Kanda maalum ya ushirikina

mbona pale makete watu wanahamisha mvua.
 
dar fisi wanafugwa for international export market, pale pugu kuna mtu anawafuga
 
Uchawi upo, kuna mzee mmoja nlikua naishi nae nyumba moja, ila Mimi ya uani yeye nyumba kubwa, sasa kila SKU alikua na tabia ya kutuwangia, basi usku nkamlia dolia usku was manane, kilichotokea mlangoni skukitegemea maanake nliskia mlango ukipiga Fujo sana ghafla chini nikaona Paka anatokeza duuuu hatari sana.
 
Soma habari za Osale Otango na wengine utajua nazungumzia nini
Wasalaaam kaka mkubwa. Imenibidi niseme kitu hapa.

Watu wanajidanganya sana kama huamini uchawi haukufiki. Hiii kitu hata si kweli,

UCHAWI HAUFANYI KAZI TU KAMA ANAYE FANYA HUO UCHAWI NDI HANA IMANI NA AFANYALO...Binadamu tunaongozwa na power na kulindwa na hizo hizo power huwezi kuwa haupo katika tawala yeyote na ukawa salama hata kidogo.

Hata wale ambao wapo kwenye tawala flan na hawati taratibu na protocals za tawala hiyo kwa ukamilifu , watapigwa vizuri tu. Hiwe ni tawala ya MUNGU au ya giza kama hufati taratibu zao utapigwa na adui wa tawala hiyo vizuri kabisa.

Tukija kwenye swala la wazungu. Hapa kuna myth nyingi sana. Kuwa hawa watu wapo very inocent kuwa hawashiriki wala hawajui hizi habari za uchawi. Nahisi ukisoma makala mbali mbali utagundua hawa jamaaa ndio wanafatilia hizi ishu kwa undani sana.

Hadi kufanya ocult na vitj vya namna hizo, mtafute na soma historia ya Aliester crowel utafunguka macho. Na hizi ishu zinaenda kwa kizazi na kizazi mfano Skull n bones imefanywa sana na kooo za kina BUSH hadi wameikuza sasa.

Tumezoea kuona ndumba na uchawi ni hadi mtu awe na hirizi kaniki , usinga etc na dhana za aina hiyo. Lakin kina watu wapo katika level za juuu za rohoni ufanya haya kwa matamshi maaana dhana zao zipo rohoni , miiili yao ni tempo na hekalu la GIZA muda wote.

Kuna ibad zinafanywa katika silaha, nguo na hata fedha watu wakiwa wanataka kwenda task , safari ngumu ya kijesh au hata kusimika utawala ili kupata matokeo wanayo taka, Check fedha za ujerumani zilivyokuwa na maagano na nguvu za giza.

Pale walipoona kuwa kuna mbabe anaweza wasumbua wanamnunua tu kwa kumpa uongozi au kumuongoza indirectly wana m_plz ili waende sawa.
............................
 
Mshana hebu siku moja utuletee uzi unaozungumzia maana ya rangi, hasa nyekundu,nyeusi na nyeupe katika ulimwengu wa ushirikina.Naona waganga wa kienyeji wanazitumia sana.Infact hata makampuni mengi makubwa.Kama ukiwa na muda tuletee pia uhusiano kati ya ushirikina na technologies. Naona tekinolojia zingine siku hizi ni ushirikina mtupu.
 
