Miss Zomboko
JF-Expert Member
- May 18, 2014
- 4,501
- 9,279
KAMPUNI ya Independent Power Tanzania Limited (IPTL), imeiomba Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam itamke rasmi kwamba Standard Chartered Bank (Hong Kong) Limited (SCBHK), si wadai wake na ibatilishe tuzo mbalimbali, ambazo ilipewa huko Ulaya bila kuwepo mhusika mkuu katika migogoro hiyo.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa IPTL, Joseph Makandege, kampuni yake inaidai SCBHK fidia ya Dola za Marekani billioni 3.240 (Sh.trilioni 6.5).
Kampuni ya IPTL haijawatambua SCBHK kama wadai wake na inahoji mahakamani uhalali wa madai yao hayo.
Kampuni ya IPTL imeifungulia SCBHK kesi mbalimbali za madai ikiwamo namba 60/2014, namba 801 na 802/ 2016, na kesi za biashara namba 67 na 75/2017 zinazoendelea katika Mahakama Kuu ya Tanzania, Dar es Salaam.
Imeeleza kustaajabishwa na taarifa zilizochapishwa kwenye vyombo vya habari nchini, kwamba SCBHK imepata tuzo ya Dola za Marekani 185,449,440 (Sh. 426,533,712,000) dhidi ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, katika kesi ya usuluhishi namba ARB/05/04 / 2015 katika Baraza la Kimataifa la Utatuzi wa Migogoro ya Uwekezaji London, Uingereza (ICSID).
Makandege aanasema IPTL pia imepokea tamko la serikali kupitia vyombo vya habari, lililotoa msimamo kwamba Serikali na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) haziwajibiki kuilipa SCBHK fedha hizo; kwamba serikali si mdaiwa bali ni mdhamini tu katika masuala ya IPTL; kwamba mdaiwa anayewajibika kulipa fedha hizo ni IPTL; na kwamba IPTL ilitoa kinga inayoikinga serikali na taasisi zake dhidi ya madai yoyote yatokanayo na IPTL kupewa fedha zilizokuwa katika iliyokuwa “Tegeta Escrow Account” katika Benki Kuu ya Tanzania (BoT).
Kimsingi, IPTL tunakubaliana na msimamo huo wa serikali. Tunatambua kwamba, kama mdhamini wake, serikali haiwajibiki kuilipia madeni yake, jukumu hilo ni lake. Serikali inawajibika tu kusimamia na kuhakikisha kwamba IPTL inalipa madeni yake yote halali inayodaiwa na wadai wake, deni hilo la SCBHK likiwamo, kama kweli ni deni halali la IPTL.
Hata hivyo, madai na tuz0 hiyo ya SCBHK ni miongoni mwa masuala ambayo bado yanabishaniwa na ambayo IPTL bado ina haki ya kuyahoji na fursa ya kuyabatilisha mahakamani. SCBHK pia bado inapaswa kuthibitisha uhalali wa tuzo hiyo katika mahakama za Tanzania. Maamuzi ya Mahakama za Tanzania (Mahakama Kuu na Mahakama ya Rufani, kama yeyote atakayekata rufani) ndiyo yatahitimisha mzozo kama kweli SCBHK ni mdai halali wa IPTL au vinginevyo.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, IPTL hatimaye itashinda katika mashauri yake hayo, SCBHK yaweza kupoteza kabisa uhalali wa kuendelea kuibughudhi IPTL na serikali kwa madai yake au yaweza kukata deni lake hilo Sh. bilioni 426.53 katika Sh. trilioni 6.5 inazodaiwa na IPTL na kuilipa IPTL kiasi kitakachobakia.
Na hatakama hatimaye itashindwa katika mashauri yake hayo, IPTL haitashindwa kulipa deni hilo la SCBHK; kwani kiwanda na rasilimali zake zingine zinatosha kuuzwa na kulipia madeni yake sambamba na hilo la SCBHK. Na hata kama hatimaye, mazungumzo yatahitajika, IPTL (siyo Serikali) ndiyo itazungumza na kukubaliana na SCBHK, kwani IPTL na SCBHK ndiyo wadau katika mashauri husika, wenye haki na wajibu huo.
