Kariakoo msimu huu wa sikukuu hapapitiki

Kariakoo msimu huu wa sikukuu hapapitiki

Wakuu kwema?

Leo nimepita kkoo kufanya manunuzi ya sikukuu! Aiseee kwanza kkoo imebadilika sana kwa Maana ya maghorofa mapya kila kona, nimeambiwa wakinga ndiyo wanaonunua nyumba Na kuporomosha maghorofa lakini pia nyomi iliyokuwepo kule ni balaa! Hapapitiki aisee. Kila kitu kinauzwa kule yaani hakuna unachoweza kukosa kkoo ila tatizo ni hiyo nyomi. Kila mtaa uko busy balaa. Nashauri angalia Kwa hii clip yangu hapo chini then ndo uamue kama unaenda kkoo au utasubiri kwanza hadi sikukuu zipite. Nawasilisha.


Mkuu, Je kule gerezani wanako uza ma vyuma nako hakupitiki ? Yaan nako kuna nyomi ?
 
Wakuu kwema?

Leo nimepita kkoo kufanya manunuzi ya sikukuu! Aiseee kwanza kkoo imebadilika sana kwa Maana ya maghorofa mapya kila kona, nimeambiwa wakinga ndiyo wanaonunua nyumba Na kuporomosha maghorofa lakini pia nyomi iliyokuwepo kule ni balaa! Hapapitiki aisee. Kila kitu kinauzwa kule yaani hakuna unachoweza kukosa kkoo ila tatizo ni hiyo nyomi. Kila mtaa uko busy balaa. Nashauri angalia Kwa hii clip yangu hapo chini then ndo uamue kama unaenda kkoo au utasubiri kwanza hadi sikukuu zipite. Nawasilisha.



Unatufanya kama wote tumetoka nanjilinji huko ndio mara ya kwanza kufika Dar,we sema unataka views tu kkoo haijaanza kujaa leo wala hayo magorofa hayajaanza kujaa leo!
 
Mkuu una mawazo mgando sana! Uelewa wako ni mfinyu sana, hilo sio tangazo! Nime share taarifa ya kile nilichokiona kkoo ili kutoa mwanga Kwa wote wenye matazamio ya kwenda kkoo kwa sasa.
Unajiona una akili sana lakini bado sana bwana mdogo

Kama unategemea kutunza familia kupitia malipo ya google ads utauza mpaka kalio kwa bei ya kutupa kabisa
 
Unajiona una akili sana lakini bado sana bwana mdogo

Kama unategemea kutunza familia kupitia malipo ya google ads utauza mpaka kalio kwa bei ya kutupa kabisa

KISIWAGA ndo biashara Yako hiyo hapa mjini? Kwanini uuuze kalio lako wakati unaweza uza hata mitumba na kuendesha familia?
 
Unatufanya kama wote tumetoka nanjilinji huko ndio mara ya kwanza kufika Dar,we sema unataka views tu kkoo haijaanza kujaa leo wala hayo magorofa hayajaanza kujaa leo!

Mzee nimekuona mjinga sana! Kwakuwa wewe umetoka nanjilinji basi unadhani kila mtu ametoka Nanjilinji, Sio kila kitu Lazima uweke comment zako. Huku ndani kuna watu wengi ni Diaspora! Waliondoka bongo kitambo sana! Wanataka kuona nini kinaendelea hapa nyumbani Na ndio sababu ya kufanya travel video Kama hiyo.
 
Wakuu.

Nimetembelea soko kuu la kariakoo kwakweli linafurahisha sana kwani ukarabati unaendelea kwa kasi ya ajabu. Ni wazi muda sio mrefu ukarabati utakuwa umekamilika hivyo hali kurejea kama kawaida.

Soko hili ambalo ni moja kati ya masoko ya kipekee zaidi Tanzania na pengine duniani lina historia ndefu sana tangu enzi za wakoloni huko. Bado sijajua hasa kampuni gani inahusika na ukarabati ila kwakweli spidi yao inatia moyo sana kwani wanafanya kazi usiku na mchana.
 
Tupe updates kwa kwenye bwawa la Nyerere.

#MaendeleoHayanaChama
 
Wakuu,

Kariakoo ina raha yake kupiga misele kama hujawahi kujaribu basi jaribu leo then utanishukuru baadaye! Kariakoo ina watu wengi sana kila siku hivyo hofu ya uchavu kuzagaa ni kubwa mno lakini Kwa sasa angalau kariakoo ni safi kabisa. Leo nimekatiza mitaa kadhaa kwakweli kunashawishi kuendelea kufanya manunuzi.
 
Wakuu,

Kwa watumiaji wa barabara za kariakoo mtakubaliana nami foleni kubwa sana itokanayo Na msongamano mkubwa sana wa watu hadi kupelekea sehemu ya dakika chache kupita Kwa zaidi ya masaa kadhaa. Ajabu ni kuwa wakati huku kwa barabara za kawaida watu wanaenda kwa tabu kutokana Na msongamano wa watu, bodaboda, magari Na bajaji upande wa magari yaendayo haraka unakuta hakuna gari Na barabara ni nyeupeeee!! Nadhani wakati umefika kwa wahusika kuliangalia hili Kwa kuruhusu magari ya kawaida kutumia barabara ya mwendokasi walau kuondoa hii tafrani.

Nawasilisha. Maendeleo hayana chama.
 
Wakuu,

Kariakoo ilikuwa Chafu sana kipindi cha nyuma. Lakini sasa hivi barabara ni safi mno! Mandhari ya Kariakoo yanavutia sana. Kwa wingi ule wa watu unaweza ambapo kila mtu ana ustaarabu wake unaweza tegemea kukuta mji ukiwa hoi kwa uchafu kila kona lakini badala yake Kariakoo Kwa sasa ndiyo inaongoza kwa usafi kuliko hata POSTA. Kuanzia hapa kituoni fire kuja mpaka huku katikati kabisa karibu Na soko kote ni kusafi mno. Bravo kwa halmashauri.

Nawasilisha.
 
Kariakoo ya kule tandamti na sikukuu au ile pale udsm au ile ya Lindi?😂
 
Wakuu,

Kariakoo ilikuwa Chafu sana kipindi cha nyuma. Lakini sasa hivi barabara ni safi mno! Mandhari ya kariakoo yanavutia sana. Kwa wingi ule wa watu unaweza ambapo kila mtu Ana ustaarabu wake unaweza tegemea kukuta mji ukiwa hoi kwa uchafu kila kona lakini badala yake kariakoo Kwa sasa ndiyo inaongoza kwa usafi kuliko hata POSTA. Kuanzia hapa kituoni fire kuja mpaka huku karikati kabisa karibu Na soko kote ni kusafi mno. Bravo kwa halmashauri.

Nawasilisha.



Naam, hii ndiyo Kariakoo ninayoifahamu. Safiiii saaaana. Naiona hata Mwendo kasi ikipita. Chakushangaza magari ni machache sana barabarani. Hii si kawaida barabara hiyo!!! Tatizo ni bei ya wese au nini.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom