Kamwe usitamani kuja jiji la Dar es Salaam.!

Kamwe usitamani kuja jiji la Dar es Salaam.!

Wachina bhanaa wamefunga wee zile bembea usiku na mchana,alaf walivomaliza wakaanza kutest mitambo wao wenyewe

Daaah nilisogea mwenyewe kuchungulia zile bembea buku 3 kwa dakika Tatu, hapo nina watoto watatu so hapo hujakaa sawa LAKI imeisha na madogo bado wanatamani ukiwatoa ni vilio mweee.... sitaki tena kujipitisha hayo maeneo nikiwa na msafara.
 
Ni mtazamo wako tu, Hakuna sehemu nzuri yenye raha Ya kuishi Kama dar, Sema wewe umezoea ukifika dar unaenda kuishi mbagara, kivure, ukonga, na kwingneko kwenye sehemu ovyo ovyo kutokana na uwezo wako Lakini nikuambie kuwa Hakuna mahali Salama pa kuishi Kama dar, Hakuna sehemu yenye ulinzi Kama dar, Hakuna sehemu yenye starehe Kama dar, kila utakachokitafuta dar kipo tena Kwa beii Ya kutupwa mikoani kufuatiliana hadi kero dar ni sehemu nzuri mno ni jiji la mastarehe Ndugu hayo mengne Ya foleni uchafu basi kakae huko Kijijini kwenu kusiko kuwa na foleni uwe unallala saa moja unasindikizwa na milio Ya nyoka na ndege sisi tuachie tule raha
Hujakosea! Tena ukute hyu ndyo walee...waga hawakui hata nguo za ndani hawanunui. mtoto wa mama, kula kwa mama, kulala kwa mama,kuishi kwa mama, kuvaa kwa mama, duuh!!

Wanakera!
 
Baadhi ya kero za jiji la Dar
1. Makanisa yasiyo na mpangilio maalum yakiambatana na kelele za nyimbo za dini na mapambio.

2. Wingi wa bajaji zisizokuwa na mpangilio maalum wa vituo, zinaendeshwa hovyo/ kihuni/ kihatari na zina makelele ya midundo ya muziki kama ukumbi wa disko.

3. Boda boda. Hapa ndio balaa kabisa, acha nisiandike maana nikiandika ntajaza kitabu.

4. Bar zisizo na mpangilia maalum, yaank zimetapakaa kila mahali, kelele za walevi na midundo ya muziki mkubwa mpaka alfajiri.

5. Uchafu. Mitaani uchafu umejaa kibao. Wakazi wanakusanya, magari ya kuzoa hayaji, malundo ya taka zinazotoa harufu mbaya yanaongezeka kila siku.

6. Usafiri. Daladala. Mabasi mengi machafu, mabovu, makonda wachafu na madereva wachafu. Daladala zinafunja sheria barabarani kila siku na matrafiki wapo tu. Dala dala hazitoshi watumiaji wa huu usafiri ni wengi mno, na wanaongezeka kila siku.

7. usafiri. Mwendo kasi. Hapa sitaandika, maana ntajaza kitabu.

8. Umeme. Umeme unakatika mara kwa mara, na ukirudi kuna wakati unarudi na nguvu kibwa mpaka vifaa vya majumbani vinaungua. Lakini wananchi wanakaa kimya tu wanamwachia Mungu.

9. Maji. Mabomba ya dawasa yanavuja sehemu kibao na upotevu wa maji ni mkubwa, japo wanajitahidi kuudhibiti, lakini bado wanahitaji kuongeza juhudi.

10. Malori ya mchanga na kokoto pamoja na mizigo. Haya yanaongoza kwa kutoa nafsi za watu hasa nyakati za usiku. Wenyewe wanasema usiku wananunua njia, kwaiyo ama zao ama zako.

Ongezea zako.
 
Habari zenu wadau.

Moja kwa moja twende kwenye mada husika. Nakusihii na kukushauri ewe uliepo huko mikoani usitamani wala kufikiria kuja Dar es Salaam. Jiji la Dar es Salaam kwa sasa limekuwa na kero nyingi sana zinazo fanya kuonekana kuwa chungu kwa wananchi.

Kero ziko nyingi ila binafsi ningependa kuzungumzia kero ya usafiri. Usafiri umekuwa ni shida sana katika jiji hili iwe asubuhi, mchana na jioni ndio tabu kweli kweli. Usafiri umekuwa shida sana kiasi kwamba ukienda katika vituo vya daladala kama vile Mbagala, Kariakoo, Banana, mawasiliano nakadhalika wananchi wamekuwa wakigombea usafiri.

Hii ni kero kubwa sana hasa kwa ndugu zetu walemavu, wazee wasiojiweza, wajawazito pamoja na mama wenye watoto wachanga. Kero hii pia imewaathiri kwa kiwango kikubwa wanafunzi, kundi hili limekuwa likichelewa kufika kwa wakati katika maeneo yao kero kubwa ikiwa ni usafiri.

Kwa hiyo kama unakuja Dar es Salaam ujue kuna kadhia ya usafiri.


Mamlaka husika chali
 
DSM ina fursa nyingi kuliko mikoa yote TZ, Dar es Salaam ina miundo mbinu ya hali ya juu kuliko mikoa yote TZ, DSM ina watu wengi kuliko majiji yote Africa mashariki, DSM kuna warembo kuliko eneo lolote TZ DSM in majengo mazuri kuliko maeneo yote TZ, usafiri ni issue ndogo sana kama vp si mtu aje tu awe anapanda bodaboda na mwendokasi
 
Dar ni basi tu,hua nashangaa kumuona mkuu wao wa mkoa anagombana na watu kwa issue zisizo za msingi wkt dar yake ina matatizo mengi,mengi,mengi,mengi,mengi,mengi,mengi sana ikiwepo Usafiri na usafi wa jiji.

Anyway ngoja wanyonge tukae pembeni.
Kumbe yapo mambo inabidi afuatilie, usafiri, usafi n.k
 
Back
Top Bottom