Kanisa la TAG mbona kama limepoa?

Kanisa la TAG mbona kama limepoa?

mchecheto

JF-Expert Member
Joined
Oct 30, 2014
Posts
1,532
Reaction score
1,465
Habari za muda huu waungwana?
Natumai mnaendelea vizuri hasa baada ya mihangaiko ya siku.

Niende moja kwa moja kwenye mada niliyokusudia kuianzisha leo.

Kwa wale wakristo mtakua mpo aware zaidi kuhusu ukristo ulivyo na ulivyo hapa nchini.

Miaka ya nyuma kidogo ukristo ulikua imeenea zaidi kwa makanisa ya Romani Catholic, Lutheran na Pentecoste. Miaka ilivyokwenda zaidi ndipo tulipo shuhudia idadi kubwa ya makanisa hapa nchini.

Nakumbuka miaka ya 2000 kanisa la TAG lilianza kuja kwa kasi sana. Kufikia miaka ya '03-0'5 walikua wanasikika sana kutokana na makongamano makubwa na mahubiri yao.
Hawa watu walikua wanaponda sana makanisa mengine hususan wakatoliki.Hapa ndipo walipopata waumini wengi kutoka makanisa kongwe niliyotaja hapo juu kutokana na miujiza waliyokua wanafanya makanisani mwao kama kutoa pepo na kuombea wagonjwa just little to mention.

Walikua kwa kasi sana na hapa matajiri wengi pia walihamia huko wakajenga makanisa nchi nzima na kukua kwa kasi kutokana na styl yao mpya ya kuabudu na mahubiri.

Ilikua changamoto sana kuoa binti wa kilokole enzi hizo.Ilifika mahali mtu akitoka katoliki,lutheran au pentecoste akajiunga TAG alikua anatengwa na familia na ndugu na aliitwa muasi.Ikafika mahali kukawa na kama ka uadui fulani kati madhehebu hayo.
Enzi hizo karibu kila mlokole alikua anaweza kutoa pepo na kuongea zile lugha zao.

Miaka ilivyo anza kwenda sasa;taratiiibu ile power yao ya ku preach na kufanya miujiza ikaanza kupotea na kufifia.
Hivi sasa wameshazoeleka na wapo very normal sana.
Hivi sasa wana intergrate na wakristo wengine vizuri sana tofauti na zamani.

Maswali yangu:

1:Kwanini TAG wamepoa sana na hawapo hot kama zamani?
2:Je mi kwa sababu waumini wamesha jaa hivyo basi hawana nia ya ku expand zaidi?
3:Au ni utandawazi unachangia?

Karibuni kwa mawazo
 
Bado TAG wapo vizuri mkuu,nadhani wabongo unawajua kwa kushobokea vipya na mda mfupi wanasahau......
Miaka ya nyuma hakukuwa na mabii/mitume wengi kama Leo,hawa jamaa wameiga vitu vingi kutoka Pentecostal churches,ingawa kuna vingine wamechakachua,
Nachowapendea TAG wanasimamia neno(bible)
Utandawazi na emerging ya kizazi cha vijana wa kisasa kanisani kunapunguza ule uamsho kama wa zamani.
Utajiri wa Wachungaji,now days Wachungaji wamekua matajili sana wa pesa,hiyo ile halo ya kutosheka imewakamata baadhi ya viongozi hata ile kasi ya kumtafuta Mungu imeshuka
N:B bado TAG ni moja ya dhehebu bora kwa makanisa ya kipetecost,
 
Limekuwa kiwanda cha kufyatua mitume na manabii fake

Manabii tata wa aina uliotaja hawatoki katika madhehebu ya Kipentekoste ya asili ya kale "orthodox" kama vile TAG, FPCT, EAGT, PEFA, Holiness, PAG, Elim, KLPT na wengineo. Wapo wachache sana kutoka madhehebu hayo. Kwa haraka ni mmoja kwa kila manabii wa aina hiyo kumi.Sababu kubwa ni kuwa madhehebu hayo ya Kipentekoste niliyotaja yanakubali Elimu ya Thiolojia Katika utendaji kazi ya Mungu.

Sifa moja ya mtu kuwa Kiongozi ngazi ya juu kama vile Mchungaji Kiongozi ni kuwa amesoma Katika Chuo cha Theolojia kwa ngazi ya Diploma ama zaidi.Elimu inaondoa hayo unayoita "feki"." Hawa hupata malezi ya kutosha ndani ya mafundisho na utendaji wa Kipentekoste asilia hadi kuiva kabla ya kusimamia makanisa makubwa.
 
Yalikuwa makanisa ya mpito tu, na Hiyo TAG itafutika au kuisha kabisa, yatabaki Makanisa ya Wachungaji tu, nayo yatafutika pale mwenye Kanisa akifa
 
Habari za muda huu waungwana?
Natumai mnaendelea vizuri hasa baada ya mihangaiko ya siku.

Niende moja kwa moja kwenye mada niliyokusudia kuianzisha leo.

