Kanisa Tanzania ni CCM?

Kanisa Tanzania ni CCM?

Maombi hulenga mtu sio chama mungu hatambui vyama viwe chadema au CCm ukiombea amani unaombea wasimamizi wa amani walioko madarakani kwa kuwataja kwa majina au vyeo ambao kazi yao masaa 24 ni kusimamia amani yaani unaombea amiri jeshi mkuu na wote wahusikao na kazi ya kusimamia amani wakiwemo polisi na majeshi yote ya ulinzi na usalama huhangaiki na bavicha au bawacha
Ushawahi kuhudhuria ama unaleta nadharia tu. Maombi huwa ya kuombea nchi sasa kama ni nchi kwa nini wengine hawaalikwi ama wao si sehemu ya nchi?
 
Wachungaji wengi waongo wameumbuliwa na unafiki wa siasa za ccm
 
Kitu cha kwanza kabisa kanisa linachotaka ni amani ambayo itawezesha neno/injili kuwafikia watu wengi sana, mambo mengine ni personal perceptions.

Zaidi kama kuna tatizo kanisa hufanya kazi ya maombi ya usiku na mchana.

"the highest risk should give maximum profit"
Yesu alisulubishwa na wapinzani ama na waliokuwa madarakani? Na wakati anasulubishwa amani ilikuwepo ama haikuwepo?
 
Ebu ficha ujinga wako hata kidogo itakusaidia.
Sasa ungejuaje ni ujinga angeuficha? Na akiuficha itamsaidia nini? Angalau ametoa ujinga wake wewe uliye mwerevu kuliko yeye, umetambua kuwa ni ujinga. Sasa umwelimishe kwa sababu mjinga anaelimika kirahisi tu.
Ebu tuwe wavumulivu tu hata kwa wale tunaodhani ni wajinga, ndani ya huo ujinga kuna kitu tofauti na werevu wako unaweza ukakiona. Binadamu wote hatuwezi kuwa sawa.
 
Unafiki tu

Sent from my VF685 using JamiiForums mobile app
 
Kwanza nitangaze kabisa Maslahi binafsi kwenye hoja yangu hii. Mimi ni Mkristo na hapa ninaposema "Kanisa" namaanisha mjumuiko wa wakristo na wala sizungumzii "madhehebu". Kwa ivo ninaposema Kanisa namaanisha mjumuiko wa wakristo wote waliomo kwenye madhehebu mbali mbali hapa Tanzania.

Kwa muda mrefu sana madhehebu mbali mbali yamekuwa yakiandaa mikesha ama matamasha ya "amani" kuombea nchi yetu. Jambo la kushangaza haijawahi hata kwa bahati mbaya kutokea kwenye matamasha hayo waandaaji wakawaalika wanasiasa toka vyama vya upinzani kuwa wageni Rasmi. Hao waandaaji wanaposema wanaombea amani wanamaanisha ni dhidi ya wapinzani? Au mungu wao anawaonesha kwamba amani inaletwa na CCM?

Mwezi uliopita ulikuwa ni kama mwezi wa mashindano ya mikutano ya kumuombea Rais John Magufuli. Lakini huwezi kuona wanaokimbizana leo kumuombea Magufuli wakifanya hivyo kwa viongozi wa vyama vya upinzani. Jee vyama vya upinzani viongozi wake hawatakiwi kuombewa ili wapate "ulinzi" wa Mungu. Ama mungu wa Maaskofu si Mungu wa viongozi wa vyama vya upinzani?

Wakati wa Uchaguzi utawasikia Maaskofu wakitoa salamu za "uchaguzi" kwa kutumia kauli mbiu zinazotumiwa na CCM. Wao "amani na utulivu" ni pale tu CCM inapobakia madarakani. Na baada ya uchaguzi hata kama kuna watu wanadai kudhulumiwa haki yao ya ushindi utawasikia Maaskofu wanasema "tunashukuru mungu" uchaguzi umepita kwa amani.

