Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 117,703
- 218,236
Taarifa inaonyesha kwamba Kamati ya Uchaguzi ya Klabu ya Simba imepitisha majina mawili ya kuwania Uenyekiti wa Simba , huku wagombea wengine wakienguliwa (sifahamu vigezo vilivyotumika ) , waliopitishwa ni Mangungu na Juma Nkamia , maana yake ni kwamba kati ya wawili hawa mmojawapo atakuwa Mwenyekiti wa Simba.
Simfahamu Mangungu kwahiyo sitamjadili .
Bali Juma Nkamia hana uwezo na wala hajawahi kuwa na uwezo wa kuongoza timu kubwa kama Simba , Nkamia ni mtu aliyejaa ubinafsi asiyeamini katika umoja , ni mtu wa majungu ambaye akipewa nafasi hiyo ataigawa Simba mapande mapande , hapaswi kupewa cheo kikubwa kama Uenyekiti wa Simba , Nkamia amekuwa kiongozi wa chini wa Simba miaka iliyopita , lakini tabia yake ya kuropokaropoka ilimfanya akang'olewa.
Pamoja na kuwa Mbunge katika bunge lililopita , lakini Nkamia hakuwa na ushawishi wowote ndani na nje ya bunge , hoja zake bungeni zilizimwa kama mshumaa jangwani , huku wananchi wa Jimbo lake wakiongoza kwa umasikini nchini Tanzania , mtu kama huyu hafai kuongoza timu ya Kimataifa kama Simba
Itaendelea...
UPDATES :
Ameangukia pua .
Simfahamu Mangungu kwahiyo sitamjadili .
Bali Juma Nkamia hana uwezo na wala hajawahi kuwa na uwezo wa kuongoza timu kubwa kama Simba , Nkamia ni mtu aliyejaa ubinafsi asiyeamini katika umoja , ni mtu wa majungu ambaye akipewa nafasi hiyo ataigawa Simba mapande mapande , hapaswi kupewa cheo kikubwa kama Uenyekiti wa Simba , Nkamia amekuwa kiongozi wa chini wa Simba miaka iliyopita , lakini tabia yake ya kuropokaropoka ilimfanya akang'olewa.
Pamoja na kuwa Mbunge katika bunge lililopita , lakini Nkamia hakuwa na ushawishi wowote ndani na nje ya bunge , hoja zake bungeni zilizimwa kama mshumaa jangwani , huku wananchi wa Jimbo lake wakiongoza kwa umasikini nchini Tanzania , mtu kama huyu hafai kuongoza timu ya Kimataifa kama Simba
Itaendelea...
UPDATES :
Ameangukia pua .