Kanisa katoliki wamwibia mjane


wewe unazungumzia issue ya Getrude Lwakatare, yule mama mchungani, mbunge na mmiliki wa shule za st. marys, yeye alienda kujenga eneo siyo la kwake na hakuwa na kielelezo chochote, ndiyo maana Ardhi wakamvunjia zile nyumba na kumrudishia lile eneo yule mjane.

Lease ni mkataba wa ukodishaji wa eneo (pango au shamba) ukisema mtu ana lease, unamaanishwa amekodishwa tu, (ila kuna kitu kinaitwa government lease, ambayo kwa Tz inajulikana kama Right of Occupancy/ hati miliki) sasa kama yeye ana lease, ujue alikodishwa kwa muda fulani, na kama muda huo umekwisha basi eneo litarudi kwa muhusika.

sisi huwa tunapenda kuwa mashabiki wa mambo tusiyoyajua bila kufanya utafiti,

sasa mleta uzi ameliHUKUMU kanisa bila kutoa uthibitisho, kama anayoyasema yana ukweli, basi alete uthibitisho, mbona yupo kimya? wakati vielelezo vipo?, kama atathibitisha hata mimi nitamsaidia, maana kaamua kulileta hili suala JF basi asisite kutoa ushahidi.

na kama anaona hapa siyo mahala pa kuweka huo ushahidi basi hakutakiwa kulihukumu kanisa kiasi hicho maana yeyw siyo mahakama.

na wanavyosema huyo mama ana hati, je ana hati ya aina gani?.
 
kitu kingine. sheria za Ardhi hususani Land Act na Village Land Act haziruhusu mtu ambaye si raia wa Tanzania kumiliki ardhi.

sasa wewe mleta uzi em tueleze, huyo mzungu alikuwa ni mtanzania au?, na kama hakuwa mtanzania hiyo ardhi alikuwa anaimiliki kwa namna gani?.

TATIZO LA WATU WENGI DUNIANI HUWA WANAPENDA KUSEMA YALE WANAYOYAJUA KWA JINSI WANAVYOJUA, ......KULIKO KUSEMA JINSI KITU KILIVYO.

sasa hapa mleta mada kasema jinsi anavyojua na siyo jinsi kitu kilivyo, na ndiyo maana ameshindwa kuthibitisha.
 
huo ushahidi mzima uko wapi? au kesho haijafika? au na wewe in mjane wa huyo muitaliano?

Mtu akikwambia kesho bila kukutajia tarehe, mwezi na mwaka husika kamwe kesho haitafika, kila siku mpya, siku itayofuata itakuwa ni kesho!
 

masuala ya ardhi watu wanayachukulia poa sana, bila kujua historia ya eneo husika, sasa hawa nao wamekazania lease, bila kujua wanazungumzia nini?
 
Usituhadae mkuu, this is second registration ya wewe mleta mada huwezi jiunga jf leo kwa ajli ya suala la huyo mjana jana 26.08.2014 please lete lease kwanza ndo tukuamini tumeenda shule cc na c bla blah u. Jipange ksha urudi kivingine mkuu

hahahaaaa, unafaa kuwa intelijensia mkuu
 
Hii Taasisi mwisho umefika, kila siku matatzo tele Mapadre kulawiti, Padri lwambano kafumaniwa, macsta malaya balaa!

wewe ndiye uliyefika mwisho, ukatoliki utaendelea kusimama na kukuwa kokote duniani.

kanisa halitakaa litetereke, bali walipingao ndio watakotetereka.
 

ni bora ya wewe ambaye umejifanya haulewi na huja support jambo lolote, mimi binafsi nazifahamu sheria vizuri tu,
wala sijataka kumbishia mleta uzi moja kwa moja japokuwa mimi nj mkatoliki, nimemuomba alete hizo documents hapa ili kuthibitisha hizo tuhuma zake.

mpakavsasa kimya, lease haokufanyi wewe kuwa mmiliki wa kiwanja. lease kwa sababu kinachofanyika hapo ni kupewa HAKI (interest in land) ya kutumia ardhi kwa kipindi fulani, na siyo haki ya kumiliki ardhi, kwa lugha rahisi unaweza sema ukodishaji. yaani ni sawa na wewe uingie mkataba na mtu mwenye jengo pale stand ta moshi, au pale kariakoo kwa ajili ya biashara (frame) aina ya mkataba itakayotumika hapo itakuwa ni lease agreement.

sasa kile kipindo kikiisha haki ya kutumia hilo eneo inakuwa imekwisha na yenyewe.

hapo kwa namna yoyote huwezi dai hilo eneo.
 
Siamini kuwa padre anaetajwa kumuachia mjane alikuwa anamiliki hiyo ardhi. Kumbuka tabia ya mapadre kumiliki mali imeanza miaka ya karibuni. Zamani (hadi kipindi kinachodaiwa huyo mjane kuachiwa shamba) mapadre na watawa walitakiwa kuishi maisha ya hali ya chini kama waumini wao hohe hahe. Hiyo lazima itakuwa ardhi inayomilikiwa na Kanisa.
 

Tunatatizo kubwa sana, huyu bwana kasema alitakiwa kuombwa ushahidi tayari wapuuzi wamesha mhukumu na kuandika upuuzi mbali mbali. Inaudhi sana.
 