Hivi msimamo wa hawa viongozi wa Kanisa kuhusu Uchaguzi wa Zanzibar ulikuwaje? Au waliamini alichokisema Lukuvi?
Kanisa halina Chama bali Waumini wa Makanisa mbali mbali ndiyo ni Wanachama wa hivyo Vyama hata kwa vile Vyama ambavyo ni kama vina mrengo wa Kiitigadi au Dini fulani bado Wanachama wao ni wa dini na madhehebu mbali mbali.
Kwa mujibu wa mada iliyo ubaoni, Neno "Kanisa" lina tafsiri pana kuliko ulivyoamanisha. Itoshe tu turejee kwenye tafsiri yako ni kwamba kuna Madhehebu ya Kikristo ambayo kwenye uchanguzi wa 2015, yalikuwa kinyume na CCM wazi wazi. Sasa ukisema KANISA ni la CCM haueleweki.
Hata hivyo Madhehebu au Makanisa mengi ya Kikristo hayaruhusu au kuhubiri siasa Makanisani. Kanisa la Kikristo kazi yao Kuu ni kumhubiri Kikristo kuwa ndiye Mwokozi wa Ulimwengu. Wanapoomba Amani huwa ni kwa Taifa na siyo kwa baadhi ya watu. Ikitokea Kanisa la mahali pamoja ( area local church) wakafanya maombi kwa Rais huwa ni suala lao kama wao na kuna baadhi ya Washirika huwa hawashiriki. Hivyo siyo sahihi kusema Kanisa ni CCM

Sent from my HUAWEI Y530-U00 using JamiiForums mobile app
 
Kwa mujibu wa mada iliyo ubaoni, Neno "Kanisa" lina tafsiri pana kuliko ulivyoamanisha. Itoshe tu turejee kwenye tafsiri yako ni kwamba kuna Madhehebu ya Kikristo ambayo kwenye uchanguzi wa 2015, yalikuwa kinyume na CCM wazi wazi. Sasa ukisema KANISA ni la CCM haueleweki.
Sema huelewi siyo sieleweki. Unapotaka kusema jambo fulani lipo hivi siku zote unaangalia wingi. Nimehesabu matamasha na hiyo mikesha na kuhitimisha kwamba Kanisa linaipendelea CCM. hayo madhehebu yaliyokuwa yanaunga mkono upinzani wazi wazi ni yapi hayo?
 
sasa kwa mujibu wa dini nani anatakiwa kuombewa zaidi kati ya mwizi na mtakatifu?
Mkuu wote wanahitaji maombi, mwizi anahitaji maombi ili Mungu ambadilishe asiwe mwizi tena. Na mtakatifu anahitaji maombi ili asirudi tena kwenye uovu.
 
Sema huelewi siyo sieleweki. Unapotaka kusema jambo fulani lipo hivi siku zote unaangalia wingi. Nimehesabu matamasha na hiyo mikesha na kuhitimisha kwamba Kanisa linaipendelea CCM. hayo madhehebu yaliyokuwa yanaunga mkono upinzani wazi wazi ni yapi hayo?
Kama ulifuatalia kwa karibu misimamo ya Madhehebu ya Kikristo wakati wa kampeni 2015, uliweza kuona.

Sent from my HUAWEI Y530-U00 using JamiiForums mobile app
 
Kanisa ni CCM tangu ianzishwe kasoro 1985-1995 na 2005-2015 na kipindi hicho lilishambulia sana Serikal na kutoa Makaripio Makubwa makubwa
 
Hao viongozi baadhi wadini wamekula mgao wa Rugemalira sasa wasipoishabikia serikali wataponea wapi?
 
Ngoja tusubiri wale Mapadiri warudishe zile hela maana wamezidiwa hata na muumini wao aliyeamua kurudisha baada ya miaka 3.

Sent from my SM-J320F using JamiiForums mobile app
 
Wale Viongoz ni wakitaifa mf rais Ila chama chake Ndio ccm lkn hawez mualika wa upinzan coz ndo itaonekana ndo siasa ILA leo mama mgwira anaweza alikwa ikawa haina shida lkn sio lowasa

Sent from my TECNO-W5 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom