Kanisa Tanzania ni CCM?

Ushawahi kuhudhuria ama unaleta nadharia tu. Maombi huwa ya kuombea nchi sasa kama ni nchi kwa nini wengine hawaalikwi ama wao si sehemu ya nchi?
 
Wachungaji wengi waongo wameumbuliwa na unafiki wa siasa za ccm
 
Yesu alisulubishwa na wapinzani ama na waliokuwa madarakani? Na wakati anasulubishwa amani ilikuwepo ama haikuwepo?
 
Ebu ficha ujinga wako hata kidogo itakusaidia.
Sasa ungejuaje ni ujinga angeuficha? Na akiuficha itamsaidia nini? Angalau ametoa ujinga wake wewe uliye mwerevu kuliko yeye, umetambua kuwa ni ujinga. Sasa umwelimishe kwa sababu mjinga anaelimika kirahisi tu.
Ebu tuwe wavumulivu tu hata kwa wale tunaodhani ni wajinga, ndani ya huo ujinga kuna kitu tofauti na werevu wako unaweza ukakiona. Binadamu wote hatuwezi kuwa sawa.
 
Unafiki tu

Sent from my VF685 using JamiiForums mobile app
 
Kanisa halina Chama bali Waumini wa Makanisa mbali mbali ndiyo ni Wanachama wa hivyo Vyama hata kwa vile Vyama ambavyo ni kama vina mrengo wa Kiitigadi au Dini fulani bado Wanachama wao ni wa dini na madhehebu mbali mbali.
Kwa mujibu wa mada iliyo ubaoni, Neno "Kanisa" lina tafsiri pana kuliko ulivyoamanisha. Itoshe tu turejee kwenye tafsiri yako ni kwamba kuna Madhehebu ya Kikristo ambayo kwenye uchanguzi wa 2015, yalikuwa kinyume na CCM wazi wazi. Sasa ukisema KANISA ni la CCM haueleweki.
Hata hivyo Madhehebu au Makanisa mengi ya Kikristo hayaruhusu au kuhubiri siasa Makanisani. Kanisa la Kikristo kazi yao Kuu ni kumhubiri Kikristo kuwa ndiye Mwokozi wa Ulimwengu. Wanapoomba Amani huwa ni kwa Taifa na siyo kwa baadhi ya watu. Ikitokea Kanisa la mahali pamoja ( area local church) wakafanya maombi kwa Rais huwa ni suala lao kama wao na kuna baadhi ya Washirika huwa hawashiriki. Hivyo siyo sahihi kusema Kanisa ni CCM

Sent from my HUAWEI Y530-U00 using JamiiForums mobile app
 
Sema huelewi siyo sieleweki. Unapotaka kusema jambo fulani lipo hivi siku zote unaangalia wingi. Nimehesabu matamasha na hiyo mikesha na kuhitimisha kwamba Kanisa linaipendelea CCM. hayo madhehebu yaliyokuwa yanaunga mkono upinzani wazi wazi ni yapi hayo?
 
sasa kwa mujibu wa dini nani anatakiwa kuombewa zaidi kati ya mwizi na mtakatifu?
Mkuu wote wanahitaji maombi, mwizi anahitaji maombi ili Mungu ambadilishe asiwe mwizi tena. Na mtakatifu anahitaji maombi ili asirudi tena kwenye uovu.
 
Kama ulifuatalia kwa karibu misimamo ya Madhehebu ya Kikristo wakati wa kampeni 2015, uliweza kuona.

Sent from my HUAWEI Y530-U00 using JamiiForums mobile app
 
Kanisa ni CCM tangu ianzishwe kasoro 1985-1995 na 2005-2015 na kipindi hicho lilishambulia sana Serikal na kutoa Makaripio Makubwa makubwa
 
Hao viongozi baadhi wadini wamekula mgao wa Rugemalira sasa wasipoishabikia serikali wataponea wapi?
 
Ngoja tusubiri wale Mapadiri warudishe zile hela maana wamezidiwa hata na muumini wao aliyeamua kurudisha baada ya miaka 3.

Sent from my SM-J320F using JamiiForums mobile app
 
Wale Viongoz ni wakitaifa mf rais Ila chama chake Ndio ccm lkn hawez mualika wa upinzan coz ndo itaonekana ndo siasa ILA leo mama mgwira anaweza alikwa ikawa haina shida lkn sio lowasa

Sent from my TECNO-W5 using JamiiForums mobile app
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…