Mkuu
Ngokongosha, japo siungi mkono aina yoyote ya ubaguzi, uwe wa kidini, jisia, ukabila, ukanda, rangi, kipato ahata umri, etc, na wengi watakuona wewe ni mbaguzi, sisi waumini wa ukweli halisi jinsi vile ulivyo, tumekuelewa!.
Tukubali tukatae, kuna udini mkubwa kwenye siasa zetu!, huu ni ubaguzi!, namna ya kuufuta sio kuunyamazia, bali kuuzungumzia wazi wazi kinaga ubaga, na ikibidi kuuzuia kwa makusudi kabisa!. Kuna watu wanadhani jina la Magufuli limeingia kwa bahati mbaya tuu!. Kuna vitu kuna watu waliviangalaia na waliisha amua kabla, hivyo wakaamua 2015 ni Magufuli. Bahati nzuri mimi ni mmoja wa watu tuliodokezwa kuhusu Magufuli, na niliwaeleza watu humu
Mgombea wa Urais Kwa tiketi ya CCM, 2015 "Could Be" John Pombe Magufuli!. kuna sababu zilitolewa why ni Magufuli!.
Nimefurahi ulipozungumzia kukubalika kwa Magufuli kama John Pombe Magufuli na sio eti kwa sababu anatoka Kanda ya Ziwa, kwa sababu ingekuwa watu wa Kanda ya Ziwa wanaukabila kihivyo, wangemchagua Cheyo kwa sababu amewahi kugombea urais!!, kitu ambacho ni ukweli kabisa Magufuli anakubalika kwa sababu ni Jembe la ukweli!.
Kule nyuma sii mara moja wala mbili, nimewahi kuuliza humu kuhusu mambo haya haya ya ukabila, udini na ukanda, nikaishia kunyooshewa vidole kuitwa mbaguzi, lakini huu ndio ukweli wenyewe, watu makini wanaoijua sayansi ya siasa, hili wanalijua ndio maana wakaja na jina la John Pombe Magufuli.
Kanda ya Ziwa ndio determinant ya nani anakuwa rais wa nchi hii, kitendo cha CCM kumteua Magufuli, kitapelekea mgombea wa CCM sio tuu kupata ushindi wa kishindo cha ajabu, bali pia atayarejesha CCM, yale majimbo yote ya kanda ya Ziwa yaliyoshikwa na Wapinzani!.
Mimi kwa sababu siku zote ni muumini wa ukweli jinsi ile ile ulivyo, sipati taabu kuitwa mbaguzi kwa kuusema ukweli, wale unaopenda kuujua ukweli huu ninaozungumzia hapa, mnaweza kupitia nyuzi zangu hizi.
Mtazamo: Kanda ya Kaskazini, CCM imechokwa mpaka basi!
Sumu ya Siasa za Udini, Ukanda na Ukabila, "Is It Real?
Tupende, tusipende: Tanzania inanyemelewa na udini!
Kete ya Dhana ya 'Zamu za Kupokezana' ina turufu yoyote katika Siasa za Tanzania?!.
Pasco.