Na Habel Chidawali,Dodoma ( MWANANCHI )
NAIBU Waziri wa Fedha na Uchumi, Omari Yusufu Mzee amewajia juu watumishi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na kudai kuwa, baadhi yao ni wezi wakubwa, jambo linalolifanya taifa likose usingizi kwa ajili yao.
Mzee alisema hayo jana katika ofisi za TRA, wakati wa ziara yake ya kutembelea taasisi mbalimbali zilizo chini ya Wizara ya fedha mjini hapa.
Tofauti na alivyozoeleka Naibu waziri huyo kwa upole, jana alikuwa mkali mithili ya mbogo aliyejeruhiwa na kusisitiza kwamba dawa ya wazembe wa taasisi hiyo nyeti imekwishachemka, kinachosubiriwa kwa sasa ni kuipua na kuanza kutoa dozi.
Ndugu zangu michezo yenu hii michafu, mtatuua kabisa, acheni ,kama
tunatoa mishahara mikubwa kuwapeni mnadhani kuwa tunawapeni kwa ajili ya kuangalia sura zenu, sivyo bali ni kutaka mfanye kazi kwa uaminifu na kufuata maadili, lakini sasa huu ni wizi mtupu mnaoufanya watu wa TRA," alisema na kuhoji "kwa nini msibadilike,.
Alisema kuwa umefika wakati kila mfanyakazi katika taasisi hiyo atapimwa uwezo wake mwenyewe na atakayebainika kuwa anashirikiana na wafanya biashara kuiibia serikali atatolewa kafara na kuwa mfano kwa wenzake.
Aliwataka watumishi hao mkoani humu kukaa chonjo, na kuahidi kufika kuwakagua wafanyakazi hao sikuya Julai Mosi na kuwapatia mikakati mipya.
Naibu waziri huyo alisema hakubaliani kabisa na watu wanaofanya kazi kwa mazoea na akawataka kubuni mbinu mpya za kazi ikiwa ni pamoja na kutoa elimu ya walipa kodi kwa kila mtanzania mahali popote hata maeneo ya barabarani na vijiweni.
Jambo lingine alilosisitiza Naibu Waziri huyo ni pamoja na watumishi hao kujenga mahusiano mazuri yasiyo ya kinafiki na walipa kodi ili waweze kulipa kodi kwa
hiari yao wenyewe bila ya kusukumwa au kufuatwa na mtu mwingine .
"Nimeambiwa hapa Dodoma hakuna uhusiano mzuri baina ya watumishi wa TRA na wafanyabiashara", alisema.
Awali, akitoa taarifa yake kwa Naibu Waziri huyo, Meneja wa mkoa wa TRA Lazaro Njarabi alisema katika lengo walilopewa kwa mkoa wa Dodoma
hadi sasa wamekusanya kwa asilimia 97 na kwamba wanatarajia kuvuka lengo katika kipindi kilichobaki kumaliza mwaka.
Njarabi alitaja lengo la makusanyo walilopewa na serikali kuwa ni Sh11.5 bilioni na hadi kufikia Februari mwaka huu walishakusanya Sh7.4 bilioni na kwamba wanaamini watavuka lengo kwa kukusanya sh. 200 milioni zaidi ya malengo.
MWISHO.
Bwana Mzee,
unataka tuamini haya ndio umegundua sasa hivi, na hio dawa itaiva lini au ndio mapishi ya mawe? tusubiri yaive.
kweli njii hiii imejaa wasaniii
NAIBU Waziri wa Fedha na Uchumi, Omari Yusufu Mzee amewajia juu watumishi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na kudai kuwa, baadhi yao ni wezi wakubwa, jambo linalolifanya taifa likose usingizi kwa ajili yao.
Mzee alisema hayo jana katika ofisi za TRA, wakati wa ziara yake ya kutembelea taasisi mbalimbali zilizo chini ya Wizara ya fedha mjini hapa.
Tofauti na alivyozoeleka Naibu waziri huyo kwa upole, jana alikuwa mkali mithili ya mbogo aliyejeruhiwa na kusisitiza kwamba dawa ya wazembe wa taasisi hiyo nyeti imekwishachemka, kinachosubiriwa kwa sasa ni kuipua na kuanza kutoa dozi.
Ndugu zangu michezo yenu hii michafu, mtatuua kabisa, acheni ,kama
tunatoa mishahara mikubwa kuwapeni mnadhani kuwa tunawapeni kwa ajili ya kuangalia sura zenu, sivyo bali ni kutaka mfanye kazi kwa uaminifu na kufuata maadili, lakini sasa huu ni wizi mtupu mnaoufanya watu wa TRA," alisema na kuhoji "kwa nini msibadilike,.
Alisema kuwa umefika wakati kila mfanyakazi katika taasisi hiyo atapimwa uwezo wake mwenyewe na atakayebainika kuwa anashirikiana na wafanya biashara kuiibia serikali atatolewa kafara na kuwa mfano kwa wenzake.
Aliwataka watumishi hao mkoani humu kukaa chonjo, na kuahidi kufika kuwakagua wafanyakazi hao sikuya Julai Mosi na kuwapatia mikakati mipya.
Naibu waziri huyo alisema hakubaliani kabisa na watu wanaofanya kazi kwa mazoea na akawataka kubuni mbinu mpya za kazi ikiwa ni pamoja na kutoa elimu ya walipa kodi kwa kila mtanzania mahali popote hata maeneo ya barabarani na vijiweni.
Jambo lingine alilosisitiza Naibu Waziri huyo ni pamoja na watumishi hao kujenga mahusiano mazuri yasiyo ya kinafiki na walipa kodi ili waweze kulipa kodi kwa
hiari yao wenyewe bila ya kusukumwa au kufuatwa na mtu mwingine .
"Nimeambiwa hapa Dodoma hakuna uhusiano mzuri baina ya watumishi wa TRA na wafanyabiashara", alisema.
Awali, akitoa taarifa yake kwa Naibu Waziri huyo, Meneja wa mkoa wa TRA Lazaro Njarabi alisema katika lengo walilopewa kwa mkoa wa Dodoma
hadi sasa wamekusanya kwa asilimia 97 na kwamba wanatarajia kuvuka lengo katika kipindi kilichobaki kumaliza mwaka.
Njarabi alitaja lengo la makusanyo walilopewa na serikali kuwa ni Sh11.5 bilioni na hadi kufikia Februari mwaka huu walishakusanya Sh7.4 bilioni na kwamba wanaamini watavuka lengo kwa kukusanya sh. 200 milioni zaidi ya malengo.
MWISHO.
Bwana Mzee,
unataka tuamini haya ndio umegundua sasa hivi, na hio dawa itaiva lini au ndio mapishi ya mawe? tusubiri yaive.
kweli njii hiii imejaa wasaniii