Jambo ambalo naamini (binafsi) lipo na halisemwi ni hili. Vita ya majimaji sio kwamba mjerumani hakupata upinzani kutoka kwa wenyeji. Hata kama Kinjekitile alishindwa nahisi wajerumani walitumia plan B kumshinda. Hili laweza kuonekana kituko lakini tukumbuke historia yetu imeandikwa na watawala wetu (wazungu) na sijaona sehemu ambayo watanganyika walipewa ushindi isipokuwa sehemu zote wanaonekana kuwa mbuzi wa kafara na kondoo wa kuchinjwa. Yani kila vita walishindwa. Sikatai kwamba walishindwa na ndio maana tulitawaliwa, lakini sio kila sehemu wakoloni waliingia kirahisi.
Kama mbinu ya kinje ingekuwa ya hovyo, amini nawaambia ile vita ingepiganwa kwa masaa machache sana yasiyozidi mawili kwasababu vitani huwa kuna kitu kinaitwa morali. Endapo mambo yatakuwa kinyume na mipango yenu kivita na mkaelemewa mapema huwa ile hamu ya kuendelea kupigana inafifia na kuwafanya aidha mjisalimishe au mkimbie vita. Ukiangalia mwanzo hadi mwisho wa vita ni almost miaka miwili ambapo kuna mwaka mmoja katikati ulianza na kuisha wakati vita ikipiganwa (1906) siku zake zote 365 kulikuwa na vita.
Swali: ngome ya Kinjekitile ilikuwa na watu bilioni ngapi walioenda vitani hadi kufanya vita idumu kwa miaka miwili? Tukumbuke kwamba waandishi wa historia wanamuandika Kinje kama kiongozi asiye na uelewa juu ya masuala ya vita na sialaha za wajerumani. Hii ni kumaanisha kwamba kila siku vita ilipopiganwa, kulikuwa na vijana wasiojua nguvu ya risasi walikuwa wanaenda na morali ya kupigana na matokeo yake wanauawa kwa risasi ambazo hazikugeuka maji (kwa mujibu wa historia) kwasababu ni dhahiri huwezi kujificha kwenye uwanja wa vita kukwepa risasi ikiwa hauyajui madhara yake. Na hapandipo najiuliza wingi wa vijana walioshiriki ile vita hata kufanya vita ichukue muda mrefu namna hii.
Hoja yangu, huenda kweli ilifika wakati nguvu asilia ya zindiko la Kinjekitile kupungua ama kuisha kabisa lakini naamini haikuwa rahisi ama haikuwa hivihivi tu, kuna namna mjerumani alitafuta namna ya kumdhoofisha kwa kuwa ni dhahiri shayiri mapambano yalikuwa makali na ndio maana vita ilidumu kwa muda mrefu vile.
Jiulize zile hekaheka za october hazikuchukua hata wiki moja (october 29 hadi november 2) lakini cha moto tulikiona, mambo yangeendelea kwa mwezi mzima mfululizo ingekuwaje? Kwa kuzingatia mfano tajwa kwenye aya hii, jiulize swali hili kwamba: kama vijana wa kinje walitumia mikuki na mishale pekee huku mjerumani akiwa na risasi (bila nguvu ya yale maji) waliwezaje ku survive mikiki na hekaheka huku wakiendelea kushuhudia/kuletewa taarifa za mauaji ya askari wenzao waliokuwa wakienda vitani bila kujisalimisha?
Mimi naamini kama Kinjekitile asingekuwa na akili, vita ingedumu labda mwezi mmoja (siku 7 za kupigwa, na zingine za kutoroka uwanja wa vita) na baada ya hapo himaya yote ingejisalimisha na hata wanajeshi wa Kinjekitile wangemuasi kwa kuwa wanakufa hovyo.
Naomba kuwasilisha.