binti kiziwi
JF-Expert Member
- Aug 4, 2014
- 15,392
- 41,849
Bongo bongo tu, Shabiby imejijengea heshima sana kati ya makampuni ya usafirishaji nchini, lakini kuna watu wanaiharibu sana. Ikitokea ukapata safari ya gafla na hujafanya booking hasa kwa ubungo, ukienda kuulizia ticket tuseme gari la muda fulani unaambiwa limejaa halafu anajitokeza mtu anakuvuta pembeni kuwa nina ticket moja ila inabidi uipandie dau, gari ya 35k atataka 45k, gari ya 25 atataka 35k. Na hapo unakuta anaticket 7 kwenye mfuko wa shati na hazijaandikwa details zozote.
Hongera kwa waliopo stendi ya Shabiby dodoma, ukifika kama ticket zimeisha wanasema kabisa zimeisha na hawana namna labda usubiri mida ya majeruhi kama kuna mtu ataahirisha safari.
Hongera kwa waliopo stendi ya Shabiby dodoma, ukifika kama ticket zimeisha wanasema kabisa zimeisha na hawana namna labda usubiri mida ya majeruhi kama kuna mtu ataahirisha safari.