Kanda ya ziwa na watanzani wote, nawasalimu kwa jina la upendo

Criterion

JF-Expert Member
Jan 8, 2008
11,798
11,881
Niliambiwa kwamba Kanda ya ziwa wanafanya sherehe na mikesha wakishangiliwa bahati nasibu aliyoipata Magufuli wakati wakubwa wanagombania maslahi.

Inanipa shida kuelewa hawa ndugu zangu kama pamoja na ongezeko la upashanaji habari ambao ulikuwa unatosha kuwapa taarifa nyingi na sahihi juu ya matukio ya watendaji na mifumo ya uongozi nchini.

Watanzania wakiwemo kanda ya ziwa, wamkuwa katika dimbwi la kilio kikuu kwa miaka mingi wakilia mateso, manyanyasho. rushwa, maisha magumu, kukosa huduma, vifo vya kulazimishiwa, uonevu, kuminywa kwa haki, kudharirishwa wanapohhitaji huduma kama vile tanesco, n.k, halafu wanaambiwa hayo mateso ni uongozi mbovu na mfumo wa utawala usiofaa, wanaelekezwa na njia sahihi.

Wanaposhindwa kuamka na kupita katika njia sahihi, wanadanganyika na shilling 5,000/= ili auze kadi yake ya kupigia kura, anaalikwa kula pilau kwenye sherehe za mafisadi, anapewa khanga na mara nyingine kupiga picha ame pause na mafisadi, tayari anasahau kwamba hao mafirauni wamempa dhiki maisha yake yote, anaendelea kukenua meno na kuyashangilia, anadiriki hata kushinda mtandaoni akiyapepelea, ni zaidi ya wendawazimu. Watafiti fanyeni kufuatilia ili mje muone Tanzania ina vichaa wangapi kwa kutumia kura zitakazopigwa kuiunga mkono ccm!.

Ukiona mtu anaunga mkono mgombea kwa sababu ni kabila lake au wanatoka kanda moja, huyo mtu ni zaidi ya marehmu asiye na fahamu. Kabila linakusaidiaje wewe kutatua matatizo ambayo umekuwa ukilia lia nayo?

Kabila la mgombea litafufua viwanda, kutengeneza ajira na kupandisha kiwango chako cha elimu ili usome, upate sifa za kufanya kazi bora na uajiriwe?

Kuwa kabila moja au kutoka kanda moja na mgombea, kunapunguzaje mfumuko wa bei na kuongeza nguvu ya shilingi ili uweze kumudu maisha kwa kipato chako?

Kuwa kabila moja au kutoka eneo moja na mgombea, kunaongezaje upatikanaji na ubora wa kiwango cha huduma katika ofisi za umma ili ukihitaji huduma za umeme, afya, elimu, masoko, ushauri wa kitaalamu, maji, polisi na usalama, mahakama, upate huduma za kiwango sahihi kwa muda sahihi na gharama halisi???

Kuwa kabila moja na kutoka kanda moja na mgombea, kunaondoaje rushwa na unyanyasaji wa raia?

Huyo mgombea atatembeza migao ya madakitari, polisi, mahakimu, walimu, shule namitaala yake, masoko ya bidhaa, ajira na kila hitaji bora kwa watu wa kabila lake au wa kandaanayotoka ambao hawatakuwa wakifanya kwa viwango tofauti na wale wa kwingine??

Unapoangalia kabila ama ukanda, ukitegemea favoritism, na nepotism, ni kweli huyo mgombea wenu atawaweza kuwabeba kabila lake na kanda yake yote bado Tanzania ibaki kuwa taifa moja? Kama mgombea wenu anasifa hizo, na ninyi mnashabikia kwa sabbu mnategemea upendeleo, je bado anasifa za kuliongoza taifa??

Na kwa kuwa mnamfahamu vizuri basi bila shaka taifa lione kwamba mgombea huyo ni bingwa wa ubaguzi na upendeleo kwamba nje ya watu wa kwao, wengine wategemee makombo yatakayosalia, kitu ambacho sikubaliani nacho.

