwa na majukumu mengi,
 
Hii nimeikuta sehemu fulani, nikaona ni vyema niikandamize huku JF huenda ikaleta changamoto ama kwa kujikumbusha ama kwa kutilia mkazo na kadhalika hasa hiki kipindi tuiendeapo ileeee siku ya wapendanao. Haya embu soma hii:

LEO nataka tukumbushane kitu kimoja nacho ni jinsi ya kumfanya mwenzi
wako aonekane maridadi wakati wote. Hapa nazungumzia wale walio katika
mahusiano ya kudumu ambao wanaishi pamoja.
"Nikiamka asubuhi jambo la kwanza ni kumuandalia mume wangu maji ya
kuoga, nahakikisha nguo zake zimepigwa pasi, viatu vimeng'arishwa,
soksi ziko safi, na akivaa lazima nimfunge tai, na nguo za kazini mimi
ndiye nachagua siku hiyo avae nguo gani" anasema Mama mmoja mkazi wa
Kimara Jijini Dar es Salaam.
Sikiliza na hii " Mimi mume wangu huwa anaandaa nguo zake mwenyewe
anafua, apige pasi au asipige shauri yake, aoge asioge atajijua, huo
muda sina kabisa siku hizi" anasema mwanamke mmoja Mkazi wa Buguruni
Jijini Dar es Salaam.
Siku zote tumekuwa tukisisitiza urembo kwa wanawake na utanashati kwa wanaume.
Mmoja ya jukumu la mwanamke ni kuhakikisha kuwa, mwanaume wake anakuwa
maridadi na mwenye kuvutia. Jaribu kuangalia ni nguo za aina gani mume
akivaa zinampendeza na hapo unaweza kumchagulia shati na suruali
ambazo rangi zake zinaendana na hata akivaa zitamfanya apendeze.
Pia suala zima la kufua na kupiga pasi vizuri ni moja ya njia ya
kuonyesha kuwa unamjali na unamjengea namna ya kujiamini
zaidi.Utunzaji wa soksi ikiwemo ufuaji wa nguo za ndani ni jambo
linalosisitizwa sana kwani wanaume wengi wanaonekana kutojali sana
vitu hivyo ama kutokana na muda au kwa kukosa ushirikiano wa wenzi wao
katika kutunza na kufanyia usafi aina hizo za nguo.
Jamani mwanaume akiwa maridadi au mtanashati huwa anamvutia kila mtu
na zaidi sifa zinakwenda kwa mkewe ambaye anaaminika kuwa ni chanzo
cha mwanaume kuwa msafi.
Jenga mazingira ya kujali usafi wa nguo za mwenzi wako ili kuhakikisha
kuwa kila kitu kinakwenda sawa.
Pia kuna wanawake wengi ambao ni wajuzi wa kufunga tai, kama hilo bado
hulifahamu tafuta mtu ambaye atakufundisha namna bora ya kufunga tai
ili uweze kumpendezesha mume wako.
Kama unapita dukani au sehemu zinakouzwa nguo si vibaya kama unaona
kuna nguo inaweza kumfaa mwenzi wako mna ukahakikisha kuwa akivaa
anapendeza usisite kununua kwani itakuwa ni zawadi nzuri sana kwake.
Jaribu kuwa na tabia ya kumvika mwenzi wako, si kuacha kila kitu
afanye yeye kuanzia kufua, kupiga pasi na hata kung'arisha viatu.
Ni vizuri kama utaamua kuhakikisha kuwa, unamuaandaa mume wako kabla
ya kwenda kazini kisha na wewe kuendelea na shughuli zako.Hilo
litaongeza upendo na amani kwenye nyumba.
Wanawake wengi wamejisahau sana na kuacha wanaume wafanye kila kitu
wenyewe jambo ambalo husababisha wanaume wengine watoke nyumbani bila
kupiga pasi au kusahau kuchana nywele.
Jirekebishe kama una tabia za kutojali usafi wa mwenza wako,
utanashati ni muhimu kwa wanaume pia usiishie kwa wanawake kujipenda
na kujiremba kila wakati huku wakisahau waume zao[