Kwa wale wakristo mtakua mpo aware zaidi kuhusu ukristo ulivyo na ulivyo hapa nchini.

Miaka ya nyuma kidogo ukristo ulikua imeenea zaidi kwa makanisa ya Romani Catholic, Lutheran na Pentecoste. Miaka ilivyokwenda zaidi ndipo tulipo shuhudia idadi kubwa ya makanisa hapa nchini.

Nakumbuka miaka ya 2000 kanisa la TAG lilianza kuja kwa kasi sana. Kufikia miaka ya '03-0'5 walikua wanasikika sana kutokana na makongamano makubwa na mahubiri yao.
Hawa watu walikua wanaponda sana makanisa mengine hususan wakatoliki.Hapa ndipo walipopata waumini wengi kutoka makanisa kongwe niliyotaja hapo juu kutokana na miujiza waliyokua wanafanya makanisani mwao kama kutoa pepo na kuombea wagonjwa just little to mention.

Walikua kwa kasi sana na hapa matajiri wengi pia walihamia huko wakajenga makanisa nchi nzima na kukua kwa kasi kutokana na styl yao mpya ya kuabudu na mahubiri.

Ilikua changamoto sana kuoa binti wa kilokole enzi hizo.Ilifika mahali mtu akitoka katoliki,lutheran au pentecoste akajiunga TAG alikua anatengwa na familia na ndugu na aliitwa muasi.Ikafika mahali kukawa na kama ka uadui fulani kati madhehebu hayo.
Enzi hizo karibu kila mlokole alikua anaweza kutoa pepo na kuongea zile lugha zao.

Miaka ilivyo anza kwenda sasa;taratiiibu ile power yao ya ku preach na kufanya miujiza ikaanza kupotea na kufifia.
Hivi sasa wameshazoeleka na wapo very normal sana.
Hivi sasa wana intergrate na wakristo wengine vizuri sana tofauti na zamani.

Maswali yangu:

1:Kwanini TAG wamepoa sana na hawapo hot kama zamani?
2:Je mi kwa sababu waumini wamesha jaa hivyo basi hawana nia ya ku expand zaidi?
3:Au ni utandawazi unachangia?

Karibuni kwa mawazo
Tanzania Assemblies of God-T.A.G is even stronger than before:
1.Imekuwa na matawi nchi nzima, kila wilaya, kila kata.
2. T.A.G is the strongest Pentecostal denomination in the country. Askofu mkuu wa T.A.G ndiye Rais wa makanisa yote ya ki Assemblies ya Africa.
3.Ndiyo dhehebu pekee la kipentecost nchini lenye vyuo vya Biblia vinavyotoa diploma, degree hadi masters kwa kushirikiana na Global University ya USA
3.Ni dhehebu la kipentecost pekee nchini linalopeleka wamisionari nje ya Tanzania kama Rwanda, Burundi, Sudan kusini, DRC, na Magasca.
4.Linahubiri injili nchini kwa kasi zaidi kuliko huko nyuma.

Ukiangalia takwimu ya Nini T.A.G ilifanya huko nyuma na nini inafanya kwa sasa, na Neno linataka kanisa liweje utagundua kuwa ndiyo lina peak kwa viwango vikubwa.
 
Makanisa ya watu binafsi nayoyakubali ni mawili tu, lile la Kakobe na la Gwajima hawa jamaa wanapinga sana watu wanao jiita mitume na manabii karne hii ya 21
 
Wachujgaji wa makanisa haya wengi ni wana usalama waliopenyezwa kwa sababu maalum,sio kumhubiri Yesu wa Nazareth,ndio maana unayaona yako mengi na wanaonyesha kila TV wakati waumini wao hata wengine hawafikishi 60

Wanachofanya ni kazi maalum ya kisaikolojia kuwaondoa wananchi kwenye hoja za kuihoji serikali kuhusu mambo ya uchumi,afya,elimu,na maendeleo kwa ujumla,na kuwaambia mambo yote na shida zao ni kazi ya mungu,hivyo waendelee kumuomba

Sehemu ngumu iliyowasumbua ni misikitini,lakini wamefanikiwa kuwakaba bakwata lakini bado usumbufu wa akina sheikh ponda na wengine upo,wao wanaita usumbufu
 
Wachujgaji wa makanisa haya wengi ni wana usalama waliopenyezwa kwa sababu maalum,sio kumhubiri Yesu wa Nazareth,ndio maana unayaona yako mengi na wanaonyesha kila TV wakati waumini wao hata wengine hawafikishi 60

Wanachofanya ni kazi maalum ya kisaikolojia kuwaondoa wananchi kwenye hoja za kuihoji serikali kuhusu mambo ya uchumi,afya,elimu,na maendeleo kwa ujumla,na kuwaambia mambo yote na shida zao ni kazi ya mungu,hivyo waendelee kumuomba

Sehemu ngumu iliyowasumbua ni misikitini,lakini wamefanikiwa kuwakaba bakwata lakini bado usumbufu wa akina sheikh ponda na wengine upo,wao wanaita usumbufu
Nikweli
 
Back
Top Bottom