Ninaomba Watanzania tusiendelee kuumizwa na mitazamo ya udini, ukabila, ukanda. Tuchague kiongozi mwenye sifa sahihi, uwezo wa kiwango na awe katika mfumo utakaomsaidia ama kumsukuma kutenda mema na haki kwa Watanzania. Kinyume cha paleni patapotea na tutatakiwa tuhesabiwe ni wafu zaidi ya marehemu. Kama tunajihesabu tuko hai, tuangalie madonda yetu anayovuja damu bado ambayo JK ametusababishia kwa favoritism na nepotism ambazo amekuwa akizifanya wazi wazi, maksudi bila haya wala hisia.


Kumchagua Magufuli kwa sababu ya kutoka naye kanda moja ama kabila moja, haikuondoeli dhiki zako kwa sababu hata kama angetamani lakini uwezo huo hana. Magufuli ni mwana cccm kama walivyo wana ccm wengine.

Hata kama Magufuli mnamwona ni mwema kama malaika wa nuru, lakini kumbukeni hataweza kuwatatutuli shida zenu nyumba kwa nyumba na hivyo mtasherehekea na kuendelea na mateso yenu na watoto wenu.

Magufuli hata atakapokuwa raisi, hatakuwa na uhuru wala uwezo wa kufanya lolote alitakalo kama CCM haijaridhia. Kumbuka amesema yeye atafuata Ccm kwanza, mengine baadaye. Ccm ndiyo iliyowaumiza na imewekeza kwenye mateso yenu milele. Fungukeni macho.

Magufuli kama Magufuli hana uwezo wa kuumba watu wa kufanya nao kazi. Ni lazima aunde srikali kwa kuwa na mawaziri hao hao mafisadi wwenye kiapo cha kulinda ufirauni kwa gharama yoyote kwa kuwa ni wanufaika. Hayo madabiliko anayfanya kwa kutumia watu gani? Kiapo chake ni KULINDA MASLAHI YA CCM KWANZA.

Ccm hao hao ambao mmewaona wakifisadi fedha zenu kwa mikataba fake, wizi mbali mbali na kisha kuteteana na kulindana ndiyo watakaokuwa wakimpa mwongozo wa namna gani afanye.

Hao hao waliokataa maoni ya Watanzania kwenye katiba na kuichakachua hadharani, ndio hayo hayo atatakiwa afanye kazi nao kwa maslahi ya ccm taifa baadaye.

Magufuli huyo ni mtii na mfuatiliaji wa kuhakikisha maagizo anayoagizwa anayatimiza kwa gharama yoyote. Itakuwaje pale atakaposimama na fimbo ya chuma, hataki mijadala wala kuhojiwa juu ya kuhakikisha anatekeleza sera za "Udini wa Cccm?, Migawanyo na matabaka kwa Watanzania,? Ulinzi wa mafisadi? Kuchakachua ellimu ili na kundi fulani ambalo halikuwa na elimu waonekane wengi wamesoma? Kulindana na kuhakikisha mikataba fake iliyokwisha kusainiwa na HIZI SHERIA MUMIANI ZA JUZI ZINATEKELEZWA BILA N AFASI YA KUFANYIWA REVIEW WALA KUHOJIWA?

Magufuli hawezi kusaliti itikadi za chama chake, na hilo ndilo kalisema. Labda niwaulize maswali:-

Nil siku gani Magufuli alisimama bungeni kama mbunge akajitenga na maamuzi ya hovyo yaonevu wa raia na kukumbutia maslahi ya mafisadi?

Magufurli akiwa Mbunge, alikuwa upande gani wkati wa kuchakachua rasimu ya katiba ya Warioba?

Juzi wakati miswada ya wizi inapitishwa, magufuli alisimama upande gani kuonyesha anajali taifa zaidi ya ccm?