Hapa kazi ipo, mie sidhani kama practically inawezekana. Ukifanya mbona utakuwa mtu wa busy kila saa. Haf kuna vitu vingine sasa vinaendwa kupitwa na wakati, labda kwa wamama wa nyumbani ambao hawana shughuli yoyote. Yaani shughuli iwe tu ya kutunza mume.
 
kama mtoto wa shule tena shule ya awali. kweli wanawake tuna kazi za ajabu?
 
7yrs kwenye ndoa siku zote namfulia mpaka underwear,nanyoosha,na brush viatu na kupiga kiwi na vest na underwear namnunulia. MALIPO? Akirudi anavua nguo na kuziweka kokote,nikiumwa atarundika nguo mpaka nipone,nilipojifungua alikuwa haishi kuuliza nitakuwa fit lini maana amechoka kujifulia na kubwa kuliko niligundua ana CHEAT na akakiri. Hawana jema hao!
 
kama mtoto wa shule tena shule ya awali. kweli wanawake tuna kazi za ajabu?

Eti mwanaume ahudumiwe kama mtoto si aende daycare!!..kweli ni kazi ya ajabu na kijinga..haitafsiri mana ya upendo ambao ni 'give&take'
sasa wengi wao ubabe mbele unafikiri huo ni upendo?!!..
 
7yrs kwenye ndoa siku zote namfulia mpaka underwear,nanyoosha,na brush viatu na kupiga kiwi na vest na underwear namnunulia. MALIPO? Akirudi anavua nguo na kuziweka kokote,nikiumwa atarundika nguo mpaka nipone,nilipojifungua alikuwa haishi kuuliza nitakuwa fit lini maana amechoka kujifulia na kubwa kuliko niligundua ana CHEAT na akakiri. Hawana jema hao!

Pole mwaya..
 
Maisha yanavyochanganya haya mambo itafika mahali hayatatekelezeka yote. Mama naye anafanya kazi, anafanya majukumu haya na ya nyumbani na ya kazini pengine na mtoto mchanga.

Hebu vuta picha, saa 11 asubuhi anakupa halafu anakuacha hapo kitandani unajisikilizia utamu. Anahakikisha Hgirl ameamka, mtoto amejiandaa kuwahi shule, chai iko mezani, usafi umefanyika kidogo. Ajiandae kwenda kazini, akukumbushe uamke usichelewe kazini, anyonyeshe mtoto, apange utaratibu wa kutwa chakula na mtoto.
Akifika kazini kuna document za kusoma, mikutano, email za kujibu, ripoti, n.k. Usisahau foleni asubuhi na jioni. Akiwa kazini anapigiwa simu nyama yote imeharibika kwa sababu umeme. Yaani mambo mengiiii.
Haya sasa hebu nieleze hayo mambo ya kufua chupi na soksi sijui itakuwaje. Kama anafanya mara moja moja kwa mapenzi sawa lakini.
Du mtoa mada umenifurahisha na hii kitchen party au sijui ni Valentine maana mpaka Bw Muosni amerudi Bongo maana alishakamatwa na mkisii wa Kenya tukamwambia hawana uvumilivu waKenya km waBongo hapa ame-kiri mwenyewe wanawake wetu chapa kz na wana upendo
Mm nafuliwa @ k2 napakuliwa nalishwa na nadekezwa mpaka nakimbia nyumba.
Yeye bado ataenda kazini na atakachopata atakileta nyumbani kwa wanangu na hataacha kurudi km wanawake wa jirani wenye tamaa za kufanya kz za biashara na nje ya nchi yao (akipata Bw sawa, utajifulia mwenyewe)
 
Back
Top Bottom