Papaa Gx
JF-Expert Member
- Oct 10, 2016
- 11,508
- 18,668
Habari zenu wadau.
Moja kwa moja twende kwenye mada husika. Nakusihii na kukushauri ewe uliepo huko mikoani usitamani wala kufikiria kuja Dar es Salaam. Jiji la Dar es Salaam kwa sasa limekuwa na kero nyingi sana zinazo fanya kuonekana kuwa chungu kwa wananchi.
Kero ziko nyingi ila binafsi ningependa kuzungumzia kero ya usafiri. Usafiri umekuwa ni shida sana katika jiji hili iwe asubuhi, mchana na jioni ndio tabu kweli kweli. Usafiri umekuwa shida sana kiasi kwamba ukienda katika vituo vya daladala kama vile Mbagala, Kariakoo, Banana, mawasiliano nakadhalika wananchi wamekuwa wakigombea usafiri.
Hii ni kero kubwa sana hasa kwa ndugu zetu walemavu, wazee wasiojiweza, wajawazito pamoja na mama wenye watoto wachanga. Kero hii pia imewaathiri kwa kiwango kikubwa wanafunzi, kundi hili limekuwa likichelewa kufika kwa wakati katika maeneo yao kero kubwa ikiwa ni usafiri.
Kwa hiyo kama unakuja Dar es Salaam ujue kuna kadhia ya usafiri.
Moja kwa moja twende kwenye mada husika. Nakusihii na kukushauri ewe uliepo huko mikoani usitamani wala kufikiria kuja Dar es Salaam. Jiji la Dar es Salaam kwa sasa limekuwa na kero nyingi sana zinazo fanya kuonekana kuwa chungu kwa wananchi.
Kero ziko nyingi ila binafsi ningependa kuzungumzia kero ya usafiri. Usafiri umekuwa ni shida sana katika jiji hili iwe asubuhi, mchana na jioni ndio tabu kweli kweli. Usafiri umekuwa shida sana kiasi kwamba ukienda katika vituo vya daladala kama vile Mbagala, Kariakoo, Banana, mawasiliano nakadhalika wananchi wamekuwa wakigombea usafiri.
Hii ni kero kubwa sana hasa kwa ndugu zetu walemavu, wazee wasiojiweza, wajawazito pamoja na mama wenye watoto wachanga. Kero hii pia imewaathiri kwa kiwango kikubwa wanafunzi, kundi hili limekuwa likichelewa kufika kwa wakati katika maeneo yao kero kubwa ikiwa ni usafiri.
Kwa hiyo kama unakuja Dar es Salaam ujue kuna kadhia ya usafiri.
