barafu
JF-Expert Member
- Apr 28, 2013
- 6,726
- 32,818
Kanisa Katoliki Tanzania Bara litaadhimisha Miaka 150 tangu Ukristo Ukatoliki uingie Tanzania bara kupitia Mji mkongwe wa Bagamoyo,na pia wataashimisha miaka 100 toka Kanisa Katoliki la Tanzania Bara kupata Padre wa Kwanza Mzalendo(Mtanzania)
Mapadre hawa walitoka katika Maeneo ya kanda ya Ziwa ambapo ni Geita,Bunda na Bukoba na wote walisoma na kulelewa ktk Seminary Ndogo ya Rubya iliyoko Jimbo La Bukoba.Hii ni kusema kuwa Bukoba ndio inajenga Historia ya Uinjilishaji wa kiroho ktk kanisa katoliki,kwanza kwa kuwa na Mapadre wa kwanza wazalendo na pia kwa kuwa na Cardinal wa Kwanza Mwafrika na kutoka Africa Muadhama Rugambwa.
Adhimisho hili linapa picha kuwa,kumbe Ukristo Ukatoliki Tanzania Bara hauna zaidi ya miaka 150...Ukilinganisha na Uislamu.Na maswali ya kujiuliza ni kuwa kwanini Ukristo ulichelewa sana kufika Afrika na Tanzania kaa ujumla na kuacha Uislam uliofika karibu miaka 500 na zaidi nyuma?
Mwaka 2012 Shirika la Roho Mtalatifu(Holy Ghost Fathers) barani Afrika,walikutana Bagamoyo Tanzania...mahali ambapo ulikuwa "mlango" wao wa kuingilia Afrika...Na hiki ndicho walichoandika
.
Maadhimisho ya Mkutano mkuu wa Shirika la Roho Mtakatifu katika Mji Mkongwe wa Bagamoyo ni tukio la kihistoria, linalotupania nafasi ya kukumbuka kwa mara nyingine tena, historia ya mchakato wa Uinjilishaji Afrika Mashariki. Katika makala zilizotangulia, Mheshimiwa Padre Philipo Massawe amebainisha vigezo na masharti yaliyopelekea hata Shirika la Roho Mtakatifu likaamua kuadhimisha Mkutano wake mkuu Bagamoyo kwa mwaka 2012.
Ametumegea kwa kina changamoto na vuguvugu la Uinjilishaji Zanzibar na Tanganyika kwa wakati ule. Leo anatuvusha mabonde na milima hadi nchini Kenya. Itakumbukwa kwamba, Bagamoyo ni chimbuko la Ukristo Afrika Mashariki.
Wamisionari hawa hawakubaki tu Tanganyika, bali pia waliingia Kenya. Kati ya mwaka 1889-1899 walianza Mombasa na sehemua za Pwani Malindi, na baadaye walikwenda Bura, Taita, Mto Tana, Machakos na mwishowe wakafika Nairobi. Hoja tunayojenga hapa siyo kuandika historia, ila ni kuonyesha sifa mojawapo inayofanya Mkutano Mkuu wa Shirika pawe ni sehemu ambayo kuna alama muhimu au makini. Kwa hii historia fupi, Bagamoyo imekuja kuwa ni Mama wa Makanisa Katoliki siyo tu kwa Tanzania bali kwa Afrika ya Mashariki.
Uamuzi wa kufanya Mkutano Mkuu wa Shirika Bagamoyo kunatupa nafasi ya kipekee kabisa kuwaenzi kwa heshima kubwa wale wamisionari wa kwanza wa Shirika. Katika utamaduni wetu wa Kiafrika hii ina maana kubwa sana kwetu. Tunasema tunaleta Shirika lote pale mahali ambapo Kanisa la Afrika ya Mashariki na ya Kati lilipozaliwa. Kitendo hiki kina maana kwamba kwamwe hatutawasahau hawa waanzilishi kwani kufanya hivyo ni kinyume na utamaduni wetu, na ukristu wetu. Tunaungama kwenye Kanuni ya Imani kwamba tunaamini katika ushirika wa watakatifu.
Kwetu sisi wanashirika na kwa wakristu wa sehemu hii ya Afrika, hawa ni mababu zetu ambao walitoa maisha yao kwa ajili ya bara letu na hasa sehemu hii ya Afrika, walijitosa kwa moyo mmoja na kwa nguvu zao zote. Kikubwa kwao kilikuwa ni HUDUMA, KUJITOLEA kabisa bila ya kujibakiza hata chembe (total dedication), kwa kuwa walisukumwa na upendo wa Kristo, aliyekufa kwa ajili yetu wote pale Msalabani.
Wao walitoa maisha yao wakifuata mfano wa Yesu mwenyewe. Maisha yao ni mfano wa imani isiyotikisika kama Yesu anavyotueleza kwenye Injili kwamba imani inaweza kusukuma milima. Imani na matumaini yao kwa Mungu haina mpaka. Walitii ile amri ya Yesu: “Enendeni duniani kote mkawafanye mataifa yote kuwa wafuasi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na la Mwana na la Roho Mtakatifu. Nanyi wafundisheni kuyashika mambo yote niliyowaamuru ninyi (Mt 28:
19).
Katika utume wao wakimisionari walikuwa na ari kama ile ya Mtakatifu Paulo ambaye tumaini lake lilikuwa “ili watu wa Mataifa wapate kuwa dhabihu inayokubaliwa na Mungu, iliyotakaswa na Roho Mtakatifu (Warumi 15:16). Tunaenda Bagamoyo kukumbuka utume wao, mateso yao, kujitoleo kwao, walikufa wakiwa vijana wadogo kabisa katika ubichi wao, na jinsi walivyotoa maisha yao kwa ajili ya kutangaza Habari Njema ya Kristo Afrika ya Mashariki.
Kama Biblia inavyotuasa, “Wakumbukeni viongozi wenu wale waliowaambia Neno la Mungu. Angalieni mwenendo wa maisha yao mkaiige imani yao.” (Waebrania 13:7). Hakuna njia iliyobora zaidi kwetu sisi isipokuwa kufuata mfano wa maisha yao ya kujitoa na kujitolea kwa watu katika utume hasa wale walio maskini na katika utumwa wa aina mbali mbali, kuiga mfano wa imani yao na kuwa na moyo wa kimisionari na wa kijasiri.
Kanda ya Tanzania inasema karibuni sana Bagamoyo mwaka wa 2012 kusheherekea kwa pamoja Mkutano Mkuu wa Kwanza wa Shirika la Roho Mtakatifu utakaofanyika kwa mara ya kwanza barani Afrika, bara ambalo ni kipenzi cha mwanzilishi wa Shirika letu Padre Fransisko Maria Pauli Libernmann. Huyu ambaye tunamwita mwanzilishi wetu wa pili wa Shirika alisema, “Moyo wangu upo Afrika, Moyo wangu upo na waafrika"
Ndi kusema,ni kweli kuwa Ukristo ilikuwa ni njia ya kueneza ukoloni na ndio maana ulikuja Tanzania Bara mara tu baada ya Makoloni kugawanywa?
Mapadre hawa walitoka katika Maeneo ya kanda ya Ziwa ambapo ni Geita,Bunda na Bukoba na wote walisoma na kulelewa ktk Seminary Ndogo ya Rubya iliyoko Jimbo La Bukoba.Hii ni kusema kuwa Bukoba ndio inajenga Historia ya Uinjilishaji wa kiroho ktk kanisa katoliki,kwanza kwa kuwa na Mapadre wa kwanza wazalendo na pia kwa kuwa na Cardinal wa Kwanza Mwafrika na kutoka Africa Muadhama Rugambwa.
Adhimisho hili linapa picha kuwa,kumbe Ukristo Ukatoliki Tanzania Bara hauna zaidi ya miaka 150...Ukilinganisha na Uislamu.Na maswali ya kujiuliza ni kuwa kwanini Ukristo ulichelewa sana kufika Afrika na Tanzania kaa ujumla na kuacha Uislam uliofika karibu miaka 500 na zaidi nyuma?
Mwaka 2012 Shirika la Roho Mtalatifu(Holy Ghost Fathers) barani Afrika,walikutana Bagamoyo Tanzania...mahali ambapo ulikuwa "mlango" wao wa kuingilia Afrika...Na hiki ndicho walichoandika
.
Maadhimisho ya Mkutano mkuu wa Shirika la Roho Mtakatifu katika Mji Mkongwe wa Bagamoyo ni tukio la kihistoria, linalotupania nafasi ya kukumbuka kwa mara nyingine tena, historia ya mchakato wa Uinjilishaji Afrika Mashariki. Katika makala zilizotangulia, Mheshimiwa Padre Philipo Massawe amebainisha vigezo na masharti yaliyopelekea hata Shirika la Roho Mtakatifu likaamua kuadhimisha Mkutano wake mkuu Bagamoyo kwa mwaka 2012.
Ametumegea kwa kina changamoto na vuguvugu la Uinjilishaji Zanzibar na Tanganyika kwa wakati ule. Leo anatuvusha mabonde na milima hadi nchini Kenya. Itakumbukwa kwamba, Bagamoyo ni chimbuko la Ukristo Afrika Mashariki.
