Nikawaida kwa siku za sikukuu hasa za eid huwa watu wanakuwa wengi sana mie nilipita na nilitaka kwenda maeneo ya ufundi kilwa road ila barabara ilivyokuwa imejaa watu nikabadilisha mwelekeo maana kero yake si ndogo.
Alafu changamoto ni kuwa huwezi hata kusogeza mguu! Nyomi ya watu ni kubwa mno.
Si walisema Bodaboda/Bajaji marufuku kuingia mjini, au Kariakoo sio mjini?
Maana naona Bodaboda na Bajaji za kumwaga kama kawa