Mpeni heshima yake
Mheshimiwa Mshana Jr,

Elimu anayoitoa ni nadra kutolewa hadharani.
Kwa karne nyingi mifumo ya elimu rasmi na isiyo rasmi ilikuwa inatoa elimu ya upande mmoja
Elimu ya nadharia na vitendo ya Falsafa za jamii, ilikuwa inatolewa bila masharti.
Elimu ya kiroho ya upande wa Mungu Yehova, ilikuwa inatolewa hadharani kila mwenye kuihitaji aliipata bure kwenye nyumba za ibada.
Elimu ya kiroho upande wa Shetani ilikuwepo lakini ilikuwa inatolewa kwa Siri, ikiambatana na Masharti mazito, mikataba, viapo, nadhiri, maagano ya damu , kafara, kwa usiri, kificho, vitisho,woga,nk.
Unasikia tu mtu fulani kalogwa, fulani ni Mchawi, Anaagua, ana majini, mizimu.nk
Watu wanasafiri kwa ungo, Fisi, na mambo mengi, ambayo yanafundishwa kwa vificho ndo maana jumuiya hizo zinajiita Secret Societies.
Mshana Jr,
ameshaweka wazi kuwa yeye kwa shari au heri alibahatika kusoma huko South Afrika, na nchi nyingine nyingi hivyo kuwa mhitimu wa kiwango cha juu kabisa wa elimu ya imani za kiroho mbadala.
Mimi naielewa elimu hiyo inaitwa. "Science Beyond Material"
Mtu anasoma kuanzia chekechea hadi PHD.
Ndugu yetu Mshana Jr, yeye ana PHD zaidi ya moja ya maswala ya Elimu ya kiroho mbadala.
Elimu ya kiroho ya imani ya Kikristo pia anayo na ni Mlutheri mzuri tu.
Ndugu yetu huyo anajitahidi kutuelimisha kuhusu nini kilichopo kwenye elimu hiyo ya kiroho yaani mambo ya uchawi, Satanism, mizimu, Secret Societies nk, kwa lengo la kuwafahamu wenzetu huko ni nini wanakifanya na kwa malengo gani.
Hii ni baada ya kuokoka na kumpokea Yesu Kristo kuwa Bwana na Mwokozi wake.
Angalieni,
Wachawi na walozi kamwe hawatoi siri za falme zao.
Hili ni jambo la kwanza lamsingi katika imani
yao hiyo, na wanaapa.
Mshana Jr, anatupa elimu bure ya kutuwezesha kumtambua adui Shetani, nini anaamini, nini anafanya nini malengo yake na zaidi ni wapi anawanasa watu wa Mungu,
Mfano, somo la ndugu
Mshana Jr lililosema
"SHETANI. adui, rafiki asiye na kinyongo"
Lilitufundisha matumaini ya shetani kupata wafuasi na uvumilivu wake.
Mtu anakua na matatizo, anakimbilia kumwomba Mungu ambariki.
Akibarikiwa na kupata mali anakuwa mwovu kuliko mwanzo. hapo Shetani anamdaka ki ulaini kabisa.
Wengine wakipata mali wanaanza kuhalibu mwili wao kwa ulevi, uzinzi nk.
Ndo maana mkiomba baraka, Mungu anawanyima kwasababu mnaomba ili kutimiza tamaa za miili yenu na sio kwa kumtukuza Mungu. Ni bora mbakie kuwa maskini mnakuwa na nidhamu kwa Mungu wenu, kuliko kutajirika na kumkufuru.
Mungu anafahamu mioyo yetu ndo maana anatupa mali kutokana na mafanikio yetu ya kiroho kuweza kuhimili vishawishi vya utajiri wa mali.
Hivyo basi
Sisi tunao endelea kutafakari Falme za Mwanga na Giza tunaendelea kuelimika kwa masomo mbadala ya Ndugu yetu Mshana Jr
Ni mtu aliye jitolea kutupa elimu hiyo bure kabisa.
Narudia tena Mshana Jr ni mtu aliyejielimisha kwa viwango vya PHD.
Ni mtu anayestahili kuheshimika na jamii kwa mchango wake wa mawazo,
Si mchawi wala mlozi na ameokoka.
Taarifa hii ni yangu mimi baada ya kuchunguza kwa makini mawazo yake, sijawahi kumhoji wala kumwona wala hajawahi kuniambia jambo lolote
Ni tafakari yangu tu kwake jinsi nilivyo msoma, maana hata mimi ni msomi wa PHD.
Hivyo tunafahamiana kimawazo tu. yaani kwa kusoma maandiko unaweza kujua kiwango cha elimu ya Mwandishi.
Ndugu Mshana Jr. endelea kuelimisha jamii, tunahitaji kuelewa kwa mapana Elimu mbadala ya kiroho uliyobobea kwayo.
Samahani ndugu Mshana Jr, kwa kukuelezea bila ridhaa yako.

Che mittoga.
 
Kuna huyu mkuu kadai
 
Ndugu Jebs

Hebu tuandikie kwa kiswahili wazo lako ili wengi tupate kuelewa.
Pia utafiti wako usiegemee upande mmoja
Ukweli uliothibitishwa kisayansi ni kuwa wanadamu walioanza kujifunza mambo ya Mungu ndio walioanza kustarabika, yaani kuijua Elimu ya Sayansi ya Jamii na Falsafa

Kumbuka vyuo vikuu vya kwanza kabisa vilijengwa Mashariki ya kati yaani eneo la Misri hadi Israel hadi Saudi Arabia, ambako ndiko chimbuko la elimu hiyo unayojivunia na elimu ya kidini ambayo wewe unaonekana huijui
Nadhani unakikumbuka chuo kikuu cha El- Azar kilijengwa lini na wapi kama ni msomi wa kuwaandikia kiingereza wasomaji wa kiswahili
Kwa taarifa yako elimu ya dini ndiyo iliyokuwa ya kwanza kufundishwa na kujifunza kabla ya elimu yako hiyo ya kiingereza
Israeli ni taifa lililo endelea sana kiteknolojia kuliko huko ulikozaliwa, na falsafa imethibitisha kuwa Waisraeli walianza kufundishwa elimu ya dini kabla ya hiyo teknolojia ambayo nayo wewe huijui kwa kiwango cha Waisraeli.
Ukisoma Sheria utakuta somo la chanzo cha zote duniani. utafika mahali utasoma kuwa sheria za kwanza kabisa zilifudishwa katika taifa la Israeli,
Amri kumi za Musa ni Sheria za kale kabisa kabla ya chuo chako cha kiingereza kuanzishwa.
Ukisoma Falsafa utakutana na mwanafalsafa wa kale kabisa anaitwa Musa
Mtu anaporejea katika maandiko ya dini sio kwamba ameishiwa hoja au hekima au hajui marejeo ya kisayansi bali dini ni moja kati ya maandiko yanayorerejewa na wasomi na yanakubalika ki ada, na yanarejerewa na wasomi wa kiwango kikubwa kabisa wa Farsafa na sayansi ya jamii kama akina Socretes, Aristotor Karl Max, nk.
Msomi wa kiingereza.
 
Am humbled kwa moyo wa Unyenyekevu mkubwa [emoji120] [emoji120] [emoji120] [emoji779] [emoji779] [emoji779]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…