BigTall
JF-Expert Member
- Mar 9, 2022
- 654
- 1,598
“Kwanza niwapongeze kwa kutambua tuliharibu misitu huko nyuma na tuna wajibu wa kuirudishia. Ninatamani programu kama hii ya upandaji na utunzaji miti unaofanywa na gereza la Wilaya la Njombe uigwe na magereza nyingine zote nchini,” amesema Haule.
Kwa upande wake Mhandishi Emmanuel Yesaya akimwakilisha Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati vijijini (REA), amesema zaidi ya hekta 470 zinakatwa kila mwaka kwa ajili ya matumizi ya nishati zisizo safi za kupikia huku watanzania zaidi elfu 33 wanafariki kutoka na matumizi ya nishati zisizo safi za kupikia.
Kwa upande wake Mkuu wa Magereza Mkoa wa Njombe, Kamishna Msaidizi wa Magereza, Joseph Mkude amewataka maafisa pamoja na askari wa jeshi hilo kuwa mabalozi wa nishati safi ya kupikia.