Tunatatizo kubwa sana, huyu bwana kasema alitakiwa kuombwa ushahidi tayari wapuuzi wamesha mhukumu na kuandika upuuzi mbali mbali. Inaudhi sana.

wamemwmbia alete ushahidi, akasepa!
 

hizo mambo ni kawaida kwa makanisa nenda ubungo uone kanisa kkkt na anglikana wanavyoiba kiwanja cha shule ndo utaamini hilo jambo si ajabu kwa hizo taasisi
 
sitafuti public sympathy mzee,hili swala linajulikana marangu nzima,iyo lease nitaiweka apa

Acha kukurupuka,Kanisa katoliki wako makini sana kwenye umiliki wa ardhi,tembea Tanzania nzima hasa sehemu zile ambazo wamisionari walifika mapema utagundua kuwa walimiliki maeneo makubwa sana na kupata lease.
kuna sehemu moja huko Mkoani Katavi inaitwa Karema,hapo Karema Wamisionari walifika miaka ya 1910's wakachukua eneo kubwa na kujipatia lease.
Hivi karibuni kulitokea mgogoro mkubwa na serikali ya kijiji baada ya Kanisa kuwakataza wanakijiji kujenga katika baadhi ya maeneo ya kijiji hicho kwa kuwa tayari wanamipango ya kuyatumia maeneo hayo.wanakijiji pamoja na wanasiasa walipinga sana hilo,lakini mwisho wa siku Kanisa lilionesha lease ambayo iko hai na barua toka kwa msajili ikionyesha kuwa kijiji kililikuta kanisa,hivyo kanisa ndilo linamiliki sehemu yenye mgogoro na hata baadhi ya sehemu walizojenga wanakijiji.
So,mleta mada inatakiwa uwemakini unapochokonoa mada usizokuwa na uhakika nazo au kwa makusudi unataka kuonewa huruma
 
mbona watu wanakuwa hawana busara,acheni ushabiki usiyo wa msingi.mi mwenyewe ninajua habari hii kw undani.hakuna mzungu aliekaribishwa pale bwana.yule jamaa alikua mmiliki halali wa eneo lile ambalo lilikuwa la familia baada ya kuwa na mtoto na yule mama ambae ni kweli alikuwa nesi pale.ndo akajenga nyumba ya familia pale.angekaribishwa angejenga nyumba.na kama ilkuwa mali ya kanisa alipojenga kanisa lilikuwa wapi?na mbona kanisa limesubiri miaka yote hiyo.ivi kuna watu walosoma kwene hili kanisa kweli.kwa nini hamjapaga mkataba wa kukaa miaka yote.Tatizo wenye ukweli wengi wamekufaga.walioko ni walaku tu na wenye wivu.Kanisa Catholic achen kumuoea yule mjane.kuweni na hofu ya Mungu.Baba askofu unaacha wapi neno linalosema kuwa dini safi ni ile inayotazama wajane na kujilinda na ubaya usitende dhambi.utasimamiaje dhambi kubwa namna hii,utalishaje kondoo ndani ya dhambi.kanisa mna maeneo mengi,la mjane litawafaa nini.acheni dhuluma yule mama pale ni kwake.Dunia na vyote viijazo ni mali ya bwana.MUNGU HADHIAKIWI.MSISALI HUKU MNAMWIBIA MJANE.just magine case kama hii ina ingia rushwa,kanisa catholic mnapata wapi fedha za rushwa.SADAKA!!!Nimeigia mtiu kule marangu anitonya kuwa kuna mianya ya rushwa sana.na rushwa inaendeshwa na kanisa catholic.
 
Benteke acha kuongea mambo ya ajabu.kuasi utawa kuna husika nini hapa?Halafu wewe huyo kijana huyo mama kutembeana wasichana Arusha ndo kunako sababisha kanisa catholic kumnyanganya mamayake eneo lake?Mbona maelezo yako hayana maana na kilichoelezwa.life stle ya mtu na choices zake,hazikuwa na umuimu hapa.Soma post uelewe
 

hayo ni yako
 

weka ushahidi usilopoke pia kuwa makini unapozungumzia imani za watu manake hapa umejumlisha kama kasuku
 

He he heee duu kweli nimeamini catholic ni kampuni yenyewe na bahressa kwa sasa hawana tofauti japo mwenzake bahresa hadhulumu mtu
 

Hii inanikumbusha jamaa mmoja aliyeletwa na babu yangu huko kijijini kwa ajiri ya kuoka mikate. Babu akamruhusu kuishi katika eneo lililo ndani ya shamba letu (ambalo lina title) wakati akitekeleza ajira yake. Bahati mbaya babu yangu akafariki hapo mwaka 1983. Miaka kama sita baada ya kifo cha babu, yule mzee muoka mikate nae akafariki, ghafla wanae wakaibuka kusikojulikana kuja kuuza shamba bila kujua mzee wao alipewa aishi wakati akitekekeza ajira yake. Na hata alipozeeka aliruhusiwa kuendelea kuishi hapo kumalizia maisha yake. Vijana hao waliondoka kwa aibu baada ya kushindwa kuthibitisha umiliki wa shamba hilo mahakamani kwa kudai kwamba walijua baba yao alilimiliki kwa sababu aliishi pale kwa muda mrefu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…