Richard
Platinum Member
- Oct 23, 2006
- 16,630
- 25,586
Kapteni John Tesha ambae ni mkufunzi (Instructor) wa wanafunzi wa kurusha ndege za kivita kajitokeza akisema alosema.
Mengi alosema Kapteni Tesha yamezungumzwa pia na aliekuwa balozi wa Tanzania nchini Cuba (Kuba) balozi Humphrey Polepole.
Kama ni kweli huyo ni Kapteni Tesha basi na ni kweli ni mkufunzi wa wanafunzi wanorusha ndege za kivita basi atakuwa ana cheti cha QIF (Qualified Flight Instructor).
Kama ni kweli Kapteni Tesha ana sifa hizi ni mtu muhimu sana kwa nchi zingine ambako ataweza kufundisha marubani wanafunzi wa kawaida, wa kibiashara na wale wa kutaka kupata cheti tu.
Huyu Kapteni Tesha ikiwa ana QIF lakini akapata pia QIFI ni kwamba aweza kutoa alama kuhusu kifaa cha matumizi yaani ndege (instrument rating).
Pia Kapteni tesha aweza kutoa mapitio kuhusu ndege (flight review) na kuiidhinisha kwamba yaweza kurushwa angani kwa matumizi ya mafunzo. Isitoshe Kapteni Tesha ni mtu ambae ana uwezo wa kutayarisha mitihani ya vitendo ambayo huchukua hadi masaa 3 ndani ya siku 60 baada ya kutoa mafunzo kwa masaa 200.
Kutokana na ujuzi wake huo wa kuwa ni mkufunzi (Instructor) Kaptei Tesha aweza kuwa amepata mafunzo kutoka katika moja ya nchi kama India, Uingereza, Canada au Afrika Kusini.
Ukiangalia sana hapo Kapteni Tesha hana muda wowote wa kufanya siasa na hata alipokuwa akisoma alokisoma amesoma kwa umakini sana na kuonyesha jinsi alivyokuwa amejiandaa. Na je, ni kweli kapteni Tesha aweza kuchukua hatua kama hiyo ya kuacha ukufunzi wake unompa ulaji na akafanya jambo alolifanya?
Pili, ni kuhusu kaimu mkurugenzi wa habari na uhusiano wa JWTZ kanali Bernard Masala Mlunga ambae akaimu nafasi hiyo kutoka kwa msemaji aliezoeleka luteni kanali Gaudentius Ilunda ambae haijulikani kama yupo likizo au vipi.
Kama kumbukumbu zangu ziko uzuri, kanali Mlunga aliteuliwa kuwa mpambe (Aide de Camp ADC) wa raisi hayati John Magufuli mwaka 2018 baada ya aliekuwa mpambe wake kanali Mkelemi kuomba kupewa majukumu mengine.
Jana baada ya kutafakari kwa kina JWTZ wakamtuma kanali Mlunga ambae sura yake si ngeni kwa watanzania wengi ambao bado wana kumbukumbu ya hayati John Magufuli, kutoa taarifa ya kutokanusha au kukanusha juu ya yale yaloelezwa na Kapteni Tesha.
Na hapo tusisahau kuwa mkuu wa majeshi mwenyewe alisema kule Mbweni kwamba huko serikalini kuna wageni ambao wamepewa ajira katika idara nyeti za serikalini, na baadae hakukutolewa maelezo yoyote kufafanua alikosema mkuu huyo wa wajeda.
Hivyo basi yaonekana kuwa leo ni siku ya Alhamisi na kuna mtu achambua mchele na hukohuko (jikoni) yupo mkata nyama na mchemshaji, mtwanga vitunguu swaumu, mmenya hiliki, bila kusahau wataonunua giligilani, chumvi na sufuria ili shaba lipikwe na watu wale.
Je, Kapteni Tesha ni chambo tu, au ndio ule msemo wa dalili ya mvua ni mawingu ndo wakaribia kuwa ni kweli?
Mengi alosema Kapteni Tesha yamezungumzwa pia na aliekuwa balozi wa Tanzania nchini Cuba (Kuba) balozi Humphrey Polepole.
Kama ni kweli huyo ni Kapteni Tesha basi na ni kweli ni mkufunzi wa wanafunzi wanorusha ndege za kivita basi atakuwa ana cheti cha QIF (Qualified Flight Instructor).
Kama ni kweli Kapteni Tesha ana sifa hizi ni mtu muhimu sana kwa nchi zingine ambako ataweza kufundisha marubani wanafunzi wa kawaida, wa kibiashara na wale wa kutaka kupata cheti tu.
Huyu Kapteni Tesha ikiwa ana QIF lakini akapata pia QIFI ni kwamba aweza kutoa alama kuhusu kifaa cha matumizi yaani ndege (instrument rating).
Pia Kapteni tesha aweza kutoa mapitio kuhusu ndege (flight review) na kuiidhinisha kwamba yaweza kurushwa angani kwa matumizi ya mafunzo. Isitoshe Kapteni Tesha ni mtu ambae ana uwezo wa kutayarisha mitihani ya vitendo ambayo huchukua hadi masaa 3 ndani ya siku 60 baada ya kutoa mafunzo kwa masaa 200.
Kutokana na ujuzi wake huo wa kuwa ni mkufunzi (Instructor) Kaptei Tesha aweza kuwa amepata mafunzo kutoka katika moja ya nchi kama India, Uingereza, Canada au Afrika Kusini.
Ukiangalia sana hapo Kapteni Tesha hana muda wowote wa kufanya siasa na hata alipokuwa akisoma alokisoma amesoma kwa umakini sana na kuonyesha jinsi alivyokuwa amejiandaa. Na je, ni kweli kapteni Tesha aweza kuchukua hatua kama hiyo ya kuacha ukufunzi wake unompa ulaji na akafanya jambo alolifanya?
Pili, ni kuhusu kaimu mkurugenzi wa habari na uhusiano wa JWTZ kanali Bernard Masala Mlunga ambae akaimu nafasi hiyo kutoka kwa msemaji aliezoeleka luteni kanali Gaudentius Ilunda ambae haijulikani kama yupo likizo au vipi.
Kama kumbukumbu zangu ziko uzuri, kanali Mlunga aliteuliwa kuwa mpambe (Aide de Camp ADC) wa raisi hayati John Magufuli mwaka 2018 baada ya aliekuwa mpambe wake kanali Mkelemi kuomba kupewa majukumu mengine.
Jana baada ya kutafakari kwa kina JWTZ wakamtuma kanali Mlunga ambae sura yake si ngeni kwa watanzania wengi ambao bado wana kumbukumbu ya hayati John Magufuli, kutoa taarifa ya kutokanusha au kukanusha juu ya yale yaloelezwa na Kapteni Tesha.
Na hapo tusisahau kuwa mkuu wa majeshi mwenyewe alisema kule Mbweni kwamba huko serikalini kuna wageni ambao wamepewa ajira katika idara nyeti za serikalini, na baadae hakukutolewa maelezo yoyote kufafanua alikosema mkuu huyo wa wajeda.
Hivyo basi yaonekana kuwa leo ni siku ya Alhamisi na kuna mtu achambua mchele na hukohuko (jikoni) yupo mkata nyama na mchemshaji, mtwanga vitunguu swaumu, mmenya hiliki, bila kusahau wataonunua giligilani, chumvi na sufuria ili shaba lipikwe na watu wale.
Je, Kapteni Tesha ni chambo tu, au ndio ule msemo wa dalili ya mvua ni mawingu ndo wakaribia kuwa ni kweli?