Atlantis
JF-Expert Member
- May 24, 2015
- 383
- 514
Kampuni kubwa ya vifaa vya kielektroniki duniani Apple, inasemekana imeiba mawazo ya wapinzani wake kama Samsung, Google na Microsoft ili kufanya maboresho katika software platforms za bidhaa zao kama iPhone na Tablets.
==============================
Chanzo: wordpress
==============================
Kampuni ya Apple Yaiba Mawazo 6 ya Washindani Wake
![]()
Kampuni kubwa ya vifaa vya kielektroniki duniani Apple, inasemekana imeiba mawazo ya wapinzani wake kama Samsung, Google na Microsoft ili kufanya maboresho katika software platforms za bidhaa zao kama iPhone na Tablets.
Ni dhaihiri kwa baadhi ya wapenzi sugu wa bidhaa za Apple features hizo zitaonekana kama mawazo mampya toka Apple lakini kwa wazoefu na watumiaji wengine wanaweza kufahamu fika kabisa kwamba si kitu kipya!
Features hizo zimekuwa updated na Apple ni katika matoleo mapya kabisa ya iOS, OS X, watchOS na Apple Music.
Features hizo ni kama zifuatazo:
1) Public Transit Information (toka Google)
Iko wazi kuwa Google Maps ndiyo Software ya kwanza kabisa duniani katika masuala ya ramani (hata kwenye semu za Apple zenyewe kuanzia I-phone 5 kushuka chini). Moja wapo ya sababu ni kwamba Google inatoa live public transit information.
Jumatatu iliyopita, Apple ilitangaza kuwa itafanya maboresho katika Apple Maps ambayo imekuwa na matatizo kwa muda mrefu sasa. katika maboresho hayo itaweka feature mpya ambayo ni Eureka – ambayo na yenyewe itakuwa inatoa live public transit information. Feature ambayo imeiiba kutoka Google Maps.
![]()
Apple Maps (kushoto) and Google Maps (kulia).2) Multi-Tasking Tablets (toka Microsoft Surface)
![]()
Microsoft Surface (juu) na iPad yenye iOS 9
(chini).iPad zilizo na mfumo wa kuongoza wa iOS 9 zinamuwezesha mtumiaji wa kifaa hicho kuweza kfungua applications mbili kwa wakati mmoja yaani multi-tasking zimepokelewa kwa shangwe na wadau mbalimbali wa msuala ya teknolojia.
wazo hili kwanza lilibuniwa na Microssoft kwenye mfumo wao wa kuongoza kompyuta wa wa Windows 8 na kwa kitambo kirefu sana!
Hata hivyo, feature hii itaboreshwa zaidi katika Windows 10, ambapo mtumiaji wa kifaa chochote kinachotumia mfumo huu ataweza kubadilisha ukubwa wa muonekano wa application iliyofunguliwa katika screen yake.
3) Picture-in-picture video (Kutoka Samsung Galaxy Note).
![]()
Samsung Galaxy Note II (kushoto) na iPad yenye iOS 9 (kulia).
Apple pia imejibosti kwa feature yake nyingine mpya ya picture-in-picture kwa kifaa chake cha iPad Jumatatu hii. Ni nzuri lakini ukweli ni kwamba feature hii ilishakuwepo katika simu za Samsung Galaxy Note na tablets kwa muda mrefu sasa.
Kwa upande mwingine, feature hii katika Android inamuwezesha mtumiaji kucheza video files za kawaida na si kutumia applications za TV za moja kwa moja yaani live. Kitu ambacho katika Apple wameboresha na kufanya iwezekane katika bidhaa zao.
4) Contextual searches (Google Now on Tap)
![]()
Now on Tap ya Android (kushoto) na Siri kwenye iOS 9 (kulia).
Wiki mbili tu zilizopita, Google ilizindua feature mpya iitwayo Google Now, kama Siri mpya, toleo hili jipya la Android voice assistant inaweza kupitia barua-pepe zako au jumbe fupi za maneno na hata kufanya makumbusho au reminders za matukio ambazo za kalenda ambazo mtumiaji mwenyewe anaziweka.
Na huduma hizi mbili za Apple na Google zinaweza kufanya uchambuzi wa mazingira kwa amri za sauti yaani voice commands.
Hii inamaanisha kuwa, wakati unaperuzi tovuti yenye habari kuhusu mlima Kilimanjaro, mtumiaji unaweza kuuliza "Itanichukua muda gani mpaka kileleni?" na itakupa jibu sahihi kwa maneno. Ndo mambo ya Artificial Intelligence hayo!
5. Smarter watch faces (Kutoka Android Wear)
![]()
Navigation kwenye Apple Watch (kushoto) na navigation on Android Wear (kulia).
Apple imekuwa ikizindua watchOS kuongeza mambo kama vile uwezo wa kubadili muonekano wa uso wa saa hii kulingana na matakwa ya mtumiaji (custom photo watch faces) na navigation kulingana na uelekeo wa mtumiaji (turn-by-turn navigation), lakini features hizi zilikuwepo katika Android kwa kitambo sasa.
6) Apple Music (Kutoka Beats Music)
![]()
Beats Music (kushoto) naApple Music (kulia).
Ingawa Apple ilinunua Kampuni hii ya Beats Music kwa $3 bilioni, imeweza kuchukua vitu vingi kutoka kwake. Muonekano wake na navigation nzima imefanana kabisa na aplication hiyo.
Chanzo: wordpress