mkumbwa junior
JF-Expert Member
- Oct 22, 2014
- 814
- 1,545
Karatu jana kuna jamaa saa saba usiku ameenda Kanisani kumgongea mlango Paroko amuombee, Paroko alivyofungua Kanisani jamaa aingie amuombee kumbe alikuwa na chuma akapiga sana. Paroko ameenda kufia Fame Medical.
Wananchi wenye hasira nao wamemuua Mtuhumiwa
----
Padri Pamphilius Nada wa Parokia ya Karatu amevamiwa na kuuwa na mtu ambaye anayedhaniwa kuwa hana akili timamu usiku wa kuamkia leo tarehe 19.7. 2023.
Mungu ailaze roho ya Marehemu mahala pema peponi. Amina.
KAMANDA WA POLISI ARUSHA ATHIBITISHA
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Justine Masejo amesema “Mtuhumiwa aliyemshambulia Padri kwa nyundo inadaiwa alikuwa na changamoto ya afya ya akili, naye alifariki baada ya kushambuliwa na Wananchi wenye hasira kali eneo la tukio.”
Wananchi wenye hasira nao wamemuua Mtuhumiwa
----
Padri Pamphilius Nada wa Parokia ya Karatu amevamiwa na kuuwa na mtu ambaye anayedhaniwa kuwa hana akili timamu usiku wa kuamkia leo tarehe 19.7. 2023.
Mungu ailaze roho ya Marehemu mahala pema peponi. Amina.
KAMANDA WA POLISI ARUSHA ATHIBITISHA
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Justine Masejo amesema “Mtuhumiwa aliyemshambulia Padri kwa nyundo inadaiwa alikuwa na changamoto ya afya ya akili, naye alifariki baada ya kushambuliwa na Wananchi wenye hasira kali eneo la tukio.”