Kampuni ya mabasi ya Shabiby ni wahuni

Kampuni ya mabasi ya Shabiby ni wahuni

maroon7

JF-Expert Member
Joined
Nov 3, 2010
Posts
11,341
Reaction score
15,842
Hii kampuni nilikua naamini ni kampuni inayojiheshimu ila leo ndio nimewadharau na sitokaa nipande tena mabasi yao.

Leo nimesafiri na basi lao namba T 132 DLC toka Dar kwenda Arusha cha ajabu tumefika moshi wakatuweka kama nusu saa kisha wakatuambia wameahirisha hawafiki Arusha wanaishia Moshi.

Wakatufaulisha kwenye libasi libovu limetoka vijijini na bahati mbaya basi lilikua limejaa tukabishana nao sana wakadai tusimame asietaka ashuke.

Kuna wamama walikua na watoto wamelalamika mno na wengine wakaamua kutafuta usafiri mwingine. Binafsi pia niligoma kusimama basi limejaa mno.

Kudhihirisha sio bahati mbaya ni uhuni kwanza walituchelewesha sana pale Same baada ya abiria kwenda kulalamika kwa polisi wamelipa nauli mara mbili na wqmegoma kurudishiwa.

Hao abiria walikua wanne mmoja aliwalipia wenzake watatu na wao bila kujua wqmelipiwa wakalipa tena baadae walipogundua wakadai refund Shabiby wakagoma ndio kisa cha kutuchelewesha tena lisaa lizima pale Same.

Hawa jamaa ni wahuni kupitiliza tofauti na wanavyoonekana na basi zao kuvutia.
 
Hadi shabibi wameanza huu ushenzi?

Cc Unforgetable
Yaani mkuu waneniharibia safari yangu kabisa,afu nilikua sijawahi panda kwa hii route ya Dar - Arusha leo nilipoona basi lao nikapanda sababu ya heshima yao...nilikuaga napanda Dom - Arusha tu na ndio hawanipati tena
 
Hizi taarifa zilipaswa zimfikie boss wao,
Mtu unaajiri watu ukitarajia wakuboreshee biashara kumbe wanakuharibia, half ukifukuzwa unaanza kulalama.
mtu hana kazi kupata tu utingo unaanza maringo na manyanyaso unasahau utokako, mimi hii mijitu inanikera basi tu, na hamna sehem nakuaga mkali kama hz,

Umaskini una consequences nying sana
shenzi zao
 
Gari zina siti 50 inakuwaje ticket zikakatwa nyingi wakati manifest idadi ni 50
 
Hizi taarifa zilipaswa zimfikie boss wao,
Mtu unaajiri watu ukitarajia wakuboreshee biashara kumbe wanakuharibia, half ukifukuzwa unaanza kulalama.
Ntahakikisha zinafika maana nikifika home lazima niwaandikie kwenye website yao. Nilitaka kwenda kituoni hapa moshi nikaona ntajichelewesha ila si mbaya hata arusha naweza enda kuwasemelea
 
Ntahakikisha zinafika maana nikifika home lazima niwaandikie kwenye website yao. Nilitaka kwenda kituoni hapa moshi nikaona ntajichelewesha ila si mbaya hata arusha naweza enda kuwasemelea
Abiria mlifanya makosa, mlitakiwa kuwapigia simu Polisi au Sumatra ili wasimamizi wa hilo basi wapewe haki yao.
 
owner wanakuwa hawajui
ungetaja basi no na saa ngapi mliondoka Dar
labda owner atawa trace watu wake
 
Hii kampuni nilikua naamini ni kampuni inayojiheshimu ila leo ndio nimewadharau na sitokaa nipande tena mabasi yao. Leo nimesafiri na basi lao namba T 132 DLC toka Dar kwenda Arusha cha ajabu tumefika moshi wakatuweka kama nusu saa kisha wakatuambia wameahirisha hawafiki Arusha wanaishia Moshi. Wakatufaulisha kwenye libasi libovu limetoka vijijini na bahati mbaya basi lilikua limejaa tukabishana nao sana wakadai tusimame asietaka ashuke. Kuna wamama walikua na watoto wamelalamika mno na wengine wakaamua kutafuta usafiri mwingine. Binafsi pia niligoma kusimama basi limejaa mno.
Kudhihirisha sio bahati mbaya ni uhuni kwanza walituchelewesha sana pale Same baada ya abiria kwenda kulalamika kwa polisi wamelipa nauli mara mbili na wqmegoma kurudishiwa. Hao abiria walikua wanne mmoja aliwalipia wenzake watatu na wao bila kujua wqmelipiwa wakalipa tena baadae walipogundua wakadai refund Shabiby wakagoma ndio kisa cha kutuchelewesha tena lisaa lizima pale Same. Hawa jamaa ni wahuni kupitiliza tofauti na wanavyoonekana na basi zao kuvutia.
Ni wahuni sana, mabasi mabaya, hawana customer care, usafiri wa uhakika ni Abood Bus
 
Msingeshuka mkuu. Sema abiria wa kibongo asilimia kubwa hatunaga ushirikiano.
Kweli kabisaa,wote wangeamua moja na kukomaa wangefika mbona huko Arusha,wasingekubali kushuka huku wengine wakiwasiliana na kituo cha polisi hapo walipo,haya mambo ya kihuni sio wakati wake huu sasa kwa karne hii asee,.
 
Back
Top Bottom