Kampuni ya uwekezaji NICOL ipo hai??

mgomba101

JF-Expert Member
Oct 21, 2011
1,817
706
Hii kampuni ilikuja kwa mbwembwe! Oooh tumekuja kuwakomboa wazawa nao wamiliki uchumi wa nchi yao! oooh tunawaacha wageni wanafaidika na rasilimali zetu.

Oooh hii kampuni ina inaongozwa na wazawa tena wazalendo wa INJII hii akina mzee mengi,mosha na m/kiti wa wazee wa Dar es salaaam ndugu Idd simba! Kilipanda! kilishuka!

Wabongo kama kawaida yao waliingia kichwakichwa kununua HISA mithili ya kununua tiketi za kamari ya BINGO au mithili ya kupanda mbegu DESI.
 
Ilishakufa muda mrefu, inadaiwa madeni kwa wingi sana. Sina uhakika kama wa TZ wana walionunua hisa walipatataarifa za kufirisiwa kwani ilitangazwa kwenye magazeti. Sielewi nini kilichoisibu, kwani wakati inaanza manjojo yalikuwa mengi sana, mpaka jamaa walisafiri mikoani kuitangaza, sijui nanianahusika na hasara hii au ndiyo KODI zetu walala hoi?
 
Ilishakufa muda mrefu, inadaiwa madeni kwa wingi sana. Sina uhakika kama wa TZ wana walionunua hisa walipatataarifa za kufirisiwa kwani ilitangazwa kwenye magazeti. Sielewi nini kilichoisibu, kwani wakati inaanza manjojo yalikuwa mengi sana, mpaka jamaa walisafiri mikoani kuitangaza, sijui nanianahusika na hasara hii au ndiyo KODI zetu walala hoi?

By Samuel Kamndaya, The Citizen Reporter
Dar es Salaam. The National Investments Company Limited (Nicol) has been delisted from the Dar es Salaam Stock Exchange (DSE).According to a DSE announcement, the company is officially out of the list of firms that trade their shares at the 13-year-old bourse.

"The DSE wishes to inform the public that as per DSE Governing Council directive issued on 31st May, 2011, the National Investments Company Limited (Nicol) has been delisted from the DSE, effective 6th June 2011," reads a statement posted on the DSE website.

This decision comes in the wake of Nicol's non-compliance with the country's listing obligations.

"In the first place, Nicol has not presented to us its audited financial statements for the past two years (2009 and 2010)…..the company has also been making some serious decisions without seeking the consent of the DSE as required by any listed company…..we understand that existing investors will now find it difficult to exit from the company, but we had no option but to take that step," the DSE chief executive officer (CEO), Mr Gabriel Kitua, told The Citizen yesterday.
 
watu washalizwa ...MWALIMU WA WATU...Pascaly Mayenga ashalalamika sana kwenye makala zake....Hii ndo Bongo akili kumkichwa
 
Hii kampuni ilianzishwa kwa nia nzuri kabisa, tatizo uendeshaji wake ulikuwa na matatizo.Kampuni hii ilikuwa njia murua kabisa kushiriki kuendesha uchumi wa nchi kwa njia ya kununua hisa kwenye miradi mikubwa inayoendeshwa na wageni kama uchimbaji wa madini,mabenki,ujenzi wa vitega uchumi kwa mtindo Build Own Transfer(BOT) n.k
 
mimi mwenyewe nilinunua hisa 2500. siku moja hisa zile nikazipeleka kuziuza pale DSE, Ilikuwa 2011 march, huwezi kuamini walinifukuza kama mwizi, nikajiuliza pesa zangu ndiyo zimeliwa na wajanja? hakikg iliniumiza sana, nikachapa lapa maka head office pale raha tower, nyimbo zikawa nyingi.. sasa nimesamehe
 
Wana JF nashindwa kuwapata NICOL kwenye Mtandao katika wiki yote hii. Je wamefilisika mpaka wameamua kuifunga tovuti yao. Nawadai HISA zangu.
 
Habari zenu Wanajanvi. NICO ni Kampuni ambayo ilikuja kwa kishindo kikubwa na kuweza kuushawishi umma kuwa ni kampuni ya ukusanyaji mitaji na kuiwekeza kwa niaba ya wanahisa. Wengi tulishwishika na wengi walinunua hizo hisa.

Wakati wanaanza ofisi zao zilikuwa pale Raha Towers ghorofa ya 4. Ni makutano ya Barabara ya Bibi Titi na Azikiwe. Ila baadae, inaonekana walihama. Ninachokiomba kwenu, ni kunijuza hawa jamaa kwa sasa ofisi zao ziko wapi? Inaonekana hata tovuti yao ilishafungwa. Hivyo hakuna taarifa ya msingi inayopatikana kwa ktumia nyenzo za kisasa.

Tafadhali inayefahamu walipo (Physical Address), anijuze.
 
NICOL wana interim management yaani uongozi wa mpito; ofisi zao zimehamia sehemu ya mikocheni barabara ya serengeti [ directly kwenye junction na Lucy Lameck road]. simu zao ni 2701323 na 2701436.
 
tafuta leso a.k.a handcatchif ya kufutia machozi kabla hujajibiwa waliko Nicol

dah! umenifurahisha sana sista watu wengi walilia sana kuhusu sakata la NICOL na wengine wapo humu jf sijui watasemaje wakiiona hii thread?!!!
 
Wewe unahoji NICOL? Kumbuka kuna PRESICIONAIR walitangaza kuuza HISA kwa mbwembwe nyingi! watu tukanunua kwa wingi!! baada ya kukusanya mamilioni ya walala hoi wameingia mitini! kimyaaaaa! leo mwaka wa tatu hatujui kinachoendelea! MAJANGA Tupu.
 
Niko wako msasani kwa mwalimu nyerere. Tafuta mwananchi ya leo au jana wametangaza kuwa wamehamia hapo kuanzia last monday
 
Reginald Mengi alikuwa mwenyekiti wa kamati ya uwekezaji Nicol. Nicol ikanunua kiwanda cha mdogo wake Benjamin Mengi, kwa mabilioni bila kufanya due-diligence, dili nzima ilikwenda kimagumashi juu kwa juu, kumbe kiwanda chenyewe mufilisi, Nicol ikala bonge la hasara. Badala ya Mengi kushtakiwa, wabongo wanamgwaya!
 
Back
Top Bottom