Karibuni Chama kipya cha Siasa - Arusha Declaration Alliance

Karibuni Chama kipya cha Siasa - Arusha Declaration Alliance

Status
Not open for further replies.
nyie mnataka kurudisha umasikini tu na chama kinachofata azimio la arusha. foleni hata kwa kipande cha sabuni au kiberiti- asante kwa azimio maisha yalikua magumu.
 
Si mbaya kuwa na vyama vipya. Ila ushauri wangu kwenye ilo jina la chama kwan badae linaweza likawaletea sitofahamu kwan watu wanaweza kujenga hoja ni chama cha watu kutoka arusha, kwan si wote wanaojua azimio la arusha. Mbali na hayo nawatakia mafanikio mema na mungu awatangulie katika kulifanikisha jambo hili
 
Kwa nini msijiunge na CCM kupunguza gharama maana tayari wao wameshaanza kuturudisha azimio la arusha...tayari sukari inanunuliwa kwa foleni, watu wanalazimishwa kufagia kinguvu, tumetoka kurusha matangazo ya bunge laivu kwenda recorded ili watu "wakafanye kazi",
 
Mtoa mada ni mtu wa vibwana wanaojiuza..kuna uzi wake hapa JF unahusu malaya wa sinza..
 
hiko chama cha siasa au cha ujasiliamali wenzenu wakizindua chama wanaandaa mikutano public place kama jangwani hapo hamnipati
 
Chama cha kurudisha Azimio la Arusha litetewe kwa nguvu zote.
 
UPDATE: tutaonekana live ITV, TBC1,clouds TV,

Kweli sihasa sijui siasa sasa imekuwa biashara,sasa hiyo hela kulipia Itv,tbc na clouds muonekane mubashara si bora mngeitumia kuchimba visima vijijini kwenu au kuchangia huduma ocean road hospital,frankly speaking watanzania kwa sasa hatuitaji utitiri wa vyama vingi visivyokuwa na tija tuna hitaji mfumo wa vyama vingi vichache,strong na vyenye tija,mfano mzuri ulionekana kwa UKAWA ulikuwa mwanzo mzuri na pengine 2020 wanaweza kuja na something more organized.Mi nashauri tu mtafute shughuli nyingine ya kufanya,ni hayo tu.
 
Malengo ni kushinda viti angalau 80% uchaguzi wa serikali za mitaa 2019 na uchaguzi mkuu 2020. Karibuni sana.
 
karibuni watanzania tulifufue azimio la arusha.
 
Tunatafuta wanachama wa kukidhamini chama tunachotaka kukisajili hivi karibuni jina la chama (tunapendekeza kiitwe - Arusha Declaration Alliance kinachofuata misingi ya Azimio la Arusha. Tafadhali tukutane;

MUDA: 26 Novemba, 2016, Jumamosi, kuanzia saa 8 mchana.

UKUMBI: RAMADA ENCORE HOTEL, City Centre, Opposite Exim Tower (Posta Mpya) - Dar es Salaam.

MGENI WA HESHIMA: JULIUS MALEMA (MB) kutoka Afrika ya Kusini
MAWASILIANO: +255 654 828025 (Ms. Warda - Kaimu Katibu Mwenezi & Mr. Frank - 0715734747 Kaimu Mweka Hazina)

NB: T-shirt, Kofia, Khanga, Chakula, Vinywaji na Nauli (Tshs. 380,000/=) vitatolewa kwa watakaohudhuria tu.
LIDUMU AZIMIO LA ARUSHA

Huu ni uharibifu wa kisiasa ambao hauna tija kwa maendeleo ya Watanzania hata chembe. Huwezi kuanzisha chama kwa dhana ya Azimio la Arusha ambalo hata hivyo linahitaji marekebisho mengi ili kuendana na hali halisi ya uchumi wa dunia na mahusiano ya kimataifa kwa sasa.

Sioni jema lolote lenye uhalisia sahihi litapatiana kwa kukopi na kubandika Azimio la Arusha kama lilivyoandikwa 1967 chini ya mfumo wa chama kimoja cha siasa na mtangamano dhaifu wa muingiliano wa kimataifa. Ama ni vigumu kwa yeyote kusema ananguvu za kupingana na mabadiliko ya dunia yanayotokea kwa kasi katika nyanja zote.

Wachambuzi wa siasa wataniunga mkono kwamba Azimio la Arusha kama lilivyo haliwezi kuhimili mazingira yalipo sasa duniani. Linahitaji maboresho. Na kama litaboreshwa, siyo azimio la Arusha tena. Kitakuwa kitu kingine.

Pili mambo mengi yaliyomo katika Azimio la Arusha ni mazuri tu na yanafaa lakini hayawezi kujitosheleza. Hivyo ni mchakato mkubwa sana unahitajika kubumba kitu kinachoweza kuleta tija katika misingi ya Azimio la Arusha.

Hata hivyo, kama ndivyo, kuna vyama vingi vya siasa Tanzania ambavyo vinaonyesha mwanga wa kusimamia maslahi ya taifa ingawa vinahujumiwa. Kwa maana ya kwamba, maono yao yanatumiwa kuwahadaa Wtanzania kisha yanachakachuliwa na hatimaye kutekelezwa kwa namna isiyo sahihi na hivyo kupoteza mwelekeo na maana nzima ya dhana hizo.

Kama kweli kila Warda, Frank na wenzako mnalengo jema, jiungeni na vyama vya siasa kimojawapo kilichopo chenye nia ya dhati, kisha mkae mboreshe kwa ku incorporate agenda zilizomo katik aAzimio la Arusha ili kuimarisha nguvu ya upinzani ingawa Tanzanaiupinzani una nguvu kuliko chama wengine.

Hiyo itaonyehsa uzalendo na uwezo wa kushirikiana na watu wengine katika kusimamia na kulinda maslahi ya Watanzania. Kuanzisha chama kipya ni ishara ya ubinafsi na udhaifu mkubwa wa ki uongozi lakini ipia wenye lengo la kuimarisha migawanyiko katika kura na inaweza kutafisiriwa kama uwakala wa hujuma kwa upinzani.

Vyama vilivyopo vinatosha, ila kama kuna wazo jipya itafutwe namna ya kuviboresha badala ya kila mwenye wazo anaanzisha chama. Viongozi wa vyama vya upinzania, fungueni milango ya kupokea maoni mapya ya kuboresha vyama venu kila inapobidi kama inaonekana ni sahihi.
 
karibuni watanzania tulifufue azimio la arusha.
Moja kati ya nguzo kuu za Azimio la Arusha ilikuwa ni kuweka njia kuu za uzalishaji mali na utoaji huduma chini ya umiliki wa dola. Utekelezaji wa hii sera ulihusisha utaifishaji wa viwanda, mashamba, biashara mbalimbali, majumba na mabenki. Huu utaifishaji ulisababisha majanga makubwa ya kiuchumi kwa sababu serikali ilishindwa kuendesha kwa ufanisi taasisi zilizotaifishwa na kufanya wananchi kurudia maisha ya zama za ujima kutokana na kukosekana kwa bidhaa muhimu nchini. Mwaka 1984 serikali ilinyoosha mikono na kuruhusu watu binafsi kuagiza bidhaa kutoka nje (Trade Liberalisation Policy). Labda nikuulize, mna mawazo gani mapya namna ya kua-approach Azimio la Arusha katika mazingira ya sasa?
 
Status
Not open for further replies.

Similar Discussions

Back
Top Bottom