Mnaoshangilishwa, naomba kila mmoja afumbe macho, awakumbuke ndugu zake waliopoteza maisha kwa sababu ya umasikini na kukosa huduma bora za afya kwa sababu ya ccm, wakumbuke wagonjwa wanaoishi kwa mitishamba na wale wanaosubiri kufa kwa sababu hawawezi kwenda india kutibiwa? Wakumbuke Wazazi wako wanaoishi katika umaskini kwa sababu wamejitoka kukusomesha kwa gharama kubwa halafu umemaliza shule huna ajira na huzuni mnayoipata wewe na wazazi wako.
wafikirie yatima wanaoishi mitaani, wanavyoongezeka kila siku kwa kuachwa na wazazi wao bila mpango wowote wa kuwapatia elimu ili waishi kama watoto wengine. Watoto wako wewe utakapokufa ghafula , serikali ya cc itawasaidia licha ya kodi kubwa unayolipa leo?

Fikiria wakulima wanavyohangaika na kilimo duni, wanashinda juani, nguo zimechanika, wamekuwa weusi ajili ya jua, macho yamekuwa mekundu, hawana hata ufahamu wala hawajui kuna kupumzika, wanalima kwa nnguvu na gharama kubwa, halafu wanapovuna hakuna soko la uhakika la bidhaa zao. Wanaletewa watu wa kuwakopa kwa bei iliyochini zaidi ya gharama walizotumia. Michango inaongezeka mara mlinzi wa shule, mara ujenzi wa nini mara nini, wakishindwa wanakamatwa, wanapigwa, wanafungiwa ofisini, wengine wanahamia porini ili wajiepushe na mateso kwa sababu hakuna anayeweza kujali na kuelewa shida zao. Wengine wameliwa na wanyama na kpoteza maisha katika kukimbia huko.

Wakumbuke Watanzania wanaopoteza haki zao kwa uonevu na kushamiri kwa rushwa. Wakienda polisi hawana rushwa wanaishia kubambikizwa kesi na wengine wameawa mikononi mwa polisi na serikali ya cccm imenyamaza kimya kuonyesha hizo ndizo sera zake.

Mfikirie alilyekwenda mahakamani huku haki zake zikiwa peupe lakini akaishia kutiwa hatiani kwa mfumo mbovu na upindishaji wa sheria. kumbuka familia za watu wamskini wasiokuwa na matumaini waliofukuzwa maeneo ya migodo wakamilikishwa wageni. Wanauawa kila siku na serikali ya ccm inasimama upande wa wageni na kuwaacha waTanzania maskini wakiishi kama wanyama katika ardhi ya nchi yao.

Yako mengi ya kusema., lakini kwa haya machache, naomba mtafakari na kisha muamuae kuendelea kusherehekea kuchaguliwa kwa Magufuli ili mradi ni mtu wa kwenu, huku mkijua mnashangilia mateso ya ndugu zenu na vizazi vyenu? Au mtaamua maamuzi sahihi ya kujiokoa ninyi, ndugu zenu na taifa zima kutoka katika mitego ya ibilisi ccm ambaye huja kama kondoo lakini ni mbwa mwitu mkali.

Mkifika hapa, najua hamtahadaika na kabila wala ukanda. Ccm na watu wake ni wale wale, na kuwashangilia nikushangilia mateso ya mauti zetu, ndugu zetu na watoto wetu.

Mwenye sikio na alisikie neno hili ambalo Tabby awaambia Kanda ya ziwa na Watanzania wote!.
 
* Magufuli hawezi kuondoa mfumo dhaifu na mbovu wa CCM, ataitumikia kama ambavyo wameitumikia wenzake...

* Nguruwe mwenye lipstick mdomoni bado anabaki kuwa nguruwe..kada wa CCM hawezi kutofautiana na itikadi na imani ya CCM....kulindana na kuendelea kuitafuna nchi...

* Tatizo watu wanashindwa kuona mfanano wa Kikwete na Magufuli na Mkapa ikiwa Magufuli atakuwa Rais...tutaendelea kupitwa na nchi nyingi duniani...Maendeleo makubwa tutababaki kuyasikia nchi za wenzetu...mwendo wa CCM hautufai kwenye karne hii ya 21...hatuhitaji ari, nguvu na kasi feki kama za Kikwete...

* Kikwete kamchagulia Magufuli mgombea mwenza ili kuendelea kulinda maslahi ya makundi flani...hamna Rais mdini duniani kama Kikwete...amewabeba sana dini yake kwenye utawala wake...badala ta kufikiria kila siku jinsi ya kutatua umaskini yeye alitumia mda wake kuweka watu wa dini yake kwenye mfumo...ndiyo maana hakuweza kujua kwanini Tanzania ni maskini....

* Watanzania tuwape fursa wapinzani...wamepiga kelele sana ni zamu yao kutenda...CCM wanaopenda kuhamasishwa na upinzani hawahamasishiki, wanachukia upinzani na hawafikiri kuwa maslahi makubwa ya Taifa ni muhimu kuliko ya chama...
 
Hv ndugu umefikilia vzr kweli kabla ya kuandika??ni kweli chama na watu wenye ukanda nchi hii huwajui?toka lini kanda ya ziwa kukawa na ukanda juu ya siasa,tena huku kanda ya ziwa mbona kuna kundi la wanachadema na wana nguvu sana tu,huku usukumani kungekua na ukanda rafiki pangekua hapatoshi nchi hii,mikoa mitano inayokaliwa na wasukuma labda kungeitwa United State of Sukuma kuanzia pale Igunga mpakani na Singida kwa maana ya Tabora kuja Shinyanga,Mwanza,Simiyu na Geita ila huku hakuna tabia ya kikaskazini,sote ni ndugu moja na uludie kufanya uchunguzi wako vyema,sipo kukuclash usemacho ila tambua huku hakuna ukanda hata kidogo
 
Mkuu ninashukuru kwa taarifa hii. Umeandika kwa huzuni sana nami najisikia vibaya kukuumiza.

Ila ninaomba uangalie mstari wangu wa kwanza. Nimesema nimeambiwa wanasherehekea. Nikaona ndugu zangu wanataka kuvalishwa upofu na ganzi ya muda wasijitambue hatimaye wafanye maamuzi yasiyo sahihi. Na hivyo nikaona niwape tahadhari.

Kama hakuna hicho kitu, ninamshukuru Mungu ili tuendelee kuitafuta Tanzania tuliyoipoteza kwa ulaghai na ufirauni wa ccm.

Ila tuendelee kuwatahadharisha wenye mawazo kama yale.


Hv ndugu umefikilia vzr kweli kabla ya kuandika??ni kweli chama na watu wenye ukanda nchi hii huwajui?toka lini kanda ya ziwa kukawa na ukanda juu ya siasa,tena huku kanda ya ziwa mbona kuna kundi la wanachadema na wana nguvu sana tu,huku usukumani kungekua na ukanda rafiki pangekua hapatoshi nchi hii,mikoa mitano inayokaliwa na wasukuma labda kungeitwa United State of Sukuma kuanzia pale Igunga mpakani na Singida kwa maana ya Tabora kuja Shinyanga,Mwanza,Simiyu na Geita ila huku hakuna tabia ya kikaskazini,sote ni ndugu moja na uludie kufanya uchunguzi wako vyema,sipo kukuclash usemacho ila tambua huku hakuna ukanda hata kidogo
 
Haya mambo ya kanda ya ziwa yanahuzunisha sana.mara hii wamesahau shida zao zote.nikamuuliza mpuuzi mmoja aliyekuja na hoja kwamba "ubunge nitawapa chadema,ila urais Magufuli",nikamuuliza kwani tatizo ni Kikwete au CCM?akanijibu wote,nikamwuliza kama ni wote je Magufuli ni chama gani?yakamshinda.Kiukweli sisi tumelaaniwa
 
Umeongea sana kwa jaziba ila ni kwasababu hauelewi kwamba sifa moja kuu ya siasa ni dynamism na unpredictability ..kilichotokea na kinachotokea ndo sifa za siasa zenyewe. Ngoja nikuulize hivi, fanya utafiti ujiuluze ni mikoa gani hasa ilikuwa inamuunga sana mkono Lowassa na mpaka sahivi na tayari tunaambiwa wamechoma hata kadi, unahisi ni kwanini? jiulize ni kwanini watu wa CCM waliokuwa nyuma ya Lowassa wameamua kwenda Ukawa na kama Ukawa haipo unahisi watakwenda chama gani? ..hakuna asiyejua kwamba sahivi siasa za Tz zimeingiliwa na udini, ukanda na ukabila. Yawezekana wewe haukuwahi kuliona hilo japo unajiita mwanasisa mpaka lilipokugusa kwenye masrahi yako lakini kwa wachambuzi wa mambo hili lipo zaidi ya muongo sasa, na kwahiyo kama kanda ya ziwa wameamua kumkubali Magufuri kwasababu ni mwenzao mie sioni tatizo, sasa utawaambia wamchukie? umesahau kila mchuma janga hula na wa kwao????
 
Magufuli aje kutuambia je, zina million 156 daily capacity charge wataendelea kulipwa DOWANS/RICHMOND?

Je, wakulima na masikini wa Tanzania watandelea kunyonywa kupitia mafuta taa bei juu?

Je, Magufuli atuambie zile Million 700 ni za nini?

je mfupa alioushindwa mkapa, yeye atauweza?

Je, Pombe magufuli,,,, utalinda wazee waliofilisi nchi na maakiba yao USWISS?

Je Magufuli... Pesa za USWISS utarudisha..

Je waziri Wa ujenzi utamteua nani?

Waziri wa fedha ni Saada Mkuya tena

Je magufuli, shillingi yetu vipi
 
Imekuwa ni jadi sasa kwa Watanzania kuwa na tatizo la kusahau namna siasa za CCM zilivyo hapa nchini. Mwaka 2005 Rais wa sasa Kupitia C CM Kikwete alionekana kuwa chaguo sahihi na baadhi ya watu na viongozi wa kidini walisema alikuwa ni chaguo la Mungu!

Lakini utendaji wake na hasa katika kushughulikia matatizo ya wananchi ya moja kwa moja haukuwaridhisha wananchi wengi na baadhi wanasema kheri aondoke mapema. Leo naona amekuja Dr. Magufuli
ghafla Watanzania naona wamesahau taabu na suluba zilizosababishwa na uongozi wa chama kile kile cha CCM. Sasa watu wameanza tena kuweka matumaini ya ukombozi mpya wa kiuchumi na tofauti za kitabaka utakaoletwa na Dr.Magufuli.

Ni muhimu tukajiuliza ni njia zipi mpya ambazo Dr.Magufuli atatokea ambazo wenzake hawakuzipitia? Wakati wananchi tukiendelea kupigika ndani ya utawala wa CCM, Dr.Magufuli alikuwa ni sehemu ya uongozi uliotufikisha hapa. CCM ina sera ambazo kwa sasa wanahitaji mfumo mpya wa uongozi na lazima wajifunze wakiwa nje ya uongozi ndipo wanaweza kuelewa haya tunayoyazungumza.

Ni vema watanzania tukawa na fikra za kimapinduzi ili kifanya maamuzi magumu dhidi utawala wa kimazoea na kuingiza utawala wa kisasa unaojali mahitaji na mawazo ya wananchi wa hali ya chini kuliko ilivyo sasa!
 
Haya mambo ya kanda ya ziwa yanahuzunisha sana.mara hii wamesahau shida zao zote.nikamuuliza mpuuzi mmoja aliyekuja na hoja kwamba "ubunge nitawapa chadema,ila urais Magufuli",nikamuuliza kwani tatizo ni Kikwete au CCM?akanijibu wote,nikamwuliza kama ni wote je Magufuli ni chama gani?yakamshinda.Kiukweli sisi tumelaaniwa

Ngoja nikujibu mkuu, tatizo la sasa si CCM bali ni JK, nasema hivi kwasababu hata wana CCM wenyewe hawakuwa wanapenda mambo ya JK na ndo maana walikuwa wanaama daily na mifano iko mingi. Magufuri ni CCM, JK ni CCM na hata Ben ni CCM lakini wanatofautiana sana kiutendaji japo wote ni CCM. Na ndo maana hata Ben mwnyewe kwa kinywa chake anamdharau sana JK. Yawezekana Ben alikuwa na mapungufu yake lakini watanzania wengi wanamkubali Ben zaidi JK, unadhani kwanini wakati wote ni CCM? Tunajadiri uwezo wa marais wetu kwa uwezo wake na ladhaifu yake badala ya chama, katika hili focus yetu ni mtu badala ya chama as kila mtu ana mapungufu yake na mdo maana tunamtafuta rais wetu, hatumtafuti malaika wa Tz
 

KICKS OF A DYING HORSE!
Kuteuliwa kwa Magufuli kumeondoka na turufu nyingi za kisaikolojia walizotumia CDM uchaguzi wa 2010 kiasi cha kuwaacha wakiweweseka!
NA HII NI KWELI KABISA!
 
Ngoja nikujibu mkuu, tatizo la sasa si CCM bali ni JK, nasema hivi kwasababu hata wana CCM wenyewe hawakuwa wanapenda mambo ya JK na ndo maana walikuwa wanaama daily na mifano iko mingi. Magufuri ni CCM, JK ni CCM na hata Ben ni CCM lakini wanatofautiana sana kiutendaji japo wote ni CCM. Na ndo maana hata Ben mwnyewe kwa kinywa chake anamdharau sana JK. Yawezekana Ben alikuwa na mapungufu yake lakini watanzania wengi wanamkubali Ben zaidi JK, unadhani kwanini wakati wote ni CCM? Tunajadiri uwezo wa marais wetu kwa uwezo wake na ladhaifu yake badala ya chama, katika hili focus yetu ni mtu badala ya chama as kila mtu ana mapungufu yake na mdo maana tunamtafuta rais wetu, hatumtafuti malaika wa Tz

Wewe ndugu wacheni kuwalisha watu uGORO msidhani kila MTU ni POYOYOZ hakuna mwanaCCM atakaeweza kuiinua hii NCH kuchagua kishabiki MTU wa mwisho alikuwa KIKWETE tu nw tunataka kung'oa hadi kiota chao kinachoitwa CCM upuuzi uliofanyika kwenye Bunge la Katiba hakuna Mwana ccm yyt aliesimama upande wa Wananchi wote hao walisimama upande wa ccm nivipi Leo mdanganye watu kuwa wanafaa kututawala tena
 
Nimesoma kiduchu hii makala nimeshindwa kuimaliza hamna jipya ni drama tu za pro-Chadema.

Dr.Magufuli kaishamaliza huu uchaguzi.

Subirini tu Slaa aanze kulalamika kuwa Usalama wa Taifa wameiba kura.
 
Wakati kule state Jeb bush na donald trump wanamendea kura za walatin na wamexco,unaona lipi la ajabu mgombea fulani kupata uungwaji mkono toka kanda fulani,isiwe nongwa.
 
Huyu nae hana hoja,ww eleza mapunguf unayoyaona na kuhisi yataharibu utendaji kazi was Dr.J.P.J.M,usituletee sababu za ukanda na udini hapa, je tatizo ni yeye? Chama au ukanda anaotokea? Ni chama kipi kikubwa nchini hakina ukanda? By z way kama watu wa ukanda huo wanaona ndo mkomboz wao ww inakuuma nn?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom