Kampeni ya Kuhamia Dodoma na Kufuta Sitting Allowances

Kampeni ya Kuhamia Dodoma na Kufuta Sitting Allowances

PM na Mawaziri wanao ofisi zao Dar es Salaam, hawawezi kukaa majimboni. Vipi kuhusu wabunge, si wanatakiwa kuwa na ofisi zao majimboni (katika hali ya kawaida)?...

Hata PM na mawaziri wengine ni wabunge.
 
Kwa mtizamo wangu, nafikiri huu ndio wakati muafaka kwa serikali kuhamia Dodoma, kwa sababu zifuatazo;

  1. Dodoma ni katikati ya nchi na miundombinu ya usafiri ni mizuri toka kila kona ya Tanzania
  2. Serikali ikihamia Dodoma,msongamano wa magari utapungua DSM
  3. DSM imejaa,ni rahisi kuandaa mji wa kisasa Dodoma kwa kuwa bado kuna maeneo ya kutosha kuliko DSM
  4. Dodoma ni eneo kame,linafaa kwa shughuli za kimjini-mjini ambazo hazitaki mvua
  5. Kwa mikakati ya kiusalama, mji ulio katikati ya nchi unafaa zaidi nao ni Dodoma
  6. Ni rahisi kutatua tatizo la maji safi na maji taka Dodoma kuliko DSM
  7. Kama katiba ya wananchi yenye muundo wa serikali tatu itaja-pitishwa, basi Dodoma itakuwa makao makuu ya serikali ya Tanganyika, Zanzibar makao yake makuu yatakuwa Unguja,na DSM itakuwa makao makuu ya serikali ya shirikisho. Wakati tukisubiri serikali ya shirikisho kuzaliwa,ni bora ikulu yao ya Magogoni ikaanza kukarabatiwa.Rais wa serikali iliyovaa koti la muungano aende Dodoma nyumbani kwake.

Kama Magufuli ataamua kuhamia Dodoma, atakuwa amefanya uamuzi mwingine wa hekima na busara, utakaosaidia kusukuma mbele maendeleo ya taifa hili.HAPA KAZI TU!
 
Huwa najiuliza ni kiasi gani kinatumiwa na watumishi wa serikali kila mwaka kutoka na kurud dodoma to dar wanapohudhuria vikao vya bunge kila mwaka zaidi ya mara tatu. Hizo gharama za mafuta..posho.. na kupoteza muda wa safari njiani ni bilikn ngap
 
Wakifuta wahakikishe wanafunzi wa vyuo vya UDOM, CBE na St. John wanapewa mikopo... Soko lao litashuka sana
 
PM na Mawaziri wanao ofisi zao Dar es Salaam, hawawezi kukaa majimboni. Vipi kuhusu wabunge, si wanatakiwa kuwa na ofisi zao majimboni (katika hali ya kawaida)?...

Wanazo....in fact rasimu ya warioba ilitaka wabunge waishi majimboni.
 
Back
Top Bottom