Kapteni Tesha ni sauti ya waliowengi Jeshini, hapo kinachosubiriwa ni nafasi (opportunity), kikitokea tu kikundi kma cha M23, utaona wimbi la uasi litakavyo tokea na kuungana na hilo kundi, hapo bado wananchi hasa waliopoteza ndugu zao…
Hilo kundi la M23 lilikuwepo kule Kibiti mbona Kapteni Tesha hakuungana nao? wanaJeshi wa JWTZ hawakuchaguliwa kujiunga na jeshi kiboyaboya kama unavyodhani. Usidhani wanajeshi wa JWTZ hawajui dunia inakwendaje.
Shida yetu pekee tuliyonayo sisi ni viongozi wezi kuachwa bila kupewa adhabu wanayostahili, wamejiwekea kinga, baaasi!!! Mengine haya ni kwaajili ya usalama na ustawi wa taifa.
Vyama vya upinzani Afrika havijafikia levels za kuongoza mataifa yao kwasababu zifuatazo:
1. Havina sera mbadala na vyama tawala
2. Vingi vinategemea nchi za Magharibi (waloni wetu) kuviingiza madarakani.
3. Wanatumia uongo na shida zilizopo Afrika kuwashawishi vijana wawaunge mkono.
4. Asilimia 80 ya shida za mataifa ya Afrika zimetokana na mfumo wa dunia unaotawaliwa na wazungu kama vile World Bank, IMF, Shirika la biashara la dunia (WTO), kura ya VETO.
5. Havina pia technolojia ya kuvuma rasilimali zetu wala masoko huru ya kuuza rasilimali zetu.
Ndiyo maana Afrika ni ileile hata kwa zile nchi ambazo vyama vya upinzani vimeshinda uchaguzi. Hata kule Libya, Iraq, DRC, Sudan, na Somalia wanachi wao sasa hivi wanazikumbuka serikali zao zilizoangushwa. Wanaona ni heri ya vile kuliko hivi, heri ya yule kuliko huyu.
Majeshi yetu yameshiriki peace keeping nyingi ndani na nje ya Afrika wanafahamu namna vyama vya upinzani vya kweli kwa taifa na vya uongo kwa taifa.