Kapata Chuo Dodoma Asome Accounts Akiwa Amesoma PCB –Ushauri

Kapata Chuo Dodoma Asome Accounts Akiwa Amesoma PCB –Ushauri

Seran

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2025
Posts
10,540
Reaction score
31,598
Habari wakuu,

Naomba kupata mawazo yenu kuhusu hili. Mdogo wangu amefaulu vizuri kidato cha sita akiwa na combination ya PCB, lakini amepangiwa kusoma chuo kimoja huko Dodoma Bachelor of Commerce in Accountancy katika. Hii kozi hakuichagua kabisa.

Jana kapokea majibu ya mkopo kutoka HESLB na amepewa kiasi cha ada 750,000, ambacho ni sawa na asilimia 97% ya ada kamili.

Nimemshauri kwamba akifika chuoni ajaribu kubadili kozi ili asome nursing badala ya accounts, maana kwa kweli kozi ya accounts haendani kabisa na PCB yake. Yeye anasema afadhali kapata chuo, wengine hawakupata kabisa hadi mwakani hii inaonyesha kwamba wanafunzi ni wengi sana na nafasi chache.

Anadai kuwa ada ya kozi ya nursing ni kama milioni 4.6 sasa swali langu ni:
Kama akibadili kozi kwenda nursing, je ataendelea kuchangiwa kiasi kilekile cha ada (750,000) au inaweza kuongezeka kulingana na kozi mpya?

Zamani waliosoma PCB wakapata daraja la kwanza walikuwa wanaenda moja kwa moja Muhimbili au Bugando, lakini sasa hali imebadilika sana. Hata waliofaulu vizuri wanakosa kozi walizochagua.

Nimewaza nikaishia hapa msaada tafadhali..
 
Wahasibu wengi sana aise! Kama amesoma PCB, nashauri apambane apate kozi itakayosaidia kuongeza nguvukazi kwenye sekta ya afya.
 
Inategemea yeye anapenda fani ipi, kwa sasa vijana wengi wanaingia mkenge kwa kusoma fani za ajabu kisa mkopo only wakirudi wanaanza kulima vibarua,
Kaa nae chini anaweza kuanza diploma kwa kozi yake anayoipenda then baadae akaenda ku update bachelor
 
Habari wakuu,

Naomba kupata mawazo yenu kuhusu hili. Mdogo wangu amefaulu vizuri kidato cha sita akiwa na combination ya PCB, lakini amepangiwa kusoma chuo kimoja huko Dodoma Bachelor of Commerce in Accountancy katika. Hii kozi hakuichagua kabisa.

Jana kapokea majibu ya mkopo kutoka HESLB na amepewa kiasi cha ada 750,000, ambacho ni sawa na asilimia 97% ya ada kamili.

Nimemshauri kwamba akifika chuoni ajaribu kubadili kozi ili asome nursing badala ya accounts, maana kwa kweli kozi ya accounts haendani kabisa na PCB yake. Yeye anasema afadhali kapata chuo, wengine hawakupata kabisa hadi mwakani hii inaonyesha kwamba wanafunzi ni wengi sana na nafasi chache.

Anadai kuwa ada ya kozi ya nursing ni kama milioni 4.6 sasa swali langu ni:
Kama akibadili kozi kwenda nursing, je ataendelea kuchangiwa kiasi kilekile cha ada (750,000) au inaweza kuongezeka kulingana na kozi mpya?

Zamani waliosoma PCB wakapata daraja la kwanza walikuwa wanaenda moja kwa moja Muhimbili au Bugando, lakini sasa hali imebadilika sana. Hata waliofaulu vizuri wanakosa kozi walizochagua.

Nimewaza nikaishia hapa msaada tafadhali..

Ndiyo, atapatiwa kiasi hicho hicho, labda kama akishabadilisha kozi na taarifa kufika HESLB anaweza kukata rufaa ya kuomba kuongezewa mkopo kulingana na ada ya hiyo kozi mpya.

Kila la kheri.
 
1. Kwanza uongo kwamba kapangiwa kozi ambayo hakuomba
2. Hawezi badili kozi kutoka accountancy kwenda ya afya yoyote kwa ngazi ya degree hizo nafas ni limited kwa vyuo vya serikal
3. Muache asome acha kuingilia maisha yake
4. Wewe utampoteza huyo dogo na kama unajifanya unamjal sana mpeleke private ukamlipie ada million 7 kama huwez punguza ushaur just watch
 
Vyitu vingine huwa anapanga Mungu, lazima ujiulize mtu kasoma pcb wapi na wapi na account?? Ila Mungu yeye anayeona mbele analo kusudi juu yake! Hoja kwamba kazi zake hamna ni uongo na ni kutengenezeana uoga! Nafasi za kazi zinatangazwa kila siku ni bahati ya mtu tu! Kuna watu wamesomea account na wameajiriwa mishahara yao ni minono sana!

Wakati mimi napply kozi ya kosomea chuo kikuu! Niliapply civil Engineering lakini nilichaguliwa kozi ya mechanical ambayo sikuipenda kabisa, nilienda kusoma basi tu baada ya kushauriwa na watu mbalimbali kuwa yamkini ni Mungu, kweli nilipomaliza tu sijawahi kukaa nyumbani nimefanya kazi taasisi tofouti na kampuni tofauti na kila taasisi na kampuni nilikuwa naajiriwa bila usaili hata kama wametangaza usaili nikituma tu maombi wananipigia simu kwenda kuanza kazi! Sasa hivi nimeajiriwa serikalini moja ya taasisi inayolipa vizuri Tanzania! Na kwenye usaili alihitajika mmoja pamoja na kuwa na wingi wa waomba kazi! Interview kuanzia writen, practical na oral ilikuwa ngumu lakini Mungu alinisaidia nikapata hiyo kazi! Kwa hiyo ndugu wakati mwingine ni mipango ya Mungu.
 
Kuna baadhi ya vitu hutaki kusema mfano ufaulu huo wa division 1 ni ya ngapi inawezekana miaka yenu ilikuwa ufaulu mzuri lakin sa hivi vipi

Kingine kama amechaguliwa commerce hapo ni lazima aliomba hiyo course pia unapomshauri abadilishe asome nursing inawezekana lakini siyo rahisi kama unavyozani japo inawezekana

Cha mwisho kwenye kuchagua course wewe mpe direction tu yeye ndo mwenye maamuzi ya mwisho hapo hamna formula
 
Huyo mdogo wako ndio wewe eee...

Nenda kasome kitu roho inapenda, sio ya kulazimishwa

Kama hutaki nenda kasome hiyo halafu urudi mtaani tuchome mahindi, tubeti na kufanya uwinga
 
Huyo mdogo wako ndio wewe eee...

Nenda kasome kitu roho inapenda, sio ya kulazimishwa

Kama hutaki nenda kasome hiyo halafu urudi mtaani tuchome mahindi, tubeti na kufanya uwinga
Nimemaliza chuo miaka na sijasoma masomo ya sayansi! Huwa hamuamini mtu akimuulizia ndugu yake kitu kwanini?
 
Kuna baadhi ya vitu hutaki kusema mfano ufaulu huo wa division 1 ni ya ngapi inawezekana miaka yenu ilikuwa ufaulu mzuri lakin sa hivi vipi

Kingine kama amechaguliwa commerce hapo ni lazima aliomba hiyo course pia unapomshauri abadilishe asome nursing inawezekana lakini siyo rahisi kama unavyozani japo inawezekana

Cha mwisho kwenye kuchagua course wewe mpe direction tu yeye ndo mwenye maamuzi ya mwisho hapo hamna formula
Yeye alitegemea masomo ya afya lakini ile kuona wengine wamekosa chuo mpaka mwakani akahofia na kuona ata hii alichaguliwa bora japo sio chaguo lake!
 
1. Kwanza uongo kwamba kapangiwa kozi ambayo hakuomba
2. Hawezi badili kozi kutoka accountancy kwenda ya afya yoyote kwa ngazi ya degree hizo nafas ni limited kwa vyuo vya serikal
3. Muache asome acha kuingilia maisha yake
4. Wewe utampoteza huyo dogo na kama unajifanya unamjal sana mpeleke private ukamlipie ada million 7 kama huwez punguza ushaur just watch

Comment imejaa hasira dadeqq!!
 
1. Kwanza uongo kwamba kapangiwa kozi ambayo hakuomba
2. Hawezi badili kozi kutoka accountancy kwenda ya afya yoyote kwa ngazi ya degree hizo nafas ni limited kwa vyuo vya serikal
3. Muache asome acha kuingilia maisha yake
4. Wewe utampoteza huyo dogo na kama unajifanya unamjal sana mpeleke private ukamlipie ada million 7 kama huwez punguza ushaur just watch
Unaongea kwa hasira wewe adui wa waalimu! Yani mdogo wangu kaniomba ushauri jinsi ya kubadili course ndio naingilia maisha yake! Mna mihemko sio poa..
 
Vyitu vingine huwa anapanga Mungu, lazima ujiulize mtu kasoma pcb wapi na wapi na account?? Ila Mungu yeye anayeona mbele analo kusudi juu yake! Hoja kwamba kazi zake hamna ni uongo na ni kutengenezeana uoga! Nafasi za kazi zinatangazwa kila siku ni bahati ya mtu tu! Kuna watu wamesomea account na wameajiriwa mishahara yao ni minono sana!

Wakati mimi napply kozi ya kosomea chuo kikuu! Niliapply civil Engineering lakini nilichaguliwa kozi ya mechanical ambayo sikuipenda kabisa, nilienda kusoma basi tu baada ya kushauriwa na watu mbalimbali kuwa yamkini ni Mungu, kweli nilipomaliza tu sijawahi kukaa nyumbani nimefanya kazi taasisi tofouti na kampuni tofauti na kila taasisi na kampuni nilikuwa naajiriwa bila usaili hata kama wametangaza usaili nikituma tu maombi wananipigia simu kwenda kuanza kazi! Sasa hivi nimeajiriwa serikalini moja ya taasisi inayolipa vizuri Tanzania! Na kwenye usaili alihitajika mmoja pamoja na kuwa na wingi wa waomba kazi! Interview kuanzia writen, practical na oral ilikuwa ngumu lakini Mungu alinisaidia nikapata hiyo kazi! Kwa hiyo ndugu wakati mwingine ni mipango ya Mungu.
Aisee! Asante sana ushauri mzuri sana huu! Ngoja nimpe huu..!
 
Back
Top Bottom