Kampeni ya ‘Anzia Ulipo’yazinduliwa rasmi Dodoma

Kampeni ya ‘Anzia Ulipo’yazinduliwa rasmi Dodoma

News TZ

Senior Member
Joined
Jun 17, 2015
Posts
169
Reaction score
88
ANZIA ULIPO LAUNCH DODOMA-68.JPG

Mkurugenzi wa Yas Kanda ya Kati, Said Idd (katikati), Meneja wa Yas Kanda ya Kati Frank Anthony (kushoto), na Meneja wa Mixx by Yas Kanda ya Kati Charles Gasper (kulia) wakifurahia jambo wakati wa uzinduzi rasmi wa kampeni ya kitaifa ya “Anzia Ulipo” iliyozinduliwa jijini Dodoma Julai 16 mwaka huu.

KAMPUNI ya mawasiliano ya Yas imezindua rasmi kampeni yake ya ‘Anzia Ulipo’ jijini Dodoma, ikilenga kuwahamasisha wakazi wa Kanda yake ya Kati, kuanza safari yao ya maendeleo kwa kutumia kile walicho nacho.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Mkurugenzi wa Yas Kanda ya Kati, Said Idd amesema Kampeni hiyo inaakisi dhamira ya Yas, kutumia teknolojia kama nyenzo ya kuwawezesha Watanzania kujikwamua kiuchumi na kijamii.

Kujikwamua huko kumejikita hasa katika maeneo yanayoendelea kukua kwa kasi kama Dodoma na mikoa ya Kanda ya Kati.
“Tunazindua kampeni hii tukiwahimiza Wakazi wa Kanda hii kutambua kuwa hakuna muda mwafaka zaidi ya sasa.

“Mafanikio hayaangalii ukamilifu bali hatua ya kwanza na ujasiri wa kuanza,” amesema Idd.

Amesema, kampeni ya Anzia Ulipo imelenga kuwapa Watanzania motisha ya kutumia teknolojia katika kuboresha maisha yao na kufikia malengo binafsi.

Aidha, amesema tayari Yas imewekeza kwenye mtandao wa kisasa wa intaneti ya kasi (4G na 5G) ili kuhakikisha huduma bora zinapatikana hata maeneo ya pembezoni.

“Leo hii, mwalimu anaweza kufundisha darasa mtandaoni akiwa kijijini, mfugaji wa nyuki kufuatilia bei ya asali kwa kutumia simu, na kijana mbunifu hapa Dodoma kuonyesha kazi zake kwa dunia nzima. Haya yote yanawezekana kwa kutumia teknolojia,” ameeleza.
Katika hotuba yake, Idd pia amewashukuru wakazi wa Kanda ya Kati kwa kuzipokea chapa za Yas na Mixx kwa moyo mkunjufu, akibainisha kuwa mwitikio huo ni uthibitisho wa kiu ya wananchi kupata huduma bora, rahisi na zenye kuleta tija katika maisha yao ya kila siku.

Hata hivyo amesisitiza kuwa, Yas itaendelea kuwasaidia vijana, wakulima, walimu na wajasiriamali kwa kuzindua huduma na kampeni zinazowawezesha kukuza maarifa, kupanua mitandao yao ya biashara, na kufikia malengo kupitia majukwaa ya kidijitali.

“Tunafahamu changamoto za ajira rasmi, ndiyo maana tunatambua na kuunga mkono nguvu ya vijana wanaoamua kujiajiri kupitia ujasiriamali.

“Yas tunawaambia, msisubiri hali iwe kamilifu, anzeni pale mlipo. Ndoto zenu ni halali, uwezo wenu hauna kikomo, na fursa zipo. Tunachohitaji ni uthubutu,” amesema kwa msisitizo.
 
ANZIA ULIPO ARUSHA-225.JPG


Mkurugenzi wa Yas - Kanda ya Kaskazini Ndugu Henry Kinabo akizungumza wakati wa uzinduzi

KAMPUNI ya mawasiliano ya Yas imezindua rasmi kampeni yake ya ‘Anzia Ulipo’ jijini Arusha, ikilenga kuwahamasisha wakazi wa Kanda ya Kaskazini, kwa ajili ya kugusa maisha ya Watanzania na kuchochea ukuaji wa biashara ndogo na kunwa.

Lakini pia, kuthibitisha dhamira ya Yas na Mixx, kuhakikisha kuwa kila Mtanzania anapata nafasi ya kufanikiwa kupitia teknolojia.

Akizungumza katika hafla fupi mara baada ya kuzindua ‘Anzia Ulipo’ jijini Arusha, Mkurugenzi wa Yas Kanda ya Kaskazini, Henry Kinabo amesema maendeleo ya kweli ni yale yanayomgusa kila mtu bila kumwacha yeyote nyuma.
“Yas imekuwa mstari wa mbele katika kutambulisha kampeni na promosheni zinazogusa maisha ya watanzania moja kwamoja tukichochea ukuaji wa biashara ndogo na kubwa.

“Tunaamini kwa dhati kwamba maendeleo ya kweli ni yale yanayomgusa kila mtu bila kumwacha yeyote nyuma.

“Hivyo, tunapozindua kampeni ya Anzia Ulipo hapa jijini Arusha na kwa wakazi wote wa Kanda ya Kaskazini, tunathibitisha dhamira ya Yas na Mixx ya kuhakikisha kuwa kila Mtanzania anapata nafasi ya kufanikiwa kupitia teknolojia,” amesema Henry Kinabo.

Amesema, kupitia kampeni hiyo, wanatoa wito mahsusi kwa kila Mtanzania kuziona fursa zilizopo katika ulimwengu wa kidijitali na kuzichangamkia.

Aidha, amesema Yas inawahamasisha Watanzania kuanza safari yao ya mafanikio kwa kutumia kile walicho nacho – iwe ni kipaji, ujuzi, au hata wazo zuri bila kungoja wakati maalum.

“Tunawakumbusha Watanzania kuwa mafanikio hayahitaji ukamilifu bali uthubutu wa kuchukua hatua ya kwanza.Sisi Yas, tunaamini kwenye nguvu ya teknolojia.

“Tunakupa huduma na bidhaa mahsusi zitakazoendana na safari yako ya mafanikio. Tumewekeza katika mtandao wa kisasa wa 4G na 5G unaopatikana kila kona ya nchi, tayari kukusaidia kupiga hatua yako ya kwanza,” amesema.

Hata hivyo alisema, katika mazingira ambayo ajira rasmi bado ni changamoto, vijana wengi wamechagua ujasiriamali – si kwa sababu hawana njia nyingine, bali kwa sababu wana ndoto na malengo makubwa.

“Tumeshuhudia ongezeko la biashara zinazoendeshwa mtandaoni – kuanzia kilimo kidijitali, ubunifu wa mavazi, utengenezaji wa maudhui na huduma nyingine nyingi.
“Haya yote yakiongozwa na vijana waliothubutu kufikiri tofauti – wakitumia teknolojia kama chombo chao cha mafanikio,” amesema Kinabo.

Kampeni ya ‘Anzia Ulipo’ Kwa wakazi wa Kanda ya Kaskazini itajikita Arusha, Kilimanjaro na Manyara. ‘Sisi Yas tunasema wakati wako,wangu na wetu ni Sasa’.
 
Back
Top Bottom