Wamisionari hawa hawakubaki tu Tanganyika, bali pia waliingia Kenya. Kati ya mwaka 1889-1899 walianza Mombasa na sehemua za Pwani Malindi, na baadaye walikwenda Bura, Taita, Mto Tana, Machakos na mwishowe wakafika Nairobi. Hoja tunayojenga hapa siyo kuandika historia, ila ni kuonyesha sifa mojawapo inayofanya Mkutano Mkuu wa Shirika pawe ni sehemu ambayo kuna alama muhimu au makini. Kwa hii historia fupi, Bagamoyo imekuja kuwa ni Mama wa Makanisa Katoliki siyo tu kwa Tanzania bali kwa Afrika ya Mashariki.
Uamuzi wa kufanya Mkutano Mkuu wa Shirika Bagamoyo kunatupa nafasi ya kipekee kabisa kuwaenzi kwa heshima kubwa wale wamisionari wa kwanza wa Shirika. Katika utamaduni wetu wa Kiafrika hii ina maana kubwa sana kwetu. Tunasema tunaleta Shirika lote pale mahali ambapo Kanisa la Afrika ya Mashariki na ya Kati lilipozaliwa. Kitendo hiki kina maana kwamba kwamwe hatutawasahau hawa waanzilishi kwani kufanya hivyo ni kinyume na utamaduni wetu, na ukristu wetu. Tunaungama kwenye Kanuni ya Imani kwamba tunaamini katika ushirika wa watakatifu.
Kwetu sisi wanashirika na kwa wakristu wa sehemu hii ya Afrika, hawa ni mababu zetu ambao walitoa maisha yao kwa ajili ya bara letu na hasa sehemu hii ya Afrika, walijitosa kwa moyo mmoja na kwa nguvu zao zote. Kikubwa kwao kilikuwa ni HUDUMA, KUJITOLEA kabisa bila ya kujibakiza hata chembe (total dedication), kwa kuwa walisukumwa na upendo wa Kristo, aliyekufa kwa ajili yetu wote pale Msalabani.
Wao walitoa maisha yao wakifuata mfano wa Yesu mwenyewe. Maisha yao ni mfano wa imani isiyotikisika kama Yesu anavyotueleza kwenye Injili kwamba imani inaweza kusukuma milima. Imani na matumaini yao kwa Mungu haina mpaka. Walitii ile amri ya Yesu: “Enendeni duniani kote mkawafanye mataifa yote kuwa wafuasi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na la Mwana na la Roho Mtakatifu. Nanyi wafundisheni kuyashika mambo yote niliyowaamuru ninyi (Mt 28:
Katika utume wao wakimisionari walikuwa na ari kama ile ya Mtakatifu Paulo ambaye tumaini lake lilikuwa “ili watu wa Mataifa wapate kuwa dhabihu inayokubaliwa na Mungu, iliyotakaswa na Roho Mtakatifu (Warumi 15:16). Tunaenda Bagamoyo kukumbuka utume wao, mateso yao, kujitoleo kwao, walikufa wakiwa vijana wadogo kabisa katika ubichi wao, na jinsi walivyotoa maisha yao kwa ajili ya kutangaza Habari Njema ya Kristo Afrika ya Mashariki.
Kama Biblia inavyotuasa, “Wakumbukeni viongozi wenu wale waliowaambia Neno la Mungu. Angalieni mwenendo wa maisha yao mkaiige imani yao.” (Waebrania 13:7). Hakuna njia iliyobora zaidi kwetu sisi isipokuwa kufuata mfano wa maisha yao ya kujitoa na kujitolea kwa watu katika utume hasa wale walio maskini na katika utumwa wa aina mbali mbali, kuiga mfano wa imani yao na kuwa na moyo wa kimisionari na wa kijasiri.
Kanda ya Tanzania inasema karibuni sana Bagamoyo mwaka wa 2012 kusheherekea kwa pamoja Mkutano Mkuu wa Kwanza wa Shirika la Roho Mtakatifu utakaofanyika kwa mara ya kwanza barani Afrika, bara ambalo ni kipenzi cha mwanzilishi wa Shirika letu Padre Fransisko Maria Pauli Libernmann. Huyu ambaye tunamwita mwanzilishi wetu wa pili wa Shirika alisema, “Moyo wangu upo Afrika, Moyo wangu upo na waafrika"
Ndi kusema,ni kweli kuwa Ukristo ilikuwa ni njia ya kueneza ukoloni na ndio maana ulikuja Tanzania Bara mara tu baada ya Makoloni kugawanywa?