Kumbe CCM napo kuna makundi??? 2015 is near the corner let's wait and see manake Lowassa want to lead the country, membe the same, Kanda ya ziwa tumewasikia wameanza mchakato!! This country is heading highway to the grave!!
measkron,
Hapo kwenye nyekundu hapo. You're very right. The country is leading straight away to its own grave!!!
Ni dhahiri nchi hii hapa tulipofikia imeshapoteza mwelekeo kwa kukosa UONGOZI BORA na SIASA SAFI kama alivowahi kusema Baba wa Taifa hili Mwl.J.K. Nyerere(RIP).
Unashangaa kuona kwamba kwa sasa kuna mnyukano wa chichini wa watu kutaka kwenda Ikulu na ilhali hawana SIFA hata kidogo za kukaa Jumba hilo takatifu!! Mtu kama Edward Lowasa,Bernad Membe, Emmanuel Nchimbi(aliyetimuliwa Uwaziri juzi),Januari Makamba, Rose Migiro na wengineo hawana sifa kabisa za kukalia kiti cha Ikulu!!!
Lakini kwa vile nchi hii inaendeshwa na Mafisadi ndiyo maana watu wanakimbilia Ikulu ili wakaendelee kufanya Ufisadi wao kwa uhakika zaidi, bila woga wala hofu! Hivi kweli itakuwaje Rais akiwa mtu kama Lowassa( Mzee wa Richmond)?Mtu aliyejiuzulu Uwaziri Mkuu kwa tuhuma za Ufisadi leo anaomba arudi Ikulu, akafanye nini? Kama u-PM ulimshinda ataweza kuvaa viatu vya Urais kweli??? No way!
Mtu kama Nchimbi hana sifa hata moja. Hapo tu kwenye Uwaziri amechemka halafu ati mtu ana ndoto za kuingia Ikulu?? Labda Ikulu ya Mafisadi na Walevi wa Madaraka! Njoo kwa Bwana mdogo Januari Makamba, sijui anapata wapi ushawoshi huu wa kutka kuingia Ikulu, bila shaka ni kwa baba yake Mzee Yusufu Makamba, kwa mtindo uleule wa wa Usultani. Kwamba kwa vile baba alikuwa Kiongozi mkuu wa CCM basi hiyo ni tiketi ya kwenda Ikulu!!! Nonsense!
Hivi Makamba Januari anafikiri kuwa Rais ni sawa na kuwa Mbunge? Kwamba unapigiwa kura unapata ushindi wa kishindo halafu unaenda kwenye mjengo wa Bunge halafu unaishia KULALA usingizi na KUUNGA HOJA KWA 100% hata kama hoja yenyewe ni uharo???Nafikiri Makamba hajui maana ya kuwa Rais wa nchi! Tunajua alikuwa mwandishi wa Hotuba za Rais Kiwete sasa anafikiri kwa mtaji huo anaweza kuwa Rais.....hakika ni kichekesho!!
Acha tusuburi hiyo 2015 nani ataingia Ikulu kama CCM watafanikiwa kuihujumu CHADEMA kwa mara nyingine. Time gonna tell.