Kaomba ufafanuzi juu ya hili..

Kaomba ufafanuzi juu ya hili..

TANMO

Platinum Member
Joined
Apr 12, 2008
Posts
12,145
Reaction score
12,886
Waungwana kutokana na ujio wa hii Teknolojia ya picha nadhani kuna baadhi ya mambo ambayo hayakustahili kuonekana na jamii flani lakini inatokea yanawekwa wazi baada ya picha kupigwa kwenye tukio husika..

Kwa mfano, kwa mujibu wa utamaduni wa dini ya Kiislamu ni kuwa wanawake hawaruhusiwi kushiriki maziko makaburini. Nilivyoziona hizi picha ndiyo nikapata swali kuwa haiwezekani ikawa tunavunja miiko ya dini kwa kuchukua picha za tukio ambalo kuna watu hawakutakiwa kufahamu jinsi jambo linavyofanyika? (Naomba kueleweshwa juu ya hili)

Nyingine ni kitendo cha picha za maiti kwenye jeneza zikitundikwa kwenye Blogs, hivi ni sawa kweli au niko nyuma kimaendeleo?

Rejea hizi picha:
003.JPG
001.JPG
006.JPG
 
mimi nafikiri upo sawa,kwani chimbuko la dini hiyo (nchi za kiarabu awaonyeshagi picha za makaburini wakati wa tukio la mwisho),
kwa mawazo yangu elimu ya DINI bado ndogo kwa watu.inatakiwa juhudi ziongeze kuelimisha.
 
mimi nafikiri upo sawa,kwani chimbuko la dini hiyo (nchi za kiarabu awaonyeshagi picha za makaburini wakati wa tukio la mwisho),
kwa mawazo yangu elimu ya DINI bado ndogo kwa watu.inatakiwa juhudi ziongeze kuelimisha.

Kwa hiyo mkuu labda tunatumia vibaya Teknolojia kwa kuonesha visivyopaswa kuoneshwa?
 
Kwani kwenye picha hizi kuna wanawake wanaonekana kwenda huko makaburini? Mimi siwaoni unless wamejibaraguza waonekane kama wanaume!!
 
Hi ni kweli kuchukua picha ya maiti au maziko haina maana ni kuongeza huzuni tu kwa watu.
 
Uko sawa kabisa mkuu, sisi jamii ya waafrica hatuna heshima kabisa na miili ya wenzetu waliotangulia mbele ya haki. Sio vizuri kucukua picha za marehemu na kuzisambaza kwenye mablogu, hasa kwa dini ya wenzetu waislamu. Hebu cheki sasa mambo yote hadharani haa watoto wadogo wanajua ni nini kinafanyika. Tuangalia tusijekuwa watumwa wa tekonolojia.

Mimi huwa najiuliza, how comes mtu unachukua mkanda wa video kwenye mazishi, kuanzia marehemu akiwa kwenye jokofu, anavyosafishwa, valishwa na kisha akiwa kwenye jeneza. What for? hivi mtu ukiangalia mkanda kama huu si ndio kujiongezea machungu?

Africa tujirekebishe kwenye hili na kupunguza mbwe mbwe misibani.
 
tunapenda kudandia sana vitu(dini na technology) au tunapenda kumeza tu kila kitu tunacholetewa
 
mimi nafikiri upo sawa,kwani chimbuko la dini hiyo (nchi za kiarabu awaonyeshagi picha za makaburini wakati wa tukio la mwisho),
kwa mawazo yangu elimu ya DINI bado ndogo kwa watu.inatakiwa juhudi ziongeze kuelimisha.
Kama ujui mambo ya dini kaa kimya usitumie akili yako, wewe umeshiona wapalestina wanavyozika???
 
Kwa waislam kuzika wazi ndio mafundisho yana sema hivyo... sijui kwa dini zingine
 
Kwa waislam kuzika wazi ndio mafundisho yana sema hivyo... sijui kwa dini zingine

Mkuu Chatu Dume hoja yetu hapa siyo utaratibu wanaotumia Waislamu kwenye kuzika, bali kitendo cha kupiga picha shughuli ya maziko (ambayo kwa mujibu wa Uislamu, kuna watu ambao hawaruhusiwi kushiriki.. na kama hawaruhusiwi kushiriki, sidhani kama wanapaswa kujua shughuli inavyofanyika)... Kingine ni tabia ya picha za maiti kuwekwa kwenye blog mbali mbali.. Pia kuna mchangiaji amezungumzia kitendo cha kurekodi video mwili wa marehemu na shughuli za mazishi....

Mapendo.
 
wewe ni muislamu? Pili pili usioila inakuwashia nini? Wenyewe wanaona utaratibu unawafaa, wataubadilishha wakiuona kero? Kwa nini uhoji mambo ya dini za wenzako!
 
wewe ni muislamu? Pili pili usioila inakuwashia nini? Wenyewe wanaona utaratibu unawafaa, wataubadilishha wakiuona kero? Kwa nini uhoji mambo ya dini za wenzako!

Mkuu umenikusudia mimi?
Kama jibu ni ndiyo, basi jaribu kunielewa kabla hujaamua kukasirika,,,
Ninachomaanisha siyo utaratibu wa Waislamu kwenye maziko bali kitendo cha kuchukua picha kaburini..
And, yes! Mimi ni Muislamu...
 
Hi ni kweli kuchukua picha ya maiti au maziko haina maana ni kuongeza huzuni tu kwa watu.

Mmmh mimi niko nyuma kweli. Nilifikiri umuhimu wa picha ni kutunza kumbukumbu!! Babu na bibi yangu walikufa na kuzikwa kukiwa hakuna tekelinalokujia ya kamera. Hivyo sikuwa na bahati ya kutambua hata walivyokuwa wanafanana. Wakati mwingine hizi picha zinakufanya kuwa karibu na marehemu kwa hisia. Kama marehemu alikuwa na impact kubwa katika maisha yako, naamini hizo picha zinaweza kuongeza chachu katika maendeleo yako.
Ni maoni yangu tu.
 
Back
Top Bottom