“Katika muktadha huo, IPTL inakubaliana na inaunga mkono kwa dhati msimamo wa serikali na inaahidi kufanya kila liwezalo kulipa madeni yake, lakini inaomba iwezeshwe kufanya hivyo kwa kulipwa madeni yake na kurudishiwa leseni yake ya kufua na kusambaza umeme wa bei nafuu na wa uhakika kwa maendeleo ya Watanzania na Taifa zima katika uchumi wa viwanda,” ulisema.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa IPTL, Joseph Makandege, kampuni yake inaidai SCBHK fidia ya Dola za Marekani billioni 3.240 (Sh.trilioni 6.5).
Kampuni ya IPTL haijawatambua SCBHK kama wadai wake na inahoji mahakamani uhalali wa madai yao hayo.
Kampuni ya IPTL imeifungulia SCBHK kesi mbalimbali za madai ikiwamo namba 60/2014, namba 801 na 802/ 2016, na kesi za biashara namba 67 na 75/2017 zinazoendelea katika Mahakama Kuu ya Tanzania, Dar es Salaam.
Imeeleza kustaajabishwa na taarifa zilizochapishwa kwenye vyombo vya habari nchini, kwamba SCBHK imepata tuzo ya Dola za Marekani 185,449,440 (Sh. 426,533,712,000) dhidi ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, katika kesi ya usuluhishi namba ARB/05/04 / 2015 katika Baraza la Kimataifa la Utatuzi wa Migogoro ya Uwekezaji London, Uingereza (ICSID).
Makandege aanasema IPTL pia imepokea tamko la serikali kupitia vyombo vya habari, lililotoa msimamo kwamba Serikali na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) haziwajibiki kuilipa SCBHK fedha hizo; kwamba serikali si mdaiwa bali ni mdhamini tu katika masuala ya IPTL; kwamba mdaiwa anayewajibika kulipa fedha hizo ni IPTL; na kwamba IPTL ilitoa kinga inayoikinga serikali na taasisi zake dhidi ya madai yoyote yatokanayo na IPTL kupewa fedha zilizokuwa katika iliyokuwa “Tegeta Escrow Account” katika Benki Kuu ya Tanzania (BoT).
Kimsingi, IPTL tunakubaliana na msimamo huo wa serikali. Tunatambua kwamba, kama mdhamini wake, serikali haiwajibiki kuilipia madeni yake, jukumu hilo ni lake. Serikali inawajibika tu kusimamia na kuhakikisha kwamba IPTL inalipa madeni yake yote halali inayodaiwa na wadai wake, deni hilo la SCBHK likiwamo, kama kweli ni deni halali la IPTL.
Hata hivyo, madai na tuz0 hiyo ya SCBHK ni miongoni mwa masuala ambayo bado yanabishaniwa na ambayo IPTL bado ina haki ya kuyahoji na fursa ya kuyabatilisha mahakamani. SCBHK pia bado inapaswa kuthibitisha uhalali wa tuzo hiyo katika mahakama za Tanzania. Maamuzi ya Mahakama za Tanzania (Mahakama Kuu na Mahakama ya Rufani, kama yeyote atakayekata rufani) ndiyo yatahitimisha mzozo kama kweli SCBHK ni mdai halali wa IPTL au vinginevyo.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, IPTL hatimaye itashinda katika mashauri yake hayo, SCBHK yaweza kupoteza kabisa uhalali wa kuendelea kuibughudhi IPTL na serikali kwa madai yake au yaweza kukata deni lake hilo Sh. bilioni 426.53 katika Sh. trilioni 6.5 inazodaiwa na IPTL na kuilipa IPTL kiasi kitakachobakia.
Na hatakama hatimaye itashindwa katika mashauri yake hayo, IPTL haitashindwa kulipa deni hilo la SCBHK; kwani kiwanda na rasilimali zake zingine zinatosha kuuzwa na kulipia madeni yake sambamba na hilo la SCBHK. Na hata kama hatimaye, mazungumzo yatahitajika, IPTL (siyo Serikali) ndiyo itazungumza na kukubaliana na SCBHK, kwani IPTL na SCBHK ndiyo wadau katika mashauri husika, wenye haki na wajibu huo.
“Katika muktadha huo, IPTL inakubaliana na inaunga mkono kwa dhati msimamo wa serikali na inaahidi kufanya kila liwezalo kulipa madeni yake, lakini inaomba iwezeshwe kufanya hivyo kwa kulipwa madeni yake na kurudishiwa leseni yake ya kufua na kusambaza umeme wa bei nafuu na wa uhakika kwa maendeleo ya Watanzania na Taifa zima katika uchumi wa viwanda,